Hivi ag werema na kombani wametumwa au kuna sababu nyingine?

roby m

Member
Nov 21, 2010
28
1
Nilishitushwa sana na kauli ya waziri wa sheria na katiba celina kombani
aliyoitoa wiki chache zilizopita kuhusu msimamo wake juu ya madai ya
katiba mpya sababu kubwa ikiwa,eti katiba iliyopo inakidhi mahitaji ya wananchi pia mchakato wa kuibadilisha unagharimu fedha nyingi na nchi haina fedha za kutosha kuendesha mchakato huo.
Nikajiuliza maswali maswali mawili,hivi fedha zinazotumia ktk safari za rais nje ya nchi,na zile zinazotumika kununua magari ya kifahari ktk serikali hii yakina kombani huku wakilindwa na katiba zinatoka wapi?
Pili nikayakumbuka yaliyotokea kwa majirani zetu wakenya nikasema hivi kipi bora damu za watu kumwagika kwa kupigania haki yao ya katiba kwa nguvu au hizo gharama ambazo serikali na kombani wake wanaziita gharama kubwa za mchakato wa katiba?
Jibu nililopata ni kuwa kombani anapenda sana siku moja akiona damu ya watanzania inamwagika kwa kudai haki yao..
ila kinachoendelea kunitisha zaidi ni hii kauli iliyotolewa hivi karibuni na anayeitwa mheshimiwa AG Frederick Werema akisema pia hakuna sababu ya kuandika katiba mpya badala yake iliyopo iwekewe viraka.matumaini na matarajio ya wengi yalikuwa ni kuona mwanasheria wao mkuu wa serikali akitoa kauli zinazojenga kwa ajili ya kuwatetea watanzania walio wengi,haya ona sasa kombani hajasomea maswala ya sheria na katiba hata wewe werema tusene nini sasa?
kutokana na kauli hizo zinazotolewa na hawa viongozi wa juu serikalini wanaohusiana kabisa na uwepo wa sheria na katiba unaonesha dhahiri sio mawazo yao bali wametumwa na kundi fulani la watu kwa maslahi binafsi,lakini kwa aliyewateua ambaye ni mheshimiwa rais kwa sababu sijaona akisimama kupinga kauli za watendaji wake wa kazi .
"Werema na Kombani mnashindwa kufikiri! sawa,lakini mnashindwa hata kutumia mawazo ya watu wengine?????????

:target:
 
Back
Top Bottom