Elections 2010 Hili Ndilo Neno La Mama Salma

TandaleOne

JF-Expert Member
Sep 4, 2010
1,644
709
Anayependa maendeleo atatambua mafanikio ya serikali-Mama Salma

NA JACQUELINE LIANA, BAGAMOYO

MWENYEKITI wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA), Mama Salma Kikwete, amesema mtu anayependa maendeleo nchini, atatambua mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha miaka mitano ya uongozi wa serikali ya awamu ya nne.

Akizungumza kwa nyakati tofauti na wanawake wa wilaya za Kibaha, Chalinze na Bagamoyo, mkoani Pwani jana {24.8.2010}, alisema mengi yaliyoahidiwa na Chama Cha Mapinduzi katika uchaguzi mkuu wa 2005, yametekelezwa.

Mama Salma Kikwete alisema, katika suala la maendeleo na mustakabali wa nchi, ni lazima wanawake waangalie ni chama gani chenye sera na ilani makini, katika kuwaletea maendeleo yao, na jamii yote ya Watanzania.

Alitaja baadhi ya mafanikio yaliyopatikana katika kipindi hicho kuwa ni ujenzi wa shule za sekondari za kata, zilizoondoa tatizo la watoto wanaofaulu na kushindwa kuendelea sekondari kwa kukosa nafasi.

Mama Salma alisema, ujenzi wa shule za sekondari umeongezeka kutoka 1,745 hadi 4,102 katika kipindi cha miaka mitano, jambo ambalo ni mafanikio makubwa, lakini kuna watu wanaojifanya kutoyaona.

Kutokana na kuongezeka kwa shule hizo, alisema idadi ya wanafunzi nayo imeongezeka ambapo uandikishaji wa kidato cha kwanza hadi cha nne ulitoka kuwa wanafunzi 401,598, mwaka 2005, hadi 1,401,559 mwaka 2009.

Kuhusu miundombinu, alisema ujenzi wa barabara zinazounganisha mikoa na wilaya nchini umewezesha wananchi kusafiri kwa haraka kutoka sehemu moja ya nchi kwenda nyingine, ikilinganishwa na hali ilivyokuwa huko nyuma.

"Zamani ilikuwa kutoka hapa (Kibaha), hadi Lindi tulilazimika kulala njiani, lakini sasa mambo ni mazuri," alisema na kupigiwa kofi.

Alisema, Chama Cha Mapinduzi kimetekeleza ilani yake kwa mafanikio makubwa, na asiye na macho haambiwi tazama, kwani wengine wanaona mafanikio hayo lakini wanajifanya hawaoni," alisema.

Mama Salma aliwaomba kina mama hao kuwachagua wagombea wa Chama Cha Mapinduzi katika uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba 31, mwaka huu katika mtindo maarufu wa CCM wa mafiga matatu.

"Siku ya tarehe 31 mwezi wa kumi, ukifika kituoni piga kura kwa mgombea urais wa CCM, mgombea ubunge wa CCM na mgombea udiwani wa CCM hayo ndiyo mafiga matatu," Alisema.

Akizungumzia kura za maoni za CCM kuwapata wagombea ubunge na udiwani, Mwenyekiti wa WAMA alisema, zilisababisha makundi tofauti kwa sababu wagombea walikuwa ni wengi.

Kwa vile mchakato huo umemalizika na wagombea kupatikana, aliwasihi wanachama wa CCM kuvunja makundi hayo na kuwa na kundi moja la CCM kwa ajili ya kukipatia Chama Cha Mapinduzi ushindi wa kishindo katika uchaguzi mkuu ujao.

Kesho, (Agosti 25, 2010) Mama Salma Kikwete ataendelea na ziara ya kuzungumza na wanawake katika wilaya za Kisarawe, Mkuranga na Rufiji, na Agosti 26, 2010 anatarajiwa kuwa Mafia.

xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx



'Zingatieni masharti mikopo isaidie wengi'

*Ni kauli ya Mama Salma kwa kinamama

God Bless Our Country and protect it from liars,disorganized and crazy people

 
Katiba inamtambua huyu mama kama mwanasiasa au mke wa rais anaeomba ridhaa ya wananchi tena?
 
Alitaja baadhi ya mafanikio yaliyopatikana katika kipindi hicho kuwa ni ujenzi wa shule za sekondari za kata, zilizoondoa tatizo la watoto wanaofaulu na kushindwa kuendelea sekondari kwa kukosa nafasi.

Mama Salma alisema, ujenzi wa shule za sekondari umeongezeka kutoka 1,745 hadi 4,102 katika kipindi cha miaka mitano, jambo ambalo ni mafanikio makubwa, lakini kuna watu wanaojifanya kutoyaona.

Hivi huyu Mama alishawahi kutembelea zile shule za msingi alizokuwa anafundisha? Natumaini HAPANA - vinginevyo asingethubutu kutamka hayo maneno!

BTW: Haya majengo (mengine hayana hata madirisha) yanayopewa jina "shule za kata" ni SHULE kweli?
 
Katiba inamtambua huyu mama kama mwanasiasa au mke wa rais anaeomba ridhaa ya wananchi tena?

Unamjua Michelle Obama????Na yule aliyepandishwa jukwaani na magwanda??Hii forum sijui inakuwaje.Mnaongelea watu badala ya ujumbe.Kweli waafrika.
 
Hivi huyu Mama alishawahi kutembelea zile shule za msingi alizokuwa anafundisha? Natumaini HAPANA - vinginevyo asingethubutu kutamka hayo maneno!

BTW: Haya majengo (mengine hayana hata madirisha) yanayopewa jina "shule za kata" ni SHULE kweli?

Fuatilia utajua kama kweli unataka kujua aliwahi kutembelea au la.Wanafunzi wangapi wameenda form 5 na 6 kutoka shule za kata???Jiulize hilo swali.Acha ubinafsi.Kama si hizo shule wangekuwa wapi???Hakuna msomi makini asiyejua mapigano ya nchi masikini kutoka katika umasikini wake hupitia nyakati zipi.Nyakati za maopportunists na manabii wa uongo wa kisiasa ambao wanatupa mema yote na kusimama kusema mabaya kwa nguvu zao zote.Ila umma makini huwatambua.
 
Unamjua Michelle Obama????Na yule aliyepandishwa jukwaani na magwanda??Hii forum sijui inakuwaje.Mnaongelea watu badala ya ujumbe.Kweli waafrika.
Wakati mwingine ni busara kumuongelea mtu aliyetoa ujumbe kabla ya kuzama katika ujumbe wenyewe.
 
Fuatilia utajua kama kweli unataka kujua aliwahi kutembelea au la.Wanafunzi wangapi wameenda form 5 na 6 kutoka shule za kata???Jiulize hilo swali.Acha ubinafsi.Kama si hizo shule wangekuwa wapi???Hakuna msomi makini asiyejua mapigano ya nchi masikini kutoka katika umasikini wake hupitia nyakati zipi.Nyakati za maopportunists na manabii wa uongo wa kisiasa ambao wanatupa mema yote na kusimama kusema mabaya kwa nguvu zao zote.Ila umma makini huwatambua.

Tandale

Takwimu ya Salma hii hapa:

Kutokana na kuongezeka kwa shule hizo, alisema idadi ya wanafunzi nayo imeongezeka ambapo uandikishaji wa kidato cha kwanza hadi cha nne ulitoka kuwa wanafunzi 401,598, mwaka 2005, hadi 1,401,559 mwaka 2009.

Takwimu ya waliofanya mtiahani Form SIX 2010 kutoka NECTA hii hapa:
Jumla ya watahiniwa 55,764, ambao ni asilimia 88.86 ya wanafunzi wote waliofanya mtihani huo mwaka huu

Kama kujiandikisha Form I-IV umefikia 1.5mil sasa inakuwaje wanaomaliza Form VI hawafiki hata 100,000?
 
