Informer
JF-Expert Member
- Jul 29, 2006
- 1,582
- 6,627
Mzungu wa kwanza kukanyaga Bukoba alikuwa ni Mjerumani Emin Pasha aliyewasili tarehe 31 Oktoba, 1890, ingawa miaka 30 kabla ya hapo Waingereza wawili, T.H. Speke na T.A Grant waliwahi kufika Karagwe na kukutana na Omukama Rumanyika l (Rugundu). Gavana wa kwanza wa kijerumani ni Julius von Soden (1891-1893) na wa mwisho ni Heinrich Schnee (1912-1916).
Gavana wa kwanza wa kiingereza ni Sir Horace Byatt (1916-1924) na wa mwisho ni Sir Richard Turnbull (1958-1961). Wahaya (wakiwemo Wanyambo) wanajulikana kama Western Interlacustrine Bantu. Walihama kutoka Uganda Magharibi katika karne za 15 na 16, hasa kutoka Bunyoro na Ankole. Koo nyingi asili yao ni Bunyoro na chache kama abamiilo/abagabo asili yao ni Ankole.
Kihanja, Ihangiro na Bukara Bakama wao ni Bahinda wakati wale wa Kiamutwara na Bugabo ni Bankango waliowaasi Bahinda na kujitangazia uhuru yapata mwaka 1820 wakati Mukama Kalemera II alipofariki. Uasi huu uliongozwa na Kitekere na baadaye kuimarishwa na mtoto wake Omukama Kaitaba (1860-1888).
Kiziba Rulers (title Omukama)
.... - .... Bike
.... - .... Kiziba Kizindo
.... - .... Ntumwa
.... - .... Kanyamaishwa
.... - .... Kibi I Nyakiiru Kaganda
.... - .... Ishamura-Njobe "elya Kiziba, elingome"
.... - .... Ishamura-Nyakabinga "elya Bunyoro"
.... - .... Wanumi
.... - .... Bwanamba
.... - .... Matwi
.... - .... Magembe I (1st time)
.... - .... Kashumba (regent?)
.... - .... Magembe I (2nd time)
.... - .... Muzinga
.... - .... Mwigara
.... - .... Burungu I
.... - .... Magembe II
.... - .... Mboneko I
.... - .... Nyarwangu
.... - .... Mulimpuzi -Regent
.... - .... Ruhangarazi I
.... - .... Nyarwangu II
.... - .... Rutajwaha
.... - .... Burungu II Kakinda
.... - .... Kibi II Rutahirwa
.... - 1870 Ruhangarazi II (d. 1870)
1870 - 1903 Mutatembwa
1898 - 1900 Rweshabura (in rebellion)
1903 - 1916 Mutahangarwa Karutasigwa
1916 - 1927 Edward George Mboneko II
1927 - 1937 William Mutakubwa
3 May 1937 - 6 Nov 1962 Nestor Lutinwa wa mwisho kusimikwa (kutendekwa)
Bakama wa Kiziba ukoo wao ni Baziba/Babiito. Baada ya kifo cha Mukama Burungu II (1800-1835) walipendelea kuitwa Abayobya. Sababu ni kwamba wanatokana na Omulangila Luyobya, mtoto wa Mukama Ruhangarazi I. Kutokana na ukatili uliopitiliza wa Burungu II, baba yake mdogo, Omulangila Luyobya, alishindwa kumvumilia na hivyo akaanzisha vita ya kumng’oa. Katika vita hii alisaidiwa sana na mtoto wake aliyeitwa Rutahilwa. Luyobya kwake kulikuwa ni Bukwali, Kanyigo.
Burungu II alijikuta katika hali ngumu ya kushambuliwa kutoka ndani na nje, kwani Bahyoza walikuwa pia wanamshambulia. Baada ya Burungu kuuawa na maadui mwaka 1835, Rutahilwa, mtoto wa Ruyobya alitawala na akapewa jina Kibi II. Baada ya Kibi II, alitawala mtoto wake Rugangarazi II (1858-1865), halafu Mutatembwa (1865-1903), aliyefuatiwa Mutahangarwa (1903-1916), kisha Mboneko II (1916-1926), halafu Mutakubwa (1926-1937), halafu Lutinwa (1937-1974).
