mchovu wa fikra
JF-Expert Member
- Jul 16, 2016
- 335
- 396
Ajira za mwaka huu ni kwa GPA maalum nayo ni kuanzia 3.5,je unayo? Kama huna jishughulishe na kazi nyingine sio Lazima serikali ikuajiri.Ila kwa ufahamu wangu wa haraka haraka wewe utakuwa mtoto wa Mkulima na kama sio basi mzee atakuwa anafanya biashara sokoni,ikiwa sivyo basi mzee wake ni dereva wa taxi na kama sio basi mzee wako ni mjanjamjanja tu wa mjini ila napo kama sio basi mzee wako ni mcheza bao vijiweni au mzee wa kahawa.Kwa upande wa pili baba zao ambao wanafanya kazi Tanesco,Nssf,NHIF,PPF,madaktari,wafanyakazi wa serikali ambao wana nafasi,na pia katika mashirika mbalimbali ya umma na binafsi wameshaajiriwa ila wewe bado,mshauri mzee wako atumie umaarufu wake na kufahamiana na watu ili uajiriwe na serikali.mimi mwenzio sina baba na hata marafiki wa marehemu baba yangu waliacha hata kunisalimia miaka 10 iliyopita nikiwa mtoto wa mtaa ila leo nimemaliza degree bado nakomaa mtaani na nishazoea hata nisipoajiriwa NITAKAMATA JEMBE KWA NGUVU ZANGU KWA KUWA SINA MSAADA MAISHANI MWANGU...! Laiti kama humu JF tungekuwa tunaonekana basi mimi ningedharaulika sana na hata mawazo yangu kutopata support.Kupitia JF najifunza mambo mengi sana.