Hili suala la wanaume kufia gest mnalichukuliaje?

Hili suala la wanaume kufia gest mnalichukuliaje?

Norshad

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2013
Posts
5,224
Reaction score
12,622
Habari wandugu,

Nielekee katika swali langu kama linavyojieleza hapo juu,

Kumekuwa na mtukio mengi ya watu kufikwa na mauti wakiwa katika nyumba za wageni, hasa wale wanaofika pale kama wapenzi, vifo hivi mara nyingi vinahusisha zaidi wanaume kuliko wanawake, napenda kufahamu ni nini kinachosababisha hali hii iongezeke mara dufu miaka ya hivi karibuni?

Nitatoa mfano ambapo jana wakati narudi nyumbani nilipita jirani na nyumba moja ya wageni ambapo kulikuwa na tafrani kubwa huku mwanamke akiwa mtupu kama utupu mnavyoujua, yule mrembo alikuwa akiwaka kwamba yule mwanaume aliyeingia naye katika hicho chumba walimokuwepo alikuwa hataki kutumia kinga, na yeye hawezi fanya mapenzi bila kinga hawajuani wamekutana juu juu tu, hivyo akawa analalama kwamba jamaa alitaka kumuingilia kinguvu, ukimsikiliza jamaa sasa ambaye naye alikuwa na taulo tu. Yeye asema yule ni malaya amemchukua kwa dhumuni la kwenda kusuuza nafsi yake.

Shida iliyotokea kule ndani ni kwamba yule mwanamke alikuwa amemuwekea madawa katika chuchu na kinywaji ili jamaa akizima yule mwanamama amuibie asepe na atakachoweza kubeba.

Sasa ile ni trick ya mwanamke mjazia nzi ili aonekane yeye jamaa ndio ana makosa lakini ni kwamba yule malaya ndio alitaka muibia na kwa kuwa ni tabia, ama mozoea ama ndio kazi yake hakuona taabu kutoka nje uchi na kumjazia nzi jamaa, sasa kwa mantiki hii inawezekana vifo vingi vinavyowakuta wazinzi huko katika nyumba za wageni vinatokana na matumizi ya madawa kama haya ya kusizishana ili mwengine atimize lengo lake.

Imefikia stage mtu akiingia na mwanamke gest, alafu ikatokea mwanamke ametangulia kutoka kabla ya aliyeingia nae, husimamishwa mapokezi na kurudishwa mpaka katika chumba walichokuwemo ili kuhakikisha usalama upo wa kutosha.

Je kuna sababu zingine ambazo zinaweza kusababisha kifo ama vifo hasa kwa wanaume huko ktk nyumba za wageni zaidi ya hii ya kuwekewa madawa ama yeye mwenyewe kwa hiyari yake kuchanganya madawa ili aonekane shababi.

Nawasilisha
 
Vifo vingi vinachangiwa na matumizi ya madawa ya kuongeza nguvu kama vile Viagra au generic Viagra zinazoitwa erecto toka India na bei zake ni nafuu shillings 3,000 kwa kidonge cha gram 100, kuna vingine ni gram 50, hizo dawa hazina tatizo kwani active ingredient inayoitwa sildernafil imeruhusiwa mpaka US na Europe na sehemu nyingi duniani kama tiba kwa mapungufu ya nguvu za kiume, tatizo kubwa ni kuwa ukiwa na high blood pressure ni hatari sana na kamwe hautakiwi kutumia hizi dawa kwa kuwa maduka yetu ya madawa yanauza hizi dawa bila kumpima mtu pressure, basi ndio akienda uko guest house na mwanamke hatari sana na hali inakuwa mbaya zaidi kama mtu kachanganya na pombe kali, tena red bull, kibaya zaidi watu wengi wana high blood pressure lakini wao hawajui
 
Watu wanajikomoa kwa kujimaliza nguvu za kiume wakitumia madawa

Watu wasichoelewa ni kuwa kuwai kumwaga na wanachodhani ni upungufu wa nguvu za kiume hio ni sychological problem na sio hormonal problem

Mkuu naomba ueleze kidogo kiurefu hapo maana hilo ni tatizo linaloukabili wengi...
 
Kifo mi mahali popote. Tena kuga juu ya kiuno ni sawa kabisa kwani pale mwanaume anatumia nguvu sana na damu nyingi inakua kwenye uume na isitoshe raha sanaa au maumivu sanaa yanaua
 
vifo hivi mimi naamini vinakuwa na sababu zaidi ya hilo tendo lilowapeleka huko
 
Yote yanaweza kuwa majibu...
Shinikizo la damu, kuji-over doze na madawa ya kuongeza nguvu, kuwekeana madawa kwenye maeneo ambayo mdomo utapitishwa...

cc: mahondaw
 
Vifo vingi vinachangiwa na matumizi ya madawa ya kuongeza nguvu kama vile Viagra au generic Viagra zinazoitwa erecto toka India na bei zake ni nafuu shillings 3,000 kwa kidonge cha gram 100, kuna vingine ni gram 50, hizo dawa hazina tatizo kwani active ingredient inayoitwa sildernafil imeruhusiwa mpaka US na Europe na sehemu nyingi duniani kama tiba kwa mapungufu ya nguvu za kiume, tatizo kubwa ni kuwa ukiwa na high blood pressure ni hatari sana na kamwe hautakiwi kutumia hizi dawa kwa kuwa maduka yetu ya madawa yanauza hizi dawa bila kumpima mtu pressure, basi ndio akienda uko guest house na mwanamke hatari sana na hali inakuwa mbaya zaidi kama mtu kachanganya na pombe kali, tena red bull, kibaya zaidi watu wengi wana high blood pressure lakini wao hawajui
Ahsante kwa mchango wako kwenye mada hii.
Ila mkuu naomba kujuzwa. Kwanza kabisa sina mahudhurio ya bar, Pili, sijawahi kutumia kilevi chochote.
Mtanziko wangu kwako ni kuhusu red bull mara kadhaa nmesikia watu wakisema si pombe, lakini hapa umeitaja kama pombe.
Tafadhari , kwa nia njema kabisa, naomba unieleweshe kwa kina.
Nawasilisha
 
Ahsante kwa mchango wako kwenye mada hii.
Ila mkuu naomba kujuzwa. Kwanza kabisa sina mahudhurio ya bar, Pili, sijawahi kutumia kilevi chochote.
Mtanziko wangu kwako ni kuhusu red bull mara kadhaa nmesikia watu wakisema si pombe, lakini hapa umeitaja kama pombe.
Tafadhari , kwa nia njema kabisa, naomba unieleweshe kwa kina.
Nawasilisha
Sio pombe ni energetic drink inayofanya mzunguko wa damu kuwa na speed kubwa mapigo ya moyo yanaenda kasi
 
Nimejifunza kitu...kumbe wanawekaga dawa/sumu kwenye matiti!!
 
Back
Top Bottom