Hii ndio Silaha Kuu ya CHADEMA!.

Hii ndio Silaha Kuu ya CHADEMA!.

CHADEMA hawana mshikamano wala ushirikiano kama taasisi ndani na nje bali wana baadhi ya viongozi wachache sana ambao wana uwezo mkubwa katika kuzicheza siasa za Tanzania huku wakisaidiwa kwa kiasi kikubwa na mabadiliko ya kisiasa, kiuchumi na kijamii ambayo hata kama CHADEMA isingekuwepo yangetokea.

Jaribu kuangalia historia ya Tanzania kisiasa, kiuchumi na kijamii kupata picha halisia ili ikusaidie kujenga hoja mbadala kujua siraha kuu ya CHADEMA.

Hata swala la kuwepo kwa katiba halijaanziswa na CHADEMA kama unavyotaka kuaminisha watu hapa JF.

Siraha kuu ya CHADEMA siyo mshikamano na ushirikiano bali ni KUWEPO kwa CCM na serikali yake madarakani kwa muda mrefu ambao umeweza kujenga LUNDO la maswali yasiyo na majibu mbadala, makosa kiutendaji kwa maksudi au kutokujua na chama na serikali kuishi kwa mazoea.

Mambo haya mpaka yamesababisha wananchi katika maeneo mbali mbali kuwachagua viongozi wa vijijini, madiwani na wabunge kutoka vyama vya upinzani ambao hawana hata uwezo ukilinganisha na wale wa CCM. UJUMBE hapa kutoka kwa wananchi ni kusema, TUMECHOKA tunataka wengine tofauti bila kujali UWEZO WAO.
 
mtaji watu ndio jambo la msingi sana kwetu wana chadema .na hii ni kwa sababu ya kuwa na sela nzenye tija kwa jamii nzima inayotuzunguka:yell:
 
Mkuu; kwa nini unasema hivi?
CHADEMA hawana mshikamano wala ushirikiano kama taasisi ndani na nje
Unaweza kututajia walau kumi (10) ambao wewe unakubali kwamba uwezo wao uko juu mno!
wana baadhi ya viongozi wachache sana ambao wana uwezo mkubwa katika kuzicheza siasa za Tanzania


Hata swala la kuwepo kwa katiba halijaanziswa na CHADEMA kama unavyotaka kuaminisha watu hapa JF.
mimi sijasema suala la katiba limeanzishwa na chadema; mimi nimesema CHADEMA wameishinikiza serikali kukubali kuanza mchakato.Wazo kama wazo lilikuwepo toka siku nyingi ila serikali ilikuwa inakwepa kutekeleza mpaka chadema walivyoweka presha kidogo.
Siraha kuu ya CHADEMA ni KUWEPO kwa CCM na serikali yake madarakani kwa muda mrefu ambao umeweza kujenga LUNDO la maswali yasiyo na majibu
Kwa hili uko sawa kabisa.kwa hiyo udhaifu uliopo CCM unaipa nguvu chadema.Hii ni kweli.
 
Asante Chadema kwa kazi nzuri. Jitihada zenu zinaiamsha serikali ya ccm na hivyo kuwajibika. Sasa basi, kuwajibika kwa ccm ni kuongeza ugumu kwa wapinzani kukamata nchi. Kazeni uzi chadema.
 
Cc. RITZ..umeulza kama cdm ndo imeishnkza serkali kuandka katba jbu ni ndio kwanza katba mpya ilikuwa ktk ilani ya uchaguz ya cdm 2005na 2010 ccm wakapora hii ajenda kwa udhaifu wa serkal ye2 isngekubal bila force ya cdm
 
Hivi CHADEMA ndiyo wameishawishi serikali ya CCM suala la katiba?

Ritz, Unauliza jibu? Kwani ccm wanasemaje kwenye ilani? Chadema na CUF ilani zao zinataka katiba mpya. CCM mnabambia kwa nyuma
 
Unapoitupa silaha yako na kubaki mikkono mitupu, ni kwa vipi basi unaweza kushinda vita?
 
Cc. RITZ..umeulza kama cdm ndo imeishnkza serkali kuandka katba jbu ni ndio kwanza katba mpya ilikuwa ktk ilani ya uchaguz ya cdm 2005na 2010 ccm wakapora hii ajenda kwa udhaifu wa serkal ye2 isngekubal bila force ya cdm

Mkuu, unasema je kuhusu hatua ambayo katiba imefikia sasa?
 
CHADEMA ni chama makini sana, asiyetaka aende akojoe akalale! utawasikia magamba wanavyokuja kuhororoka hapa sasa hivi.
 
Mkuu, unasema je kuhusu hatua ambayo katiba imefikia sasa?
Hivi wewe si unajiita Kiongozi wa ACT? Lakini sijawahi kuona umeikosoa CCM ila unaisifia tu. kama nakosea nioneshe. ACT ni mpinzani wa nani? Chadema tu au? Kiukweli mimi huwa sielewi hasa wewe na Mwl. Kaijage maana ni kuiponda Chadema na kuisifia CCM mwanzo mwisho.
 
Jambo la muhimu zaidi ni CHADEMA kujipambanua kwamba kiko kwa malsahi ya wana nchi kuhakikisha rasilimali za nchi hii kwanza nikwamanufaa ya wananchi, na kama ndiyo hivyo basi ili Chama hiki kiweze kufanikiwa kupambana na propaganda za chama tawala kinabidi kupata sapoti kubwa kutoka kwa wanachiwenye mapenzi mema na nchi hii. kwani iwe chama tawala au cha upinzani bila wananchi kukisapoti hakifiki popote.
Kwa jinsi ilivyo basi wananchi tunajukumu kubwa sana la kutoa sapoti kwa chama ili kiweze kufikia malengo

Habari njema ni kuwa watanzania japo kwa kasi ndogo wameanza kuamka, sio rahisi kuwadanganya kama ilivyokuwa hapo awali, kwa hiyo tutafika tu, no matter how long it will take.
 
Thanks Mods
Leo nimeondoa like yangu kwa huyu mnafiq betlehem
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom