Hili la Rais Magufuli la kutoa pesa linanichanganya

mafutamingi

JF-Expert Member
Feb 14, 2011
2,772
2,171
Mara nyingi Rais Magufuli anapokuwa katika ziara hunukuliwa akisema atatoa fedha zifanye hiki au kile.

Jambo hili limefanyika mara nyingi kiasi kwamba taswira inajengeka kuwa ili sehemu fulani ipate barabara, maji, kituo cha afya, n.k ni lazima Rais atamke.

Kwa uelewa wangu ni kwamba miradi yote inayotekelezwa nchini huwa inatokana na fedha zilizopitishwa na bunge kwenye bajeti husika.

Sasa kama ni hivyo, je ile kauli ya Rais kwamba anatoa fedha za kufanya hiki au kile ziko ndani ya bajeti iliyoidhinishwa na bunge?

Kama iko ndani je ni sahihi ya yeye kusema atatoa fedha? Kama haiko kwenye bajeti je pesa anayoitamka itatoka wapi?

Hayo ndo mambo yanayonichanganya.

Naomba nielemishwe.
 
Uelewa wangu uko hivi..!
  • 1. Fuatilia makadilio ya mapato na matumizi ya fedha ambayo yanapitishwa na Bunge labda hufikia trillion 30+ na katika hilo utakuta labda serikali imepanga asilimia 40 ya bajeti itaenda kwenye miradi ya maendeleo ikiwemo kujenga barabara zenye urefu wa Km 700 kwa mwaka na uboreshaji wa vituo vya afya. Mwisho wa siku ukija kumsikiliza Waziri waFedha wakati akitoa tathimini ya utekelezwaji wa Bajeti utakuta licha ya ahadi hizo zote za kutoa hela huko utakuta ni 30% tu ya fedha za maendeleo ndizo zilitoka serikalini kwenda kwenye miradi ya maendeleo.
  • Mwisho namnukuu Baba wa taifa:- alikuwa kwenye ziara mikoani kipindi yuko madarakani akakuta watoto njiani huko wakiwa wanaenda shule hawana unform wala viatu na nguo zenyewe walizovaa zimechakaa akajisemea mwenyewe "Loh..! Mzigo wote huuu ni wangu..!" Kwaiyo kila kero na tatizo na mizigo ya shida ni ya Rais wa nchi na ndiyo maana leo kila atakachofanya ata mtu wa chini yake akafanya vibaya lawama zote zitaenda kwa John. Leo utalala ndani huendi ata kupiga mishe zako alafu utaamka utasema maisha magumu huku ukimshushia lawama John, Je, Kwanini umlumu John wakati unajua mtaji wa masikini ni nguvu zake mwenyewe?
 
Mara nyingi Rais Magufuli anapokuwa katika ziara hunukuliwa akisema atatoa fedha zifanye hiki au kile.
Jambo hili limefanyika mara nyingi kiasi kwamba taswira inajengeka kuwa ili sehemu fulani ipate barabara, maji, kituo cha afya, n.k ni lazima Rais atamke.
Kwa uelewa wangu ni kwamba miradi yote inayotekelezwa nchini huwa inatokana na fedha zilizopitishwa na bunge kwenye bajeti husika.
Sasa kama ni hivyo, je ile kauli ya Rais kwamba anatoa fedha za kufanya hiki au kile ziko ndani ya bajeti iliyoidhinishwa na bunge?
Kama iko ndani je ni sahihi ya yeye kusema atatoa fedha? Kama haiko kwenye bajeti je pesa anayoitamka itatoka wapi?
Hayo ndo mambo yanayonichanganya. Naomba nielemishwe.
TUMIA PESA IKUZOEE.
 
ukiona hivyo anazo hela ndio mana anaahidi atatoa
Mara nyingi Rais Magufuli anapokuwa katika ziara hunukuliwa akisema atatoa fedha zifanye hiki au kile.

Jambo hili limefanyika mara nyingi kiasi kwamba taswira inajengeka kuwa ili sehemu fulani ipate barabara, maji, kituo cha afya, n.k ni lazima Rais atamke.

Kwa uelewa wangu ni kwamba miradi yote inayotekelezwa nchini huwa inatokana na fedha zilizopitishwa na bunge kwenye bajeti husika.

Sasa kama ni hivyo, je ile kauli ya Rais kwamba anatoa fedha za kufanya hiki au kile ziko ndani ya bajeti iliyoidhinishwa na bunge?

Kama iko ndani je ni sahihi ya yeye kusema atatoa fedha? Kama haiko kwenye bajeti je pesa anayoitamka itatoka wapi?

Hayo ndo mambo yanayonichanganya.

Naomba nielemishwe.

Sent usingJamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom