Mambo yote ya Science ni kama theories tuu. Ambazo hizo theory zikifanyiwa majaribio na zikirudisha majibu "sawa" kila zinapojaribiwa, wana-assume ni "Facts ". Hiyo haimaanishi ikiwa ni fact haiwezi kuwa proven wrong.
Scientists hawajawahi kuacha kufanya utafiti ndiyo maana kama unafuatilia sana utaona maelezo yao kama vile yanapingana, unakuta mwanzo walisema hivi, baada ya muda wakasema hivi, na sasa wanasema hivi., ni kwasababu bado wanaendelea na utafiti kugundua uwezekano wa kitu fulani kutokea na sababu zinazopelekea kitu kutokea.
Kuna Case zipo kwenye mitandao ambazo zinafanyiwa research. Na zinaonekana kuna wanawake kweli wanabeba ujauzito wakiwa period au siku moja, mbili , tatu kabla hajaingia period but there's a lesser chance.
Wenye sayansi yao wanasema "For birth control, the only safe assumption is that your partner could get pregnant anytime you have unprotected sex."
Vipindi vingine kwenye mwezi may have a lower probability(uwezekano mdogo) lakini haimaanishi huwa haitokei.
Kwahiyo ukisoma article mbali mbali ukiachana na tulizofundishwa shuleni utagundua "It's possible though uncommon". Kumbuka hata kama chance ni 0.0000001% bado inamaana kubwa sana kwa watafiti. Na those chances depends on a variety of factors. Nimesema tofauti na tulivofundishwa shuleni kwa sababu vitabu vya shuleni havifanyiwi updates mara kwa mara kila baada ya tafiti mpya kukamilika. Elimu ya darasani tuu haitoshi inatubidi kuendelea kutafuta maarifa mapya.
Muda wote ni muhimu kuepuka unprotected sex tofauti na hapo Utashangