Jokajeusi
JF-Expert Member
- Jun 1, 2018
- 6,336
- 10,895
Habari Wakuu!
Kanda ya kaskazini inajumuisha Mikoa mitatu ambayo ni mkoa wa Arusha( na Manyara), Tanga na Kilimanjaro. Mikoa hii ni moja ya mikoa iliyobarikiwa karibu kila kitu. Nathubutu kusema kanda ya kaskazini ni zaidi ya nchi ya maziwa na asali. je si kanda ya kaskazini yenye mali asili nyingi kupita kanda yoyote ile. Mali asili zilizopo huko huweza kuingia katika top ten kiulimwengu.
Nikianza na Rasilimali watu. Kanda hii kuna makabila mbalimbali yenye mila na destu zao. Wapo Wachaga, Wapare, Wamasai, Wasambaa, wadigo, wazigua, wabondei, Wameru, Wambulu, wambugu n.k. Kila kabila linavijikabila ndani yake. Hakuna sifa yoyote kiulimwengu ambayo watu wa kanda hii hawana. Kama ni wanawake wazuri hii ndio kanda iliyobarikiwa kuliko kanda zingine. Watoto kutoka Tanga, Watoto kutoka Manyara ndio usiseme kabisa.
Kwa habari ya elimu kanda hii wanatisha. Karibu kila familia kuna zaidi ya watoto wawili wenye shahada. Kila ukoo unawatu wenye shahada mbili au hata tatu. hii tafsiri yake ni kuwa watu kutoka huko wapo vizuri kielimu. Tofauti na kanda nyingine au hata nchi nyingine ambazo unaweza kukuta kwenye familia hakuna hata mwenye elimu ya kidato cha sita. Kutokana na watu kuwa na elimu katika kanda hii ndio maana hata maendeleo yao si haba.
Kwa habari za miundo mbinu kama barabara, reli, viwanja vya ndege, bandari n.k. Kanda ya kaskazini imesheheni. Kuna kiwanja kimoja cha ndege cha kimataifa(KIA) ambacho kinaruhusu ndege kutoka mataifa ya nje kufika kanda hiyo. Pia vipo viwanja vya ndege vidogo vidogo. Ipo bandari ya Tanga ambayo Kanda hii inaweza kupokea meli kutoka sehemu yoyote duniani. barabara ya lami kiasi wamejitahidi ukilinganisha na kanda zingine na nchi zingine. Reli nayo ipo. Nini kimebakia kwenye habari ya miundo mbinu. Jibu ni hakuna.
Huduma za kijamii kama Zahanati, Hospitali, Shule, Vyuo vya ufundi, Vyuo vikuu, Umeme, huduma za kibenki, Makanisa, Misikiti, Vyombo vya habari n.k. Ipo hospitali kubwa ya KCMC ambayo ni moja ya hospitali kongwe na bora katika nchi hii. Kila wilaya kuna Zahanati kama si hospitali ndogo. Vyuo vya ufundi (VETA) Karibu kila kata kama si wilaya vipo. Vyuo Vikuu vinavyotoa kozi mbalimbali vipo. Kanda hii ndio kanda pekee yenye shule nyingi kuliko kanda yoyote hapa duniani na hata baadhi ya mikoa ya nchi fulani barani Afrika. Usishangae katika kata moja kukawa na shule za msingi hata 10, Shule za sekondari tano. Hii ni kusema kuwa wanayohaki kupata elimu wengi. Umeme upo karibu kila kijiji. Vyombo vya habari zikiwemo Redio kadha wa kadha. Huduma za kibenki kila wilaya na hata baadhi ya kata kuna vituo vya kutolea pesa. Huduma za mawasiliano ipo, kila mtandao unashika vizuri. Hakuna tabu ya kufanya miamala ya simu.\
Wasomi na Wataalamu katika kanda hii ni wengi sana. Ndio kanda pekee inayoongoza kwa kuwa na wasomi wengi na wataalamu wengi. Wanasheria, Madaktari, Waalimu, Wahandisi, Wakandarasi, Wanasiasa, Wachungaji, Wahasibu, wataalamu wa mambo ya fedha, Wataalamu wa mawasiliano na kompyuta, Madereva, Makanika n.k. kwenye nchi hii kila fani niliyoitaja hapo wengi wao wanatoka Kanda ya kaskazini.
Rasilimali kama Mbuga za wanyama, Madini, Mlima Kilimanjaro, Bwawa la Nyumba ya Mungu, Mapango ya ambani, Bahari ya Hindi, Maziwa na mito, Ardhi kubwa yenye Rutuba, Tabia ya nchi nzuri, Miti ya matunda n.k. Kilichokosekana hapa ni Gesi na mafuta tuu. lakini hayo mengine yapo kanda ya kaskazini.
Wasanii na watu maarufu. Kanda ya kaskazini ndio kanda pekee yenye wasanii lukuki wanaoeleweka. Wasanii wengi na watu maarufu wengi hutoka kanda hii. Wengi hutoka TANGA, ARUSHA NA MOSHI. Hivyo ni kusema Kanda hii ni moja ya kanda iliyobarikiwa kupita zote.
Ndio Kanda pekee ambayo watu wake wanapenda kwao na kujivunia kwao. Ni watu ambao hawasiti kujitambulisha popote pale. Mtu hata asipoulizwa hujikuta akisema kuwa kwetu ni Moshi, mara home ARA chuga, ooh kwetu Tanga. Hii huifanya kanda hii kuonekana inaubaguzi na umimi kutokana na hulka ya majigambo.
Matajiri na Wafanya biashara wakubwa. Hakuna ubishi kuwa kanda ya kaskazini inaongoza kwa kuwa na watu wenye mpunga na jala la kufa mtu. Atakayebisha ni yule asiyeijua nchi hii vizuri au ambaye hajatembea mikoa mingi katika nchi hii. Karibu kila kata kwenye majiji makubwa hapa nchi huwezi kukuta matajiri kumi bora wa kata hiyo alafu usikute watano wanatoka kanda ya kaskazini. Si Dar es Salaam, si Mbeya, si Mwanza popote pale lazima matajiri wanne au watano katika kata hizo lazima watoke huko kaskazini. Kanda hii inaheshimu pesa sana. Watu wake hawaoni aibu kufanya hata ni shughuli ya kuuza nyanya bila kujali mtu huyo kaenda shule au hajaenda. Wanachoangalia je kuna mpunga basi.
Majambazi, mafisadi na wahujumu uchumi. Ndio kanda pekee inayoweza kutoa Mafisadi, majambazi na wahujumu uchumi kushinda kanda yoyote hapa nchini. Ujambazi wa kimataifa pia umefanya na watu wa kanda hii. Si ajabu mtu kutoka Arusha akienda Kenya kupiga tukio la kijambazi. Hii imepelekea kanda hii kuogopwa na kutokuaminiwa kabisa na kanda zingine hasa kwenye ishu za pesa. Ndio Kanda pekee ambayo hawataki mchezo na mali zao. Si rahisi umdhulumu mtu kutoka kanda hii. Ukisikia kesi ya kuku ng'ombe anauzwa ili kuendesha kesi basi huko kaskazini ndio mtindo.
Ndio Kanda pekee ambayo hawakatai watoto. Na si rahisi kuchukua damu yao.
Ndio kanda pekee inayojiona Superior kuliko kanda zingine. Mtu kutoka huku hata kama hajaenda shule huwezi kumuendesha na kumdharau eti kisa wewe umeenda shule au unavijipesa.
Ikumbukwe kwamba mtu yeyote anaweza kuwa kanda ya kaskazini iwe kwa damu au kuzaliwa huko.
Nawasilisha!
Kanda ya kaskazini inajumuisha Mikoa mitatu ambayo ni mkoa wa Arusha( na Manyara), Tanga na Kilimanjaro. Mikoa hii ni moja ya mikoa iliyobarikiwa karibu kila kitu. Nathubutu kusema kanda ya kaskazini ni zaidi ya nchi ya maziwa na asali. je si kanda ya kaskazini yenye mali asili nyingi kupita kanda yoyote ile. Mali asili zilizopo huko huweza kuingia katika top ten kiulimwengu.
Nikianza na Rasilimali watu. Kanda hii kuna makabila mbalimbali yenye mila na destu zao. Wapo Wachaga, Wapare, Wamasai, Wasambaa, wadigo, wazigua, wabondei, Wameru, Wambulu, wambugu n.k. Kila kabila linavijikabila ndani yake. Hakuna sifa yoyote kiulimwengu ambayo watu wa kanda hii hawana. Kama ni wanawake wazuri hii ndio kanda iliyobarikiwa kuliko kanda zingine. Watoto kutoka Tanga, Watoto kutoka Manyara ndio usiseme kabisa.
Kwa habari ya elimu kanda hii wanatisha. Karibu kila familia kuna zaidi ya watoto wawili wenye shahada. Kila ukoo unawatu wenye shahada mbili au hata tatu. hii tafsiri yake ni kuwa watu kutoka huko wapo vizuri kielimu. Tofauti na kanda nyingine au hata nchi nyingine ambazo unaweza kukuta kwenye familia hakuna hata mwenye elimu ya kidato cha sita. Kutokana na watu kuwa na elimu katika kanda hii ndio maana hata maendeleo yao si haba.
Kwa habari za miundo mbinu kama barabara, reli, viwanja vya ndege, bandari n.k. Kanda ya kaskazini imesheheni. Kuna kiwanja kimoja cha ndege cha kimataifa(KIA) ambacho kinaruhusu ndege kutoka mataifa ya nje kufika kanda hiyo. Pia vipo viwanja vya ndege vidogo vidogo. Ipo bandari ya Tanga ambayo Kanda hii inaweza kupokea meli kutoka sehemu yoyote duniani. barabara ya lami kiasi wamejitahidi ukilinganisha na kanda zingine na nchi zingine. Reli nayo ipo. Nini kimebakia kwenye habari ya miundo mbinu. Jibu ni hakuna.
Huduma za kijamii kama Zahanati, Hospitali, Shule, Vyuo vya ufundi, Vyuo vikuu, Umeme, huduma za kibenki, Makanisa, Misikiti, Vyombo vya habari n.k. Ipo hospitali kubwa ya KCMC ambayo ni moja ya hospitali kongwe na bora katika nchi hii. Kila wilaya kuna Zahanati kama si hospitali ndogo. Vyuo vya ufundi (VETA) Karibu kila kata kama si wilaya vipo. Vyuo Vikuu vinavyotoa kozi mbalimbali vipo. Kanda hii ndio kanda pekee yenye shule nyingi kuliko kanda yoyote hapa duniani na hata baadhi ya mikoa ya nchi fulani barani Afrika. Usishangae katika kata moja kukawa na shule za msingi hata 10, Shule za sekondari tano. Hii ni kusema kuwa wanayohaki kupata elimu wengi. Umeme upo karibu kila kijiji. Vyombo vya habari zikiwemo Redio kadha wa kadha. Huduma za kibenki kila wilaya na hata baadhi ya kata kuna vituo vya kutolea pesa. Huduma za mawasiliano ipo, kila mtandao unashika vizuri. Hakuna tabu ya kufanya miamala ya simu.\
Wasomi na Wataalamu katika kanda hii ni wengi sana. Ndio kanda pekee inayoongoza kwa kuwa na wasomi wengi na wataalamu wengi. Wanasheria, Madaktari, Waalimu, Wahandisi, Wakandarasi, Wanasiasa, Wachungaji, Wahasibu, wataalamu wa mambo ya fedha, Wataalamu wa mawasiliano na kompyuta, Madereva, Makanika n.k. kwenye nchi hii kila fani niliyoitaja hapo wengi wao wanatoka Kanda ya kaskazini.
Rasilimali kama Mbuga za wanyama, Madini, Mlima Kilimanjaro, Bwawa la Nyumba ya Mungu, Mapango ya ambani, Bahari ya Hindi, Maziwa na mito, Ardhi kubwa yenye Rutuba, Tabia ya nchi nzuri, Miti ya matunda n.k. Kilichokosekana hapa ni Gesi na mafuta tuu. lakini hayo mengine yapo kanda ya kaskazini.
Wasanii na watu maarufu. Kanda ya kaskazini ndio kanda pekee yenye wasanii lukuki wanaoeleweka. Wasanii wengi na watu maarufu wengi hutoka kanda hii. Wengi hutoka TANGA, ARUSHA NA MOSHI. Hivyo ni kusema Kanda hii ni moja ya kanda iliyobarikiwa kupita zote.
Ndio Kanda pekee ambayo watu wake wanapenda kwao na kujivunia kwao. Ni watu ambao hawasiti kujitambulisha popote pale. Mtu hata asipoulizwa hujikuta akisema kuwa kwetu ni Moshi, mara home ARA chuga, ooh kwetu Tanga. Hii huifanya kanda hii kuonekana inaubaguzi na umimi kutokana na hulka ya majigambo.
Matajiri na Wafanya biashara wakubwa. Hakuna ubishi kuwa kanda ya kaskazini inaongoza kwa kuwa na watu wenye mpunga na jala la kufa mtu. Atakayebisha ni yule asiyeijua nchi hii vizuri au ambaye hajatembea mikoa mingi katika nchi hii. Karibu kila kata kwenye majiji makubwa hapa nchi huwezi kukuta matajiri kumi bora wa kata hiyo alafu usikute watano wanatoka kanda ya kaskazini. Si Dar es Salaam, si Mbeya, si Mwanza popote pale lazima matajiri wanne au watano katika kata hizo lazima watoke huko kaskazini. Kanda hii inaheshimu pesa sana. Watu wake hawaoni aibu kufanya hata ni shughuli ya kuuza nyanya bila kujali mtu huyo kaenda shule au hajaenda. Wanachoangalia je kuna mpunga basi.
Majambazi, mafisadi na wahujumu uchumi. Ndio kanda pekee inayoweza kutoa Mafisadi, majambazi na wahujumu uchumi kushinda kanda yoyote hapa nchini. Ujambazi wa kimataifa pia umefanya na watu wa kanda hii. Si ajabu mtu kutoka Arusha akienda Kenya kupiga tukio la kijambazi. Hii imepelekea kanda hii kuogopwa na kutokuaminiwa kabisa na kanda zingine hasa kwenye ishu za pesa. Ndio Kanda pekee ambayo hawataki mchezo na mali zao. Si rahisi umdhulumu mtu kutoka kanda hii. Ukisikia kesi ya kuku ng'ombe anauzwa ili kuendesha kesi basi huko kaskazini ndio mtindo.
Ndio Kanda pekee ambayo hawakatai watoto. Na si rahisi kuchukua damu yao.
Ndio kanda pekee inayojiona Superior kuliko kanda zingine. Mtu kutoka huku hata kama hajaenda shule huwezi kumuendesha na kumdharau eti kisa wewe umeenda shule au unavijipesa.
Ikumbukwe kwamba mtu yeyote anaweza kuwa kanda ya kaskazini iwe kwa damu au kuzaliwa huko.
Nawasilisha!