[

Takwimu ya waliofanya mtiahani Form SIX 2010 kutoka NECTA hii hapa:


Kama kujiandikisha Form I-IV umefikia 1.5mil sasa inakuwaje wanaomaliza Form VI hawafiki hata 100,000?[/QUOTE]

u gat a point?? kuna uongo hapo, au na yeye anpewa takwimu za uongo kama mume wake??????????
 
Fuatilia utajua kama kweli unataka kujua aliwahi kutembelea au la.Wanafunzi wangapi wameenda form 5 na 6 kutoka shule za kata???Jiulize hilo swali.Acha ubinafsi.Kama si hizo shule wangekuwa wapi???Hakuna msomi makini asiyejua mapigano ya nchi masikini kutoka katika umasikini wake hupitia nyakati zipi.Nyakati za maopportunists na manabii wa uongo wa kisiasa ambao wanatupa mema yote na kusimama kusema mabaya kwa nguvu zao zote.Ila umma makini huwatambua.

Matokeo ya 2009/10 ya Shule Za KATA kwa Mkoa wa Dar es Salaam:

Matokeo yaliyotangazwa na Baraza la Mitihani la Taifa (Necta) mwishoni mwa wiki, yanaonesha kuwa kati ya shule hizo, 26 zilizoko katika Wilaya za Kinondoni na Temeke, zimefanya vibaya baada ya jumla ya wanafunzi wake 2,321 kufeli,
huku 2,963 wakifaulu kwa kiwango cha daraja la nne.Kwa mujibu wa matokeo hayo, kati ya shule zilizofanya vibaya, baadhi zimefikisha wanafunzi 119, nyingine 129 na nyingine 176 waliofeli, huku waliofaulu kwa kiwango cha daraja la kwanza wakiwa ni 45.
Jumla ya waliofaulu kwa kiwango cha daraja la pili katika shule hizo,
ni 120 wakati waliofaulu kwa kiwango cha daraja la tatu wakiwa 533.
 
Huyu mama anaugonjwa wa mumewe! Nadhani naye akili zinaanza athirika nasubiri aanze kula mieleka!

Mbona alishaanza!! Siku mme wake ameanguka jangwani na yeye alianguka pia.

Ila ananikera kweli kwa kitendo cha kujivunia ujenzi wa shule ambazo watu tuliuza hadi vijiko ili tutoe michango ya ujenzi wa hizo shule! Sijui kwanini hao anaowahutubia hawamuulizi haya? Mwenzake Mkapa alitekeleza MMEM bila kututoza hata shilingi moja. Sasa huyu Kikwete katuchangisha hadi senti ya mwisho bado anajisifia.
By the way, shule ni majengo pekee au ni muungano wa majengo, wanafunzi, walimu, vifaa vya kufundishia na samani? Huyu jamaa inaonekana hakutaka kabisa kujifunza kutoka kwa Mkapa wakati anatekeleza MMEM, kwa sababu mwenzake pamoja na kuongeza udahili wa wanafunzi almost kwa asilimia 100, bado hakukuwa na shida kubwa ya walimu na vifaa vya kufundishia kama ambavyo imekuwa kwake. Nina wasiwasi na aina ya watu anaowahutubia. Manake katika hali ya kawaida, hotuba kama hii inapaswa kuwa na maswali kibao.
 
Mbona alishaanza!! Siku mme wake ameanguka jangwani na yeye alianguka pia.

Ila ananikera kweli kwa kitendo cha kujivunia ujenzi wa shule ambazo watu tuliuza hadi vijiko ili tutoe michango ya ujenzi wa hizo shule! Sijui kwanini hao anaowahutubia hawamuulizi haya? Mwenzake Mkapa alitekeleza MMEM bila kututoza hata shilingi moja. Sasa huyu Kikwete katuchangisha hadi senti ya mwisho bado anajisifia.
By the way, shule ni majengo au wanafunzi, walimu, vifaa vya kufundishia na samani? Huyu jamaa inaonekana hakutaka kabisa kujifunza kutoka kwa Mkapa wakati anatekeleza MMEM, kwa sababu mwenzake pamoja na kuongeza udahili wa wanafunzi almost kwa asilimia 100, bado hakukuwa na shida kubwa ya walimu na vifaa vya kufundishia kama ambavyo imekuwa kwake. Nina wasiwasi na aina ya watu anaowahutubia. Manake katika hali ya kawaida, hotuba kama hii inapaswa kuwa na maswali kibao.

Unajua vijana wangapi wako pale UDSM kutoka hizo shule unazozizarau???Leo wangekuwa wapi kama si hizo shule??Acheni ubinafsi.Watanzania wanasoma comments zenu na wanaona upungufu wa akili zenu.
 
[

Takwimu ya waliofanya mtiahani Form SIX 2010 kutoka NECTA hii hapa:


Kama kujiandikisha Form I-IV umefikia 1.5mil sasa inakuwaje wanaomaliza Form VI hawafiki hata 100,000?

u gat a point?? kuna uongo hapo, au na yeye anpewa takwimu za uongo kama mume wake??????????[/QUOTE]

Mwambie Dr.Slaa akutafutie takwimu za kweli.
 
Mwambie Dr.Slaa akutafutie takwimu za kweli.[/QUOTE]




witch hunt????it wont work out.!!!!!!!
 
Unajua vijana wangapi wako pale UDSM kutoka hizo shule unazozizarau???Leo wangekuwa wapi kama si hizo shule??Acheni ubinafsi.Watanzania wanasoma comments zenu na wanaona upungufu wa akili zenu.

Ndugu yangu Tandale one, hizo shule JK kazijenga lini na hao waliosoma wamefika UDSM lini? Umeshauona huo mpango wa MMES wenyewe, plan yake na implementation yake? Umeshasoma evaluation report ya hiyo MMES? Be careful my friend jaribu kuongea kwa Data.

MMES ni mpango wa Mkapa wa mwaka 2004, wakati huu mipango ilikuwa ni kuongeza shule kidogo kidogo kila mwaka kulingana na uwezo wa serikali. Shule zilizodahili wanafunzi mwaka 2005 chini ya serikali ya Mkapa, zilikuwa na walimu wa kutosha kiasi na atleast wanafunzi kadhaa waliweza kuendelea na masomo ya A-level kutoka katika hizi shule mwaka 2008. Mwaka 2006/7, ndipo akina Lowassa wakaja na mkakati wa kujenga tu majengo yasiyokuwa na idadi ambayo hayakuendana na uwezo wa serikali kusomesha walimu na kununua vifaa vya kufundishia. Ndipo ikaja idea ya voda fasta, ambayo haikuwa na mafanikio. Wanafunzi wale ambao walisoma katika mfumo wa elimu wa akina Lowasa na Kikwete (kuanzia 2006) ndio hao waliomaliza form four mwaka jana ambao bado hawajafika chuo kikuu.

Sasa wewe unaongelea wanafunzi gani walioko UDSM chini ya MMES ya Lowassa na Kikwete? Au wao wamefuata mfumo gani wa Elimu? Wamemaliza form four na kuingia UDSM?
 
unajua vijana wangapi wako pale udsm kutoka hizo shule unazozizarau???leo wangekuwa wapi kama si hizo shule??acheni ubinafsi.watanzania wanasoma comments zenu na wanaona upungufu wa akili zenu.
uwezo wako wakufikiri wewe unayeisifia ccm ambayo imezeeka haina jipya haina mtazamo mpya kazi kuturudisha na kututesa na umaskini cha uhanga wa ujinga wewe huoni umaskini uliotopea huwenda wewe pia nifisadi
 
Anayependa maendeleo atatambua mafanikio ya serikali-Mama Salma

NA JACQUELINE LIANA, BAGAMOYO

MWENYEKITI wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA), Mama Salma Kikwete, amesema mtu anayependa maendeleo nchini, atatambua mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha miaka mitano ya uongozi wa serikali ya awamu ya nne.