Mutakubwa aliondolewa na wakoloni mwaka 1937 na hakuwa na mtoto. Hivyo ndugu yake Mboneko aitwaye Nestor Lutinwa alichaguliwa kumrithi, na akatawala mpaka Nyerere alipofutilia mbali utawala wa Bakama.
Sababu ya kuondolewa kwa Mutakubwa ni inadaiwa ni ufuska uliokithiri, ukiwemo ule wa kulazimisha mama yake Muchureza alijaribu kumkanya lakini hakusikia. Hivyo alikwenda kumuomba DC wa Kikoloni amsaidie kumkanya. Badala ya kumkanya DC alimfukuza, kwani kwa mzungu kubaka ni dhambi isiyosameheka. Lakini DC hakuelewa kuwa Mukama hawezi kuwa na hatia ya kumbaka mwanamke au kufanya uasherati, kwani kwa mila zetu wanawake wote ni mali ya Mukama. Hivyo watu wakawa wanamuimba Muchureza kuwa ni “kilimi nyakwelega ayagambiile omujungu ati Omukama nasiyana”. Maana yake, wimbo ulikuwa unamsuta Muchureza kwa kujichongea (okwelega) bila sababu ya msingi.
Mutakubwa, baada ya kufukuzwa, alimalizia maisha yake pale Kigarama, kwa Edward Kasano, kwani baba yake Edward alikuwa tumbo moja na Mutakubwa, wote wakiwa ni watoto wa Muchureza. Alifariki mwaka 1948 na kuzikwa pale Kigarama.
Jambo la ajabu ni kwamba wazee pale kijijini waliendelea kumpa heshima kama Mukama wakimwamkia Habuka Izoba, Habuka Rugaba, Habuka Nyakusinga, nk. Inadaiwa mtu akishasimikwa kama Mukama anakuwa na namna ya uungu (semi-divine). Hivyo ukimnyima heshima yake unaweza ukapatwa na mabaya.
Mavazi ya Asili ya Wahaya (Olubugo)
Nyumba za asili za wahaya
Gavana wa kwanza wa kiingereza ni Sir Horace Byatt (1916-1924) na wa mwisho ni Sir Richard Turnbull (1958-1961). Wahaya (wakiwemo Wanyambo) wanajulikana kama Western Interlacustrine Bantu. Walihama kutoka Uganda Magharibi katika karne za 15 na 16, hasa kutoka Bunyoro na Ankole. Koo nyingi asili yao ni Bunyoro na chache kama abamiilo/abagabo asili yao ni Ankole.
Kihanja, Ihangiro na Bukara Bakama wao ni Bahinda wakati wale wa Kiamutwara na Bugabo ni Bankango waliowaasi Bahinda na kujitangazia uhuru yapata mwaka 1820 wakati Mukama Kalemera II alipofariki. Uasi huu uliongozwa na Kitekere na baadaye kuimarishwa na mtoto wake Omukama Kaitaba (1860-1888).
Kiziba Rulers (title Omukama)
.... - .... Bike
.... - .... Kiziba Kizindo
.... - .... Ntumwa
.... - .... Kanyamaishwa
.... - .... Kibi I Nyakiiru Kaganda
.... - .... Ishamura-Njobe "elya Kiziba, elingome"
.... - .... Ishamura-Nyakabinga "elya Bunyoro"
.... - .... Wanumi
.... - .... Bwanamba
.... - .... Matwi
.... - .... Magembe I (1st time)
.... - .... Kashumba (regent?)
