Hii ndo timu ya kushangilia bila presha

Hii ndo timu ya kushangilia bila presha

Nao pia watafungwa kwani ubelgiji na spain ni timu ipi yenye mastaa zaidi. Ubelgiji haiwafikii hata argentina kwa mastaa
 
Kama unataka kufurahia michuano ya fainali za kombe la dunia kwa kushangilia timu isiyokupa presha ya kufungwa basi shangilia UBELGIJI(Belgium) huko utakutana na wachezaji wakali kama:-Mignolet(Liverpool),V.Kompany(M.city),Lukaku,Miralas(Everton),Fellaini,Januzaj(M.United) n.k

Mmmmh, mimi nadhani kama hutaki ugonjwa wa moyo shangilia Uholanzi (Netherlands) kaka. for sure utanenepa
 
hakuna sie jua kuwa Brazil ndo bingwa, hapa tunaenda kushuhudia already determined results.

Determined results???
Hamna porojo huku mkuu. Unavuna ulichopanda pia bahati iwe upande wako! FULL STOP
 
mkuu ndio chama langu hili sio unahama timu kwa ajili ya mchezaji mmoja

THE THREE LIONS ndo chama langu pia! Hata wakiitwa underdogs, POA tu! Roho yangu imechagua hapo. Ukiniuliza kwa nini, sijui, ila nawapenda sana!! Leo Fingerz crossed!
 
Timu ya taifa wengine tumechoka kuulizwa hivi Tanzania hakuna timu ya mpira,
Na kwa jinsi tunavyopenda mpira roho inauma sana
Sasa sisi huyo Ngassa trial ya westham tu ilimshinda, si kwamba Redknapp akumkubali kwa kipaji/skills bali Ngassa alishindwa fitness test za mpira wa uingereza.
Ni kweli
Binafsi naona serikari imekosa mkakati wa kutupa national pride katika michezo and more needs to be invested it can boost national morale and solidarity in times like this you know.
Nakubaliana na wewe mkuu ingawa Raisi Kikwete alijitahidi kuhamasisha michezo hasa mpira wa miguu lakini haikusaidia
 
Na kwa jinsi tunavyopenda mpira roho inauma sana

Nakubaliana na wewe mkuu ingawa Raisi Kikwete alijitahidi kuhamasisha michezo hasa mpira wa miguu lakini haikusaidia
Nilichokiona mimi kupitia kipindi cha TV ni kocha wa timu ya Musoma or Shinyanga akisisitiza mpira wa leo unavyochezwa na kujitahidi kutoa nidhamu kwenye chama chake, katika swala hilo hilo wachezaji wazamani pia wamekiri sikuhizi wachezaji hawana nidhamu na awaheshimu nafasi yao kulinganisha na wao ambao wengine walikuwa wakikimbia kila asubuhi kwa ajili ya stamina tu, licha ya mazoezi ya mchana.

Serikari inatakiwa kuweka academy ya mpira ndio nitaamini hipo seriously, na academy za michezo mengine. Mfano Kenya kwenye riadha tu kuna clubs kadhaa ambazo zipo sponsored na serikari ama previous successful athletes ambao wanarudisha kwao kutokana na mapenzi ya taifa. Hawa jamaa wanafanya summer camps na wanagharamia wanariadha kipindi hicho cha tizi na matunda yanaonekana as days go Kenya is getting successful, Haile Gebresellasie amekopi mfumo huo matunda yanaonekana, sie wambulu tunawaangalia tu wakati jamaa wakiwekeza kule wakenya tungewatia adabu.

Kwa hivyo kama tupo serious na matokeo ya baadae lazima tuanze mapema na vijana, leo timu ya ivory coast karibu wote wamecheza pamoja wakiwa wadogo tangia academy na wanajuana vizuri tu, huko ndio kuwa serious. Wanariadha, wakimbiaji wakubwa wa kimataifa wanajuana tangia kwenye junior championships, where it that investment in Tanzania kwa vijana. Mastaa wengi wa UMISETA leo ndio walevi wakubwa.
 
Nilichokiona mimi kupitia kipindi cha TV ni kocha wa timu ya Musoma or Shinyanga akisisitiza mpira wa leo unavyochezwa na kujitahidi kutoa nidhamu kwenye chama chake, katika swala hilo hilo wachezaji wazamani pia wamekiri sikuhizi wachezaji hawana nidhamu na awaheshimu nafasi yao kulinganisha na wao ambao wengine walikuwa wakikimbia kila asubuhi kwa ajili ya stamina tu, licha ya mazoezi ya mchana.

