zitto junior
JF-Expert Member
- Oct 7, 2013
- 19,083
- 28,745
Nashukuru kwa maelezo yako ila kuna kitu sijui unapindisha au umesahau nachokubali kweli wahutu walichinja watutsi ila ni baada ya watutsi kuanza kuchinja wahutu walipokuwa wamevamia Rwanda.....Watutsi pengine wasingevamia rwanda kama wangekubaliwa haki yao ya kurejea kwenye nchi yao hata thread ni kama imeonesha hivo,walianza kuunda kikundi cha uasi baada ya kukataliwa kurudi rwanda na pia wakakataliwa kukaa uganda then wakajikuta stateless.Halafu ni kama huelewi maana ya genocide, genocide ni mauaji yanayofanywa kwa misingi ya kufuta uwepo wa kikundi flani kwa misingi ya dini au kabila au vitu kama hivyo so huwezi kusema kuna watu walifanya genocide kwa kujilinda,huwezi kusema kuna mtu/watu walifanya genocide kwa kujilinda kwa kuua mpaka kitoto kichanga cha siku moja au huwezi kusema kuna watu walifanya mauaji kujilinda kwa kuua raia wasiokuwa na silaha waliojificha mashuleni au makanisani.
Niweke rekodi vizuri ni kwamba walikufa watu 1,070,000 (UN) na statistics zilizopo ni kwamba watutsi mpaka vita inaanza walikuwa laki 7 na kwenye takwimu za UN inasema walipona watusi laki 3..... Sasa swali linakuja kma watutsi walikufa laki 4 kati ya vifo million 1 je hao laki 6 wengine ambao sio watutsi walikuwa kabila gani??? Si ni wahutu.....
Sasa basi kivp mseme genocide ni pale wahutu wanapoua watutsi ila mnasahau kuwa wahutu walikufa zaidi ya watutsi kwenye vita ile hilo ndio concern yangu mkuu