Hii ndoto ina maana gani?

LA7

JF-Expert Member
Aug 26, 2019
455
1,665
Naombeni mnitafsirie hii ndoto,

Najua tunaotaga ndoto nyingi ila kuna ndoto ukiota inakuwa ngumu kuisahau

Ilikuwa hivi:

Sikumbuki tulikuwa wangapi ila ilikuwa ni zaidi ya watu watatu, tukiwa tunatembea pembezoni mwa reli mara likaja treni la mizigo likawa limepooza mwendo, tukaomba lifti tukapanda mimi nikawa nimekaa na dereva.

Sasa kufika kwa mbele tukakuta hakuna reli yaani ikawa tu njia ya kawaida ya vumbi nikamuuliza dereva akaniambia nichukue nimsaidie kuendesha.

Kweli nikawa naendesha japo njia ilikuwa mbovu sana makorongo na magogo mengi ila nilijitahidi sana kuipitisha treni katika njia nzuri hata kuipitisha mashambani nikikuta njia mbovu sana lakini kulikuwa na uhakika wa 100% mia kwamba huko mbele tutaingia kwenye reli.

Naombeni tafsiri ya hii ndoto.

MSHANA JR nakusubiria hapa.
 
Unaonekana una nyota ya uongozi. Reli mara nyingi inanyooka, ni mara chache sana kukuta imepinda. Uongozi hautaki mtu mbabaishaji, na wakati huohuo anatakiwa kuwa mtu wa haki. Unaoneokana hupendi kudhurumu haki za wengine; hiyo ni sifa kuu ya viongozi.

Unesema kuna mahala ilibidi dereva wa train akuachie usukani, na wewe ukamudu kuendesha train mpaka kukaribia njia nzuri, hiyo maana yake kiongozi wakati fulani hupitia mambo magumu (nyakati ngumu) lakini hapaswi kukata tamaa na badala yake ajitahidi kuishinda hali hiyo ngumu na hatimaye kupita mapito na kurejea hali njema.

Dunia iliumbwa yenye milima na mabonde, vivyo hivyo katika maisha yetu, tukipata mema, tujue kuna wakati tutakabiliwa na ugumu. Hii ni kutokana na kanuni za asili zilizoko hapa duniani; kwa kila jema utakalopata basi ujue kuna kinyume chake (action and reaction are equal but in opposite direction).

Kikubwa tunachopaswa kuzingatia ni uvumilivu tunapokutwa na magumu; maana yanaweza kutangulia mabaya kabla ya mema; hapa wengi hukata tamaa na kuacha mazuri yanayokuja. Tuwe na ustahimilivu!
 
Niambie kuhusu uchumi wako, ndoto inaonyesha huu ndio muda wako wa mafanikio
 
Ndoto yako ni nzuri sana hapo inaonyesha ww na rafiki zako kutakua na raisi waziri mkuu na makamu wake huyo dereva alikua magufuli alipoona mambo magumu akakupa ww nchi uiongoze. Umeona hali ilivyo kwenye uongozi?

Basi msimlaumu bi tozo hata yeye kajitahidi sana
 
  • Thanks
Reactions: LA7
Niambie kuhusu uchumi wako, ndoto inaonyesha huu ndio muda wako wa mafanikio
ndo nimehamia arusha toka singida nimefungua ofisi ya ufundi simu radio tv studio kurusha movie nyimbo nk. Ipo na mwezi mmoja sasa
 
Unaonekana una nyota ya uongozi. Reli mara nyingi inanyooka, ni mara chache sana kukuta imepinda. Uongozi hautaki mtu mbabaishaji, na wakati huohuo anatakiwa kuwa mtu wa haki. Unaoneokana hupendi kudhurumu haki za wengine; hiyo ni sifa kuu ya viongozi.

Unesema kuna mahala ilibidi dereva wa train akuachie usukani, na wewe ukamudu kuendesha train mpaka kukaribia njia nzuri, hiyo maana yake kiongozi wakati fulani hupitia mambo magumu (nyakati ngumu) lakini hapaswi kukata tamaa na badala yake ajitahidi kuishinda hali hiyo ngumu na hatimaye kupita mapito na kurejea hali njema.