Akizungumza kwa nyakati tofauti na wanawake wa wilaya za Kibaha, Chalinze na Bagamoyo, mkoani Pwani jana {24.8.2010}, alisema mengi yaliyoahidiwa na Chama Cha Mapinduzi katika uchaguzi mkuu wa 2005, yametekelezwa.

Mama Salma Kikwete alisema, katika suala la maendeleo na mustakabali wa nchi, ni lazima wanawake waangalie ni chama gani chenye sera na ilani makini, katika kuwaletea maendeleo yao, na jamii yote ya Watanzania.

Alitaja baadhi ya mafanikio yaliyopatikana katika kipindi hicho kuwa ni ujenzi wa shule za sekondari za kata, zilizoondoa tatizo la watoto wanaofaulu na kushindwa kuendelea sekondari kwa kukosa nafasi.

Mama Salma alisema, ujenzi wa shule za sekondari umeongezeka kutoka 1,745 hadi 4,102 katika kipindi cha miaka mitano, jambo ambalo ni mafanikio makubwa, lakini kuna watu wanaojifanya kutoyaona.

Kutokana na kuongezeka kwa shule hizo, alisema idadi ya wanafunzi nayo imeongezeka ambapo uandikishaji wa kidato cha kwanza hadi cha nne ulitoka kuwa wanafunzi 401,598, mwaka 2005, hadi 1,401,559 mwaka 2009.

Kuhusu miundombinu, alisema ujenzi wa barabara zinazounganisha mikoa na wilaya nchini umewezesha wananchi kusafiri kwa haraka kutoka sehemu moja ya nchi kwenda nyingine, ikilinganishwa na hali ilivyokuwa huko nyuma.

"Zamani ilikuwa kutoka hapa (Kibaha), hadi Lindi tulilazimika kulala njiani, lakini sasa mambo ni mazuri," alisema na kupigiwa kofi.

Alisema, Chama Cha Mapinduzi kimetekeleza ilani yake kwa mafanikio makubwa, na asiye na macho haambiwi tazama, kwani wengine wanaona mafanikio hayo lakini wanajifanya hawaoni," alisema.

Mama Salma aliwaomba kina mama hao kuwachagua wagombea wa Chama Cha Mapinduzi katika uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba 31, mwaka huu katika mtindo maarufu wa CCM wa mafiga matatu.

"Siku ya tarehe 31 mwezi wa kumi, ukifika kituoni piga kura kwa mgombea urais wa CCM, mgombea ubunge wa CCM na mgombea udiwani wa CCM hayo ndiyo mafiga matatu," Alisema.

Akizungumzia kura za maoni za CCM kuwapata wagombea ubunge na udiwani, Mwenyekiti wa WAMA alisema, zilisababisha makundi tofauti kwa sababu wagombea walikuwa ni wengi.

Kwa vile mchakato huo umemalizika na wagombea kupatikana, aliwasihi wanachama wa CCM kuvunja makundi hayo na kuwa na kundi moja la CCM kwa ajili ya kukipatia Chama Cha Mapinduzi ushindi wa kishindo katika uchaguzi mkuu ujao.

Kesho, (Agosti 25, 2010) Mama Salma Kikwete ataendelea na ziara ya kuzungumza na wanawake katika wilaya za Kisarawe, Mkuranga na Rufiji, na Agosti 26, 2010 anatarajiwa kuwa Mafia.

xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx



'Zingatieni masharti mikopo isaidie wengi'

*Ni kauli ya Mama Salma kwa kinamama

God Bless Our Country and protect it from liars,disorganized and crazy people


Nahisi baada ya JK kuondoka Ikulu mapendo yao yatapungua kidogo!
 
Huyu TandaleOne kama Malaria Sugu vile! yaani wanafikiri kwa umbali wa pua, I doubt his/her level or eductaion and in that matter his/her thinking ability! Maana hapa tunaweza kuwa tunajaribu kumuelewesha mtu kumbe uwezo wake wa kufikiri ni wa Form four ya shule za kata!
 
Back
Top Bottom