Hii ni sawa jamani!? [Kwa wanaume tu!]

Tatizo si kila mwanaume bali tu baadhi yetu,lakini nikukumbushe kuwa mumeo haandaliwi na mtu mwingine yeyote bali wewe.The way unataka mumeo awe wewe unahusika,kwanini msingumze mbona atakuwa anakuelewa tu kama kweli anakupenda.
Nafahamu kuwa hili lipo na hata mie kuna wakati nadhani ndiye mwenye majukumu mengi kuliko mke wangu kitu ambacho si kweli labda kutokana na mfumo tuliorithi toka kwa mababu,but kama mnajipa nafasi ya kujadiliana juu ya mambo yenu litakuwa vizuri.Hilo linajadilika ndani ya nyumba!
 
hiyo na kupigiwa honi well just time urself jamani mbona unataka fanya ishu kubwa kumbe kitu kidogo tuu. ng'ombe mzima umeshamla sasa kuwahi dakika 2 tuu unataka ilete ugomvi
 

Oups.... Haya na iwe hivyo.

Wenye maumivu ya wanaume na wapate nafuu.

Amen.
 
Kazi zote my wife naweza nisisaidie, lakini kufunga milango never, hata kama ameifunga lazima niipitie upya kuhakikisha.
 
Pole mamy hapo ndo huwa nanuniwa sometimez maana lazima ningesema kama nimekwazika .
 
Hili ni tatizo naweza sema kuwa ni la kihistoria,kwani nililiona tangu kwa wazazi wangu,baba yangu naweza sema alikuwa mkoloni(RIP) kwake muda ilikuwa ni muhimu sana,tulikuwa tunaenda kanisani kwa miguu kwani ilikuwa 10mins walk mpaka kanisani na tulikuwa tunaenda kama familia,mama(RIP) always alikuwa mtu wa mwisho na baba alikuwa anakasirika sana kumsubiri mama.My wife was the same,mtapata breakfast pamoja ready to go,mnaweza hata toka pamoja ndani mara amesahau kitu anarudi...........lol!,was getting pissed off.........Na hapo it was just two of us,with washers for dishes and clothes

Tuna thamini sana uwajibikaji wenu kama mama wa familia lakini nanyi muwe mnawajibika na muda basi.
 
Pole sana dada, siyo wanaume wote wako hivyo, binafsi wa kwangu kwa kweli huwa tunasaidiana.
 
Bado hajakukwida usiku kucha
acha nile maisha mie
naamka zangu huyooo bafuni ....
duh
unafanya wengine tuonekane machiz ofcin,

nimejikuta nacheka sasa naulizwa nacheka nn,
nikasingizia nakumbukia ushind wa man
 
Kazi zote my wife naweza nisisaidie, lakini kufunga milango never, hata kama ameifunga lazima niipitie upya kuhakikisha.
hapa unaogopa wanaweza wakatoroka usiku au wezi wasiingie
 
haya mambo ya chumbani nyie mnaleta barazani angali humu jf tuna teenagers nao unataka wachangie,waulzeni wakbwa wenzenu
 
Mmh mbona kila siku ni post za matatizo ya ndoa 2?sijawahi ona uzi uloletwa kuonyesha mema na raha ya ndoa,hv ndoa ni matatizo tu?mbona mwatutisha tulio single?
 

mambo ni yale yale, coz men use the same rule all over the world, and if there is some changes, another problem will arise! Cha Maana mwombe Mungu awajalieni hekima kwenye ndoa yenu
 

Asprin nampenda na kumheshimu mume wangu
kwa hiyo kuandika humu si kumvua nguo , ila nilikasirika sana na nikashindwa kumwambia, na yeye pia ametambua kuwa nimekasirika sana. nilichokuwa nataka ni kuwa nilikosa wa kumuuliza nifanyeje nikaamua kuuliza. na kuuliza si ujinga, kuliko ningerudi home leo nimenuna, ni bora nimeuliza na nimepata solution.

kama wewe uko hivyo pia naomba ujirekebishe maana huwa mnatuumiza sana.
 
hiyo na kupigiwa honi well just time urself jamani mbona unataka fanya ishu kubwa kumbe kitu kidogo tuu. ng'ombe mzima umeshamla sasa kuwahi dakika 2 tuu unataka ilete ugomvi

mzabzab unanitia mashaka kwanza wewe ni mwanaume/mwanamke?
na je umeoa au umeolewa?
maana afadhali apige honi bila kufoka, mtu anakupigia honi huku anafoka na keshamwambia mlinzi afungue geti anaanza kutoka kwa hiyo mm nitoke ndani nakimbia kama mtoto kulikimbiza gari. hiyo ni sawa? usiseme kitu kabla hakijakukuta.
 
pole sana,siku nyingine uwe unajiendea tu na daladala ili kupunguza bughuza kama hizo.We ukichelewa mwambie atangulie!
 

Jamani si umwambie huyo mumeo nyumbani, au ni member humu ndani!

I understand how you feel, lakini ungemfanya na mumeo aelewe ingesaidia. Kuliko sympathy tunazokupa hazitasaidia sana, sana sana naweza kukushauri nawe ununue gari lako ili kila mtu aende kazini kivyake; is it applicable to your case?
 
I hate waiting, hizo habari za kumpikia chai, sijui nini siyo ruhusa za kufanya akusubiri hapo nje. Keep time wewe ni mtoto wa kiafrica acha habari za kushindana utakuja letewa small house bure. Kikubwa ni kwamba you should know your man better, ikibidi jitahidi uwe unakuwa wa kwanza kutoka.!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…