GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,892
- 109,610
Nashauri Rais anapoapishwa tu apewe muda fulani kwa Kutulia ili aweze Kuchagua Watendaji alio na uhakika nao Kiufanisi ili anapowateua basi wafanye Kazi na siyo kuteua Watu (Watendaji) kwa Kubeti au Kubahatisha kama inavyoonekana sasa.
Kwa Mtazamo wangu GENTAMYCINE hasa kwa hii tabia ya sasa ya Marais Wetu Kuteua na Kutengua itazalisha Upigaji na Rushwa Kuongezeka kwa Watendaji Wanaoteuliwa kwakuwa watakuwa wanajua hawana uhakika wa Kudumu katika Nafasi zao hivyo cha Msingi ukishateuliwa (Ukishaula) anza Kwanza Kuiba (Kupiga) na Kuchukua mno Rushwa ili hata Rais akija Kukutumbua tayari Wewe umeshajikamilisha Kiutajiri na kwamba hutoathirika Kimaisha.
Na. nina uhakika hiki nilichokielezea hapa ndiyo kipo sasa on the ground ndiyo maana unaona wale Wote wanaotumbuliwa hakuna mwenye Kujali au mwenye Nyuso ya Huruma au hata ile ya Usununu (Kuchukia) bali Wote huwa Kawaida huku wakichekea Matumboni mwao, wakimcheka Kimoyomoyo aliyewatumbua kuwa amechelewa kwani Wameshajitajirisha vya Kutosha kwa muda aliowaamini kwa Mtindo wa Kubeti na Kuwabahatisha.
Wateuliwaji waaminiwe ili Wadumu!
Kwa Mtazamo wangu GENTAMYCINE hasa kwa hii tabia ya sasa ya Marais Wetu Kuteua na Kutengua itazalisha Upigaji na Rushwa Kuongezeka kwa Watendaji Wanaoteuliwa kwakuwa watakuwa wanajua hawana uhakika wa Kudumu katika Nafasi zao hivyo cha Msingi ukishateuliwa (Ukishaula) anza Kwanza Kuiba (Kupiga) na Kuchukua mno Rushwa ili hata Rais akija Kukutumbua tayari Wewe umeshajikamilisha Kiutajiri na kwamba hutoathirika Kimaisha.
Na. nina uhakika hiki nilichokielezea hapa ndiyo kipo sasa on the ground ndiyo maana unaona wale Wote wanaotumbuliwa hakuna mwenye Kujali au mwenye Nyuso ya Huruma au hata ile ya Usununu (Kuchukia) bali Wote huwa Kawaida huku wakichekea Matumboni mwao, wakimcheka Kimoyomoyo aliyewatumbua kuwa amechelewa kwani Wameshajitajirisha vya Kutosha kwa muda aliowaamini kwa Mtindo wa Kubeti na Kuwabahatisha.
Wateuliwaji waaminiwe ili Wadumu!