Companero
Platinum Member
- Jul 12, 2008
- 5,605
- 1,704
1: Darasa Liloloungua na Kupelekea Selebriti Ahamie Pabliki Inglishi Midiamu
2. Mzambarau alioukwea Selebriti Nyani uko Pembeni ya Darasa Jipya
3. Bembea Zimeongezeka - Enzi za Selebriti Ngabu zilikuwa Chache Sana
----------------------------------------------------------------------------------
Katika matembezi yangu ya alfajiri huwa napita kwenye shule mbalimbali. Leo nimepita tena katika shule niliyosoma chekechekea. Maswali mbalimbali yalinijia kichwani hasa baada ya mwanafunzi wa zamani wa shule hiyo kudai kuna jengo liliungua. Cha ajabu tulikuwa tukicheza kwenye jengo hilo na kulitumia kama ulingo wa kupigania na kufanya mazoezi ya skauti. Nikiwa mdau nambari wani wa elimu Tanzania na mwanahistoria wa kujitegemea wa Taifa, ningependa kujua haya:2. Mzambarau alioukwea Selebriti Nyani uko Pembeni ya Darasa Jipya
3. Bembea Zimeongezeka - Enzi za Selebriti Ngabu zilikuwa Chache Sana
----------------------------------------------------------------------------------
1. Shule hii ilijengwa lini na nani?
2. Kwa nini iliitwa shule ya vidudu?
3. Nini kililiunguza jengo lake la awali?
4. Mbona siku hizi hawaruhusu kuingia?
5. Wadau gani maarufu wamefundwa hapo?
Bahati mbaya sikuweza kupiga picha kwa kuwa simu yangu haina kamera. Punde tu nitakapopata kamera nitapiga baadhi ya picha ili niweze kuzitumia kuuliza maswali vizuri zaidi. Wadau wa shule hiyo naomba mjimwage ukumbini kujibu maswali.