Hii ndiyo TBC halisi

Hii ndiyo TBC halisi

…ngoja nicopy hili bandiko, nikitoka kwenye miangaiko yangu ya kutafuta ugali(watz hatuli mikate) nikae chini nitafakari…lkn kwa ufupi tu ninaweza kuifananisha TBC na mamba amayetafuna windo lake huku machozi yakimbubujika, hapo ndio utajiuliza huyu mamba anakiurumia hicho kiumbe acho tafuna ama anafurahia utamu wa nyama?…
 
Hakuna kama tbc nchi hii wengine wasisite kuiga mfano wao.
 
Kwako SUPER PREDATOR mwandishi wa hii tamthilia ya Nyumbu na Simba, ni mhusika yupi kati ya hao TBC na ITV amehegemea katika maisha halisi ya hao wanyama?

Mkuu watu wanapenda kujua ukweli ndiyo maana wakubwa wanapenda kuangalia ITV, na kwa maana hiyo ITV inapata matangazo mengi zaidi kuliko TBC, TBC wanategemea ruzuku ya kodi zetu ndiyo maana wao hawajali sana hata kama hawapati watazamaji wengi.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu ukiendelea namna hi sheria ya mtandao wala haitakuja kukugusa but watu wazima tumekuelewa sana. Big up cause nimegundua siku hizi hata wafanyakazi wa TBCccm (akiwepo na mkuu wao) nao kwakua ni watu wazima wanaangaliaga super brand badala ya kwao.
 
TBC ya Leo ni ile inayoonyesha upendo na mambo mazuri tu. Kwa mfano kama wanaonyesha kipindi cha wanyama basi utaona nyumbu wanakula majani bila bughuza yoyote na pembeni utaona simba wamepumzika, na simba wengine wanawabeba watoto wao kwa upole kwenye midomo yao.

Harafu utasikia mtangazaji wa tbc anasema nyumbu ni wanyama wapole sana na wenye ushirikiano wa hali ya juu sana, hawagombani wala kufokeana. Baada ya hapo wanaamia kwa simba utasikia simba ni mnyama mpole sana na hasa kama ameshiba, tena huwabeba watoto wao kwa upole sana.

ITV ipo vile vile wao utaona nyumbu anavyohangaika kutafuta malisho na maji, nyumbu wanavyopigana, nyumbu wanavyokufa kwenye mazingira tofauti. Harafu utamuona simba anavyowinda, anavyokula, anavyoua simba watoto na wanavyouana wao kwa wao.

Harafu utamsikia mtangazaji anakwambia nyumbu hula kwa tahadhali sana kwa sababu anajua muda wowote atakamatwa na kuliwa na wanyama wanaokula nyama, utamsikia mtangazaji anakwambia simba anapowinda huwa hana huruma mpaka apate chakula chake na kushiba na wakati wa kula simba huwa hawana ushirikiano Mara nyingi utakuta wanagombana wakati wa kula.

Sasa kutokana na utangazaji wa aina hiyo watoto wengi wanapenda kuangalia TBC, na kutokana na utangazaji huo watu wazima wengi wanapenda kuangalia ITV hivi ni kwa nini?.
Mkuu wenye akili zao tumekuelewa hongera sana
 
…ngoja nicopy hili bandiko, nikitoka kwenye miangaiko yangu ya kutafuta ugali(watz hatuli mikate) nikae chini nitafakari…lkn kwa ufupi tu ninaweza kuifananisha TBC na mamba amayetafuna windo lake huku machozi yakimbubujika, hapo ndio utajiuliza huyu mamba anakiurumia hicho kiumbe acho tafuna ama anafurahia utamu wa nyama?…

TBC ina watangazaji makini na waelewa sana ila wanalazimishwa kufuata maelekezo ya wakubwa
 
ITV superbrands milele...
TBC wanapata ruzuku za serikali lazma waoneshe utiifu ivi piga mfano wananchi tusingekua na tv kama ITV tungekua tunaongopewa tu vituko vya serikali ya ccm vina mwisho
 
Back
Top Bottom