Hii ni halali kweli? Huku si kuumizana?

Hii ni halali kweli? Huku si kuumizana?

Na mawasiliano siku hizi yalivyorahisishwa mtu anaweza kuwa yuko Frankfurt anapanga kujirusha na mpenzi wake wa zamani yuko kasulu.. Chezeya technology weye!!!

Umeona eeh! Utata mtupu!
 
Wadau habari za jioni,poleni na kazi,
Watu Wameoana,wamezaa watoto 2/3. Mme/Mke anakuonyesha picha za Boyfriend/Girlfriend wake kipindi wako chuo kwenye album yake.yuko yeye katikati halafu pembeni kushoto na kulia marafiki zake.Hii imekaaje?

Na wewe muonyeshe zako, tena zile mlizopiga mkiwa mmekaa ki-hasara hasara.
 
Hicho kitu hata mimi kilishawahi kunitokea kwa mpenzi wangu. lakini wala sikua na maumivu hata kidogo nilichukulia kitu cha kawaida tu....... badae akaanza kusema simpendi kwanini simuonei wivu? na ndivyo nilivyo nikishajua kunakitu unakifanya au unataka kunionyeshea kitu fulani ili roho iniume au nione wivu huwaga siruhusu kitu cha namna hiyo kwangu, raha jipe mwenyewe.
 
Na wewe muonyeshe zako, tena zile mlizopiga mkiwa mmekaa ki-hasara hasara.
Nikifanya hivyo mimi ndo ntaumia zaidi kwa wivu,coz mimi siwezi mwanaume huwezi kuwa na picha za utupu,yeye akikuonyesha unaweza lia na kumpigia magoti kuomba suluhu....
 
mbona kawaida hata mdingi wangu alituonyesha girlfriend wake wa kwanza mambo ya kawaida sana
Mhhh,mother pia aliona hiyo kitu?huwa hawachelewi kusema una mtoto wa nje na yule girlfriend wako.....
 
Mhhh,mother pia aliona hiyo kitu?huwa hawachelewi kusema una mtoto wa nje na yule girlfriend wako.....

maza kkaona ila kama ana watoto nje haituhusu ili hali hajatutambulisha haitupi shida
 
kama ulichukua kitu used hakuna chaajabu labda kama hakukueleza b4 kwamba alikuwa na mtu but kama alikwambia alikuwa na mtu sio issue kukuonyesha picha ya m2 wake wa zamani!na mind you penzi huwa halifi akikumbushiwa atagawa matutamu tena !
 
Mh inaweza isiwe mbaya lakini anafanya hvyo kwa maana ip hasa .na anasema maneno gan wakati anakuonesha picha hyo .mana kama anamsifiasifia ni balaa hapo
 
Yeye za zamani...naye amuoneshe za ma bar-maid wake,za hivi karibuni!!
 
Kwa hiyo ndio hatutaliona tena lemba lile hadi Eid ndogo au miaka 52 ya uhuru wa Tanganyika, whichever comes first!? 🙂🙂
Hahahahahahahaha hapana tutaliona soon.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Hahahahaha sasa pengine ana historia nae huyo ex wake jamani hebu acheni hizo tatizo liko wapi yeye si tayari kasha kua wako. Labd huyo ex wake ndie alimsaidia kumpa vibomu wakati wako shule na ndivyo vilivyomfanya afike hapo. Hahahahahahah enewei naamini kutakua na sababu muhimu . Mimi nikiiona picha ya ex wake na kama namzidi kwa uzuri mbona atakoma nitamtania mpaka ajute. nikiona jamaa hanielewi basi na mimi natafuta picha yoyote hata kama sikuwahi kua na ex namwambia huyu alikua ex wangu nilimpenda sana ili iwe ngoma droooooo.
Ngoma iwe Droo,kutafuta picha yoyote...duuu nimeipenda sana blessed hiyooo.
 
Anakuonesha ili iweje?anazitunza ili iwaje?kumbukumbu gani ambayo anaona ni muhimu aendelee kuwa nayo? Hii ni dalili ya kukosa ustaarabu! Najiuliza ikitokea siku wakakutana na kubadilshana mawasilino kisha wakaanza kusimuliana enzi zileee huku picha ikiangaliwa kila mara ili kurudisha fikra nyuma je unatarajia nn hapo?...mm sioni mantiki kabisaaa
kweli bora zichanwe banaaa
 
Unajua tunatofautiana mitazamo na yote ipo sawa. Mimi akinionyesha wala sijikii vibaya cha msingi kwangu ni uaminifu wake tu. Huenda ana sababu za msingi za kutunza picha hizo na ndio maana anazo. Kwa kumuonyesha kua sijali nitamuuliza anajisikiaje anapoziangalia picha hizo.

Atakuambia anajisikia vibaya, kumbe anajisikia vizuri sana anampigia hata simu kwamba wakutane wapi ili wakumbushie.
 
inategemea na jinsi mlivyo, na namjua dada mmoja hivi,ameolewa ila akiwa na mume wake akamuona demu mkali amepita anamshtua mume wake amuangalie huyo demu , she is o.k with that .
 
picha hazina tatizo hizo ligi labda ukiwa empty mfukon ndio utalianzisha.. PICHA TU.. labda km hizo za siku hizi wanapiga wakiwa vibaya vibaya hapo sawa, ila km niya kawaida ina shida gani.! tufanye mambo ya maendeleo ndani ya nyumba huo wivu peleka kwenu
 
Atakuambia anajisikia vibaya, kumbe anajisikia vizuri sana anampigia hata simu kwamba wakutane wapi ili wakumbushie.
Cha msingi ni uaminifu na mawasiliano unapoona kitu kisichokupendeza ni vema kuambizana
 
Ngoma iwe Droo,kutafuta picha yoyote...duuu nimeipenda sana blessed hiyooo.
Hahahahaha issue si kuumizana tu hiyo mbona rahisi sana hata picha ya classmate inatosha halafu unamwambia huyu ulimpenda sana . Tena unatafuta picha ya mtu handsome kumzidi mbona atajinyonga.
 
Back
Top Bottom