Serikari inatakiwa kuweka academy ya mpira ndio nitaamini hipo seriously, na academy za michezo mengine. Mfano Kenya kwenye riadha tu kuna clubs kadhaa ambazo zipo sponsored na serikari ama previous successful athletes ambao wanarudisha kwao kutokana na mapenzi ya taifa. Hawa jamaa wanafanya summer camps na wanagharamia wanariadha kipindi hicho cha tizi na matunda yanaonekana as days go Kenya is getting successful, Haile Gebresellasie amekopi mfumo huo matunda yanaonekana, sie wambulu tunawaangalia tu wakati jamaa wakiwekeza kule wakenya tungewatia adabu.

Kwa hivyo kama tupo serious na matokeo ya baadae lazima tuanze mapema na vijana, leo timu ya ivory coast karibu wote wamecheza pamoja wakiwa wadogo tangia academy na wanajuana vizuri tu, huko ndio kuwa serious. Wanariadha, wakimbiaji wakubwa wa kimataifa wanajuana tangia kwenye junior championships, where it that investment in Tanzania kwa vijana. Mastaa wengi wa UMISETA leo ndio walevi wakubwa.
Mkuu kote uko sawa na umechambua vizuri sana. Na hii inatakiwa tufuate mfano wa serikali ya Senegal baada ya timu ya Taifa kuwa inasua sua mara kwa mara walichofanya ni kusitisha timu ya Taifa kushiriki na kuanza kuinoa upya na matunda yake yameonekana kina FADIGA, SULEYMAN CAMARA, HENRY CAMARA, DIAO(DJAO), EL HADJI DIOUF, DIOP na wengineo, si unaona ujio wao ukawa na mabadiliko ya hali ya juu.

Nakubaliana na wazo lako kwahiyo kama itawezekana na sisi tuanze kuandaa academy nina uhakika baada ya miaka kadhaa tunaweza kuja na timu inayoeleweka.

Hapo nyeusi kwa mwalimu wa Musoma/Shinyanga hajakosea hata kidogo ni kweli wachezaji wetu akipata jina kidogo basi nidhamu lazima ishuke na kuanza kujisikia anajiona ameshafikia kiwango cha hali ya juu na nidhamu kushuka kumbe michezo ni pamoja na nidhamu ili upate kuwa na mafanikio sio kuridhika na kuwa na jina Tanzania.

Ukiachilia mbali Ngasa, kuna mchezaji kama NIZAR KHALFAN(Vancouver white caps) alikuwa anakuja vizuri sijui na yeye kimemsibu nini maana hasikiki tena kabisa. Anaetuwakilisha kwa sasa nafikiri ni MBWANA SAMATA sidhani kama kuna mwingine
 
Three Lions because i have unconditional love with them.

Extra
All the African representatives and Holland because they have large numbers of blacks, equality of selection based on talent and their attitude towards racism.
Mkuu na FRANCE nao
 
Kama unataka kufurahia michuano ya fainali za kombe la dunia kwa kushangilia timu isiyokupa presha ya kufungwa basi shangilia UBELGIJI(Belgium) huko utakutana na wachezaji wakali kama:-Mignolet(Liverpool),V.Kompany(M.city),Lukaku,Miralas(Everton),Fellaini,Januzaj(M.United) n.k

kwenye mpira vinavyocheza si majina ndugu ni zaidi ya hapo
 
hakuna sie jua kuwa Brazil ndo bingwa, hapa tunaenda kushuhudia already determined results.
Mkuu bado, michuano ya mwaka huu wengi wamejiandaa usichukulie kirahisi rahisi tuendelee kufanya subra
 
Unaota mchana; kwa lipi hao Brazil wanastalihi sifa hizo? Kuifunga Croatia? Subiri utaona watakavyofanywa hivi karibuni!


Sent from my iPhone using JamiiForums

Aisee kama ni utabiri nimeshinda! Yaani kichapo ilichopata mikononi kwa wajukuu wa Hitler kimesambaratisha mashabiki wote hadi wabrazil wenyewe!


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Back
Top Bottom