Hii ndio intelejensi ya kamanda Kova?

Hii ndio intelejensi ya kamanda Kova?

Usoka.one

JF-Expert Member
Joined
Nov 20, 2013
Posts
770
Reaction score
374
Leo nimepita Ubungo mataa nikaona kuna askari wa upepelezi (waliovalia kiraia)wanakamata boda boda na kuwanyanganya funguo kwa ajili ya makosa madogo madogo ambayo ni ya kupewa onyo tu!Lakini wanasumbuliwa hadi utawahurumia.Cha kushangaza ni kwamba kulikuwa na askari waliovaa kiraia kama 30.Hivi kweli hii nguvu inayotumika kwa hawa vijana wanaojitafutia riziki kwa nini isitumike kuzuia uhalifu na hao majambazi wanaoua raia na polisi?au nchi imefilisika hadi tulipwe mishahara kwa faini za boda boda?
 
Msigwa alisema, VIONGOZI TUBADILIKE NAMNA TUNAVYOFIKIRI. Itasaidia sana..... Watu wanafanya kazi bila kuwa na malengo.
 
Tz sio wabunifu tunakusanya billioni 3 kwa mwezi tunatumia bil5 lazima ukimbizane na wamachinga/bodaboda kama alivyosema baba wa taifa.
 
Tatizo ni kuwa wanafanya kazi kwa mazoea zaidi badala ya kubuni mbinu mpya
 
hivi umeuliza kwanza....? au umeamua kusema wale ni makachero?
 
ktk maandamano na panyaroad wanaweza sana...

ktk mauaji ya albino wameishia kukamata waganga wa jadi..

pole tz.
 
Back
Top Bottom