Hii ni zaidi ya Vita...

May 22, 2017
65
298
INGEKUWA WEWE UNGEFANYAJE?

UMEMUAGA mkeo unaenda kazini, ukapita kwa mchepuko wako, wakati unajimwaya-mwaya na mchepuko, mume wa mchepuko akagonga mlango, ikabidi ufichwe uvunguni mwa kitanda.

Wakati bado upo uvunguni ka mchepuko kakamuaga mume wake kwamba, kanaenda saloon, mume wa ka-mchepuko naye akaona ndo muda wa kuita mchepuko wake, akauita ukaja, wakajimwayamwaya kwa sana muda huo wee bado upo uvunguni.

Mara mchepuko wako akarudi kutoka saloon, akagonga mlango, ikabidi mume wa mchepuko wako aufiche uvunguni mchepuko wake. Kucheki hivi kumbe mchepuko wenyewe ndio mke wako uliyemuaga unaenda kazini, kwa hiyo wewe na mke wako wote mkawa mmefichwa uvunguni.

Ukisikia vita ya tatu ya dunia, ndo hii sasa.

Ungefanyaje?
 
Hapo umekonekti chaja, chaji imeanza kuingia, subiri hadi iwe full
 
Dogo acha kutuletea mambo ya kitoto humu. Tangu lini mchepuko ukawa na mume
 
Kama ni mke wa mtu akiwa na mahusiano na Mwanaume mwingine huyo Mwanamke atakuwa ni Mchepuko.
Mke wa mtu anabakia kuwa mke wa mtu. Mchepuko ni yule mwanamke ambaye hajaolewa halafu anachukuliwa na mwanaume aliyeoa!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom