Hii ndoto ina maana gani?

IRINGA ONE

Senior Member
Mar 19, 2015
139
96
Habari Jf , Naomba Niende Moja Kwa Moja Kwenye Mada, Mimi Ni Mwanaume Wa Miaka 36 Ambaye Nimesoma Mpaka Ngazi Ya Kati, Historia Ya Elimu Ni Kuwa Kidato Cha 2 Hadi 4 Nilikosa Ada Hivyo Kupata Adha Nyingi Sana, Ikiwemo Kurudishwa Nyumbani Na Kupigwa Viboko Kwa Miaka Yote Hiyo Pale Ninapoenda Nyumbani Na Kurudi Bila Ada! Tatizo Ni Hili, Baada Ya Kupata Ajira Mkoa Fulani Nimekuwa Nikiota Nipo Shule Nafukuzwa Kuwa Sijalipa Ada Na Adha Nyingine, Ambapo Baada Ya Kutoka Ndotoni Huwa Na Mfadhaiko Sanaaa Na Mapigo Ya Moyo Kuwa Juu. NB. KUMBUKA DENI LA SHULE NILISHALIPA WAKATI NACHUKUA VYETI HIVYO SIDAIWI. Wandugu naja kwenu kwa utabiri wa ndoto hii, AHSANTENI.
 
Bado unasumbuliwa na adha mbalimbali ulizopitia. Mambo hayo yameingia mpaka sub conscious yako. Vumilia kitambo yatakwishaa.
 
ni kitu ambacho kilikuumiza sana moyoni na bado kinakusumbua hata baada ya kulipa deni bado kovu limebaki moyoni mwako kwa yale maumivu moyoni uliyoyasikia (like,why me)..omba kwa Mungu wako akurehemu kovu liishe, wasamehe wazazi wako kwa kutoweza kulipa ada hiyo kwa kipindi kile hadi ukawaunachapwa, ni maisha waelewe ila ilikuumiza moyoni..pole sana, usipoomba msaada kwa Muumba wapo hiyo hali haitapita
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom