lebadudumizi
Senior Member
- Jun 9, 2011
- 149
- 20
Mambo ya Nkono yametokea wapi hapa tunazungumza ujambazi wa Lema mzee acha uvivu wa kufikiri.Ukitaka kumjadili Mkono fungua thread yake tutajimwaga.Ufisadi wa Mkono hauwezi kuwa utetezi wa ujambazi wa Lema.
uKIJUBU NA HILI JIBU NA HILI HAPA CHINI
NIMROD ELIREHEMA MKONO![]()
Mheshimiwa Nimrod E. Mkono ni Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijiji na Mshiriki Mkuu wa kampuni ya mawakili ya Mkono & Company Advocates ya Dar es Salaam. Barua ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Mahesabu ya Serikali inaainisha kuwa Benki Kuu imekuwa ikilipa malipo makubwa kwa Mkono & Co. Advocates hasa yale yanayohusu kesi ya Valambhia ambapo Benki Kuu inadaiwa jumla ya shilingi bilioni 60. Kwa mujibu wa barua ya wakaguzi tayari Mkono & Co. Advocates wamekwishalipwa shilingi 8,128,375,237 kwa fedha taslimu kwa kesi hiyo ambayo bado iko mahakamani. Malipo haya ni sawa na asilimia 13.5 ya deni lote inalodaiwa Benki Kuu. Hoja ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu ni kuwa kesi hii haina muda maalumu wa kumalizika na hivyo inawezekana kabisa malipo ya wanasheria yakazidi kiasi cha fedha inachodaiwa Benki Kuu.