Hii ndio ndege ya Rais Wetu

Vitalis Konga

Senior Member
Sep 22, 2018
127
231
FB_IMG_1577365499030.jpg


Na:Vitalis John Konga
(Mwana Vasamwenda)

Gulfstream G550 Jet hii ndio ndege inayotumiwa zaidi na Rais wa Tanzania Mh John Pombe Joseph Magufuli katika ziara mbali mbali ndani na nje ya nchi ingawa tunazo Dutch Fokker F-28 na Dutch Fokker F-50 ambazo anaweza kuzitumia pia. Ndege hii kwa majina ya utani huwa inaitwa Flying Ikulu au Flying Statehouse. Ilinunuliwa mwaka 2004 wakati wa uongozi wa Rais mstaafu Mh B.W. Mkapa kwa kiasi cha takribani Dolar Million 40 Ingawa sasa inauzwa Dolar Million 60.1 cash on hand kama mkopo inakuwa inauzwa ghali zaidi.

Imetengenezwa na kampuni ya General Dynamics Gulfstream Aerospace Unit Iliyoko Georgia-USA, hii ndege inauwezo wa kusafiri takribani kilomita 10700 bila kutua hii ni zaidi ya kuwa hewani kwa masaa zaidi ya 9. Uwezo wake ni kubeba abiria 18 tu, Imesajiliwa kwa namba 5H-ONE.

Ndege kama hii hutumiwa zaidi na marais mf.Rais wa Uganda Mh Y.K.Museveni,Rais wa Nigeria Mh M.Buhari nk, na viongozi wakubwa wa nchi mf waziri wa mambo ya ulinzi wa USA ,wafanyabiashara wakubwa duniani mf Carlos Slim wasanii wakubwa duniani mf P.Diddy.

Uganda walinunua ndege kama hii mwaka 2009 baada ya sisi kuinunua mwaka 2004.Hizi ndege toka zianze kutengenezwa mwaka 2003 hazijawahi kupata ajali duniani,hii ina maana kuwa ni salama zaidi.

ENJOY GOVERMENT PROTECTION IN THE AIR

Vitalis Konga
Njombe Mjini

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuvimbiwa ubwabwa hukooo... Afu unakula na Beer..!!
 
Back
Top Bottom