.... - .... Magembe I (2nd time)
.... - .... Muzinga
.... - .... Mwigara
.... - .... Burungu I
.... - .... Magembe II
.... - .... Mboneko I
.... - .... Nyarwangu
.... - .... Mulimpuzi -Regent
.... - .... Ruhangarazi I
.... - .... Nyarwangu II
.... - .... Rutajwaha
.... - .... Burungu II Kakinda
.... - .... Kibi II Rutahirwa
.... - 1870 Ruhangarazi II (d. 1870)
1870 - 1903 Mutatembwa
1898 - 1900 Rweshabura (in rebellion)
1903 - 1916 Mutahangarwa Karutasigwa
1916 - 1927 Edward George Mboneko II
1927 - 1937 William Mutakubwa
3 May 1937 - 6 Nov 1962 Nestor Lutinwa wa mwisho kusimikwa (kutendekwa)
Bakama wa Kiziba ukoo wao ni Baziba/Babiito. Baada ya kifo cha Mukama Burungu II (1800-1835) walipendelea kuitwa Abayobya. Sababu ni kwamba wanatokana na Omulangila Luyobya, mtoto wa Mukama Ruhangarazi I. Kutokana na ukatili uliopitiliza wa Burungu II, baba yake mdogo, Omulangila Luyobya, alishindwa kumvumilia na hivyo akaanzisha vita ya kumng’oa. Katika vita hii alisaidiwa sana na mtoto wake aliyeitwa Rutahilwa. Luyobya kwake kulikuwa ni Bukwali, Kanyigo.
Burungu II alijikuta katika hali ngumu ya kushambuliwa kutoka ndani na nje, kwani Bahyoza walikuwa pia wanamshambulia. Baada ya Burungu kuuawa na maadui mwaka 1835, Rutahilwa, mtoto wa Ruyobya alitawala na akapewa jina Kibi II. Baada ya Kibi II, alitawala mtoto wake Rugangarazi II (1858-1865), halafu Mutatembwa (1865-1903), aliyefuatiwa Mutahangarwa (1903-1916), kisha Mboneko II (1916-1926), halafu Mutakubwa (1926-1937), halafu Lutinwa (1937-1974).
Mutakubwa aliondolewa na wakoloni mwaka 1937 na hakuwa na mtoto. Hivyo ndugu yake Mboneko aitwaye Nestor Lutinwa alichaguliwa kumrithi, na akatawala mpaka Nyerere alipofutilia mbali utawala wa Bakama.
Sababu ya kuondolewa kwa Mutakubwa ni inadaiwa ni ufuska uliokithiri, ukiwemo ule wa kulazimisha mama yake Muchureza alijaribu kumkanya lakini hakusikia. Hivyo alikwenda kumuomba DC wa Kikoloni amsaidie kumkanya. Badala ya kumkanya DC alimfukuza, kwani kwa mzungu kubaka ni dhambi isiyosameheka. Lakini DC hakuelewa kuwa Mukama hawezi kuwa na hatia ya kumbaka mwanamke au kufanya uasherati, kwani kwa mila zetu wanawake wote ni mali ya Mukama. Hivyo watu wakawa wanamuimba Muchureza kuwa ni “kilimi nyakwelega ayagambiile omujungu ati Omukama nasiyana”. Maana yake, wimbo ulikuwa unamsuta Muchureza kwa kujichongea (okwelega) bila sababu ya msingi.
Mutakubwa, baada ya kufukuzwa, alimalizia maisha yake pale Kigarama, kwa Edward Kasano, kwani baba yake Edward alikuwa tumbo moja na Mutakubwa, wote wakiwa ni watoto wa Muchureza. Alifariki mwaka 1948 na kuzikwa pale Kigarama.
Jambo la ajabu ni kwamba wazee pale kijijini waliendelea kumpa heshima kama Mukama wakimwamkia Habuka Izoba, Habuka Rugaba, Habuka Nyakusinga, nk. Inadaiwa mtu akishasimikwa kama Mukama anakuwa na namna ya uungu (semi-divine). Hivyo ukimnyima heshima yake unaweza ukapatwa na mabaya.
Mavazi ya Asili ya Wahaya (Olubugo)
Nyumba za asili za wahaya