cheupe sr
Senior Member
- Aug 18, 2012
- 102
- 34
Ni kitambo sasa nimekuwa nawaza hivi inakuaje mwanamke anaweza kutoka nje ya ndoa wakati mume ulimpenda mwenyewe na mkakubaliana kwa moyo kabisa kuishi pamoja kama mume na mke.. that means umemkubali kwa kila kitu...Kwa wewe mwanaume ambaye umeoa na mkeo anakuonyesha mapenzi yote na kukupa na huduma muhimu zinazohitajika, si kwamba ujione tena wewe ndo kama Mungu na kuanza kunyanyua mabega juu kana kwamba mkeo anaomba kazi kwako, onyesha mapenzi na wewe kwa mwenzio. Naweza kusema kwa asilimia kubwa wanaume wengi hawana mahaba ya dhati kwa wake zao. Though wakati mnaoana mapenzi yalikuwepo. Mfano mwanaume haujui kuappreciate chochote mkeo anachofanya pia always chochote anachosema mkeo ni lazima upinge.. Why for God sake.. Hii hali inazidi kuwa mbaya kwa wanaume naweza kusema ma HB.. wana hizi tabia sana sana sana...Hata kama na wewe ni beauty lady lakini lazima akufanyie mapozi kidogo na vi maringo maringo vya hapa na pale.. Jamani mapenzi ni two way traffic, sio eti mimi nifanye kazi ya kukupenda wewe na kukuhudumia kama mke halafu wewe usinionyeshe any affection, unafikiri uhusiano huu utadumu kwa muda gani?? Unajua wanaume wamekaa kutulaumu tu wanawake mara ooh hawajitumi lakini mi nasema chanzo cha yote hayo ni wewe mwanaume.. wewe umetekeleza wajibu wako wa kumpenda mkeo? Wanawake nawaze nikasema kwa asilimia kubwa sana wako very flexible na hasa kwenye mahusiano. utakavyo mtreat mwanamke kwenye uhusiano nivyo naye atakavyo respond.. Usitegemee treatment nzuri kutoka kwa mkeo wakati wewe mwenyewe haumfanyia hiyo treatment, au wanawake wao hawahitaji mapenzi??? Men you should change your attitude and at least show love to your partners otherwise am telling you hao wanawake walio kwenye ndoa wanahangaika hawatafuti kingine zaidi ya affections only.... Stay blessed all of you and good day.