Hii ni aina gani ya maneno

Hii ni aina gani ya maneno

Sentensi za kiswahili huanza na kiima kisha kiarifu. Kimuundo sentensi yako si fasaha. Ilipaswa kuwa
-Hajafika hapa tangu jana.
Na kwa muundo huo hapo kiima si dhahiri (kiima kapa) maana hakionekani bali kinafahamika, ni YEYE.
Neno TANGU ni Kihusishi cha Wakati kama yalivyo maneno-kabla ya...na baada ya...
 
Hicho ni kivumushi, kwasababu mara nyingi kivumishi huwa mbele ya Nomino au Kiwakilishi..... sasa katika sentensi yako hapo kuna Nomino kapa. Ukisema 'Tangu jana hajafika" sehemu iliyopigiwa mstari ni kivumuishi kirejeshi.
 
Sentensi za kiswahili huanza na kiima kisha kiarifu. Kimuundo sentensi yako si fasaha. Ilipaswa kuwa
-Hajafika hapa tangu jana.
Na kwa muundo huo hapo kiima si dhahiri (kiima kapa) maana hakionekani bali kinafahamika, ni YEYE.
Neno TANGU ni Kihusishi cha Wakati kama yalivyo maneno-kabla ya...na baada ya...

Hapo umenikosha kwa kweli
 
Kweli sentesi yake ni ya muundo wa zamani na si sahihi.
SAHIHI: Hajafika hapa tangu jana. -Hicho ni Kielezi cha wakati.
 
Back
Top Bottom