Mkimaliza za marekani, tujadili na zetu wenyewe
Au ndio mke wa maskini, kuwadi mumewe
Nani anashika usukani, nani ni baridi
Kati ya Joh makini, na ngosha Fid
Ama mbishi na zaeed, sio tu 50 na did
Inapendeza mnapoeleza hip hop na miiko
Wapi na lini ilikuwa chimbuko,
Mtiririko wa list ya maandiko
Sio twist ni mziki wenye wenye mashiko
Mtu kama common hayupoKwanini uamini Billboard?
Wewe unaamini hiyo list imekamilika?
Kwanini infuential rapper kama 2PAC hawajamweka?
Kwanza hiyo list inaonekana ipo biased sana.
Nilitegemea mtu kama 2pac awepo,nilitegemea NWA wawepo.
Kwa sababu mimi ninaamini kuwa mc mkali lazima uwe CHANGE AGENT. Sasa kwa mtu kama Kendric Lamar ambaye hana hata miaka 5 kwenye peak ya muziki huu unakuja kusema ni mc mkali?
Sikatai kuwa Kendric ni mkali lakini hiyo ya kusema mcs wakali kuwahi kutokea duniani.
Mavazi
- Nguzo tano za HIPHOP
1. Udijei
2. Michano
3. Machata
4. Mabreka
5. Ufahamu
Michano ya ‘Kinyamwezi’
Kipindi hiki cha miaka kati ya 88 hadi 93 watu (wengi waliojumuika na kuunda Kwanza Unit) walikuwa wanashinda na kanda za nyimbo za Hip Hop za New York, na ni kawaida kichwa akajua nyimbo hata kumi zote za santuri moyoni. Na ni kipindi ambapo disco la Clouds pia lilikuwa linapata kila santuri na single kutoka Marekani.
Na Kwanza Unit (baadhi, kabla haijawa KU Crew) walikuwa mara nyingi wanashinda Mawingu, hata kabla hakujawa studio ya kurekodi. Vilinge hivi vilijumuisha uangaliaji wa video za muziki na filamu za Marekani, soultrain video, kanda za redio kama zile za Tim West Wood (DJ maarufu sana wa Hip Hop na mtangazaji wa redio), n.k. Hizi kanda watu wanazo hadi leo.
Uwezo wa kuchana wa hawa watu wa karibu ulikuwa mkubwa kiasi kwamba kama wanachana nyimbo ya mtu inafanyika kama ambavyo unaisikia kwenye CD leo na zao za kuandika. Kifupi Kwanza Unit walikuwa na uwezo wa kuchana kama wanyamwezi wenyewe.
Nimeskiliza 'run tingz' ya KU. Bado najaribu kuelewa unavyosema "walikuwa na uwezo wa kuchana kama wanyawezi wenyewe". Stick to the facts, Chief, not opinions.