Dunia iliumbwa yenye milima na mabonde, vivyo hivyo katika maisha yetu, tukipata mema, tujue kuna wakati tutakabiliwa na ugumu. Hii ni kutokana na kanuni za asili zilizoko hapa duniani; kwa kila jema utakalopata basi ujue kuna kinyume chake (action and reaction are equal but in opposite direction).

Kikubwa tunachopaswa kuzingatia ni uvumilivu tunapokutwa na magumu; maana yanaweza kutangulia mabaya kabla ya mema; hapa wengi hukata tamaa na kuacha mazuri yanayokuja. Tuwe na ustahimilivu!
Nashukuru mungu huwa nafanya kila niwezalo kumpa mtu haki yake hasa kama nadaiwa
 
dogo niliyemtuma dukani karud na mangi nyumbani

hela niliyompa ya zamani akaitupa jalalani
 
Naombeni mnitafsirie hii ndoto,

Najua tunaotaga ndoto nyingi ila kuna ndoto ukiota inakuwa ngumu kuisahau

Ilikuwa hivi:

Sikumbuki tulikuwa wangapi ila ilikuwa ni zaidi ya watu watatu, tukiwa tunatembea pembezoni mwa reli mara likaja treni la mizigo likawa limepooza mwendo, tukaomba lifti tukapanda mimi nikawa nimekaa na dereva.

Sasa kufika kwa mbele tukakuta hakuna reli yaani ikawa tu njia ya kawaida ya vumbi nikamuuliza dereva akaniambia nichukue nimsaidie kuendesha.

Kweli nikawa naendesha japo njia ilikuwa mbovu sana makorongo na magogo mengi ila nilijitahidi sana kuipitisha treni katika njia nzuri hata kuipitisha mashambani nikikuta njia mbovu sana lakini kulikuwa na uhakika wa 100% mia kwamba huko mbele tutaingia kwenye reli.

Naombeni tafsiri ya hii ndoto.

MSHANA JR nakusubiria hapa.
Kuna jambo linaloelekea kuyumba nawe ndio utakuwa mwokozi wake! Inawezekana ni la kifamilia, ukoo kazini ama ishu tu za kimaisha kwa washkaji nk
 
Naombeni mnitafsirie hii ndoto,

Najua tunaotaga ndoto nyingi ila kuna ndoto ukiota inakuwa ngumu kuisahau

Ilikuwa hivi:

Sikumbuki tulikuwa wangapi ila ilikuwa ni zaidi ya watu watatu, tukiwa tunatembea pembezoni mwa reli mara likaja treni la mizigo likawa limepooza mwendo, tukaomba lifti tukapanda mimi nikawa nimekaa na dereva.

Sasa kufika kwa mbele tukakuta hakuna reli yaani ikawa tu njia ya kawaida ya vumbi nikamuuliza dereva akaniambia nichukue nimsaidie kuendesha.

Kweli nikawa naendesha japo njia ilikuwa mbovu sana makorongo na magogo mengi ila nilijitahidi sana kuipitisha treni katika njia nzuri hata kuipitisha mashambani nikikuta njia mbovu sana lakini kulikuwa na uhakika wa 100% mia kwamba huko mbele tutaingia kwenye reli.

Naombeni tafsiri ya hii ndoto.

MSHANA JR nakusubiria hapa.
@Mshana Jr
 
Naombeni mnitafsirie hii ndoto,

Najua tunaotaga ndoto nyingi ila kuna ndoto ukiota inakuwa ngumu kuisahau

Ilikuwa hivi:

Sikumbuki tulikuwa wangapi ila ilikuwa ni zaidi ya watu watatu, tukiwa tunatembea pembezoni mwa reli mara likaja treni la mizigo likawa limepooza mwendo, tukaomba lifti tukapanda mimi nikawa nimekaa na dereva.

Sasa kufika kwa mbele tukakuta hakuna reli yaani ikawa tu njia ya kawaida ya vumbi nikamuuliza dereva akaniambia nichukue nimsaidie kuendesha.

Kweli nikawa naendesha japo njia ilikuwa mbovu sana makorongo na magogo mengi ila nilijitahidi sana kuipitisha treni katika njia nzuri hata kuipitisha mashambani nikikuta njia mbovu sana lakini kulikuwa na uhakika wa 100% mia kwamba huko mbele tutaingia kwenye reli.

Naombeni tafsiri ya hii ndoto.

MSHANA JR nakusubiria hapa.
Hongera, ndoto nzuri kwako

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom