Hili silielewi.

IGWE

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2011
Posts
9,714
Reaction score
8,118
Wasalaam wapendwa.......
Niko hapa home baada ya kutoka kijiweni kutafuta riziki nimejipumzisha.,mara namuona mama mtoto wangu anatoka kuelekea sokon(sio mbali na home) huku simu kaiacha mezan.
Simu inaita mara kadhaa bila kupokelewa(sina kawaida ya kupokea simu ya mtu bila ridhaa yake) hii ni ktk juhudi za kutekeleza na kuilinda ile law of privacy kwenye mawasiliano ya simu.

Mara namuona mama mtoto anaingia na kapu la matunda na vitu vingine_namuambia simu imeita mara nyingi,analalamika eti kwanini sijapokea...eti sio vizuri ninavyofanya.

My take,..Je_ni sahihi kupokea simu ya mkeo/mumeo ikiita na kama yeye hayupo...?
 
Ngoja jinsia ya ke waje maana wanaongoza kwa wivu.
 
Wewe unajihangaisha kumuelewa mkeo? Unajipa kazi ya ziada ambayo hukuumbiwa. Kazi yako ni kumpenda tuuu, bhaaaas!
Halafu unamdaka na mada ya kuwa simu yake iliita, kwani hairekodi missed calls? Si angeangalia mwenyewe akaona. Manake ulitegemea akujibu vipi suala lako? Acha uchokonovu. Shaurilo!
 
Kwa hiyo hayo manung"uniko ni mtego...mmmmh

Siku nyingine akiacha simu mwambie, simu yako iliita nikapokea af mwangalie vizuri usoni utaona atakavyohamaki!! Hahahaaa....! Acha kabisa haya mambo ya upekuzi wa simu ya mwenza..!!
 

Noted...
 
Siku nyingine akiacha simu mwambie, simu yako iliita nikapokea af mwangalie vizuri usoni utaona atakavyohamaki!! Hahahaaa....! Acha kabisa haya mambo ya upekuzi wa simu ya mwenza..!!

ahahahaaaaaaaaaa.....hii nzuri mkuu
 
Sidhani kama ni vibaya kupokea sim ya mke au mume wako kama yupo mbali. Unjibu tu in short "samahani mwenye simu ametoka kidogo"
 
Upokee kwani simu yako? au wewe ni telephone operator? utakufa kwa BP bulee!
 
Sidhani kama ni vibaya kupokea sim ya mke au mume wako kama yupo mbali. Unjibu tu in short "samahani mwenye simu ametoka kidogo"

Nimekupata mkuu.....
 
endelea hivyo hivyo kutopokea
ukitaka presure na kufa kabla ya wakati
pokea hiyo simu 1 day hahaaa!tutakukosa bure!

 

Hivi hela ya sokoni ulimpa???
Je ni nani alimjazia kapu lake maana aliondoka bia mfuko
Lazima akulaumu ili usihisi maana sisi wanawake tuna mbinu nyingi hasa kama tumesahau evidence mahali
ila nakushauri usiwe unapokea simu au kuzipekua utazirai
 
Waweza pokea simu ya mkeo lkn inategemea mnaishije hapo kwenu. Kama umepewa rukhsa ya kupokea simu yake basi sio mbaya lkn ujiandae na yako itakapopokelewa siku moja usije kurusha ngumi tu. Ni vizuri wote mkiwa waaminifu ktk maisha yenu ya ndoa wala hapatakua na tabu ya hizo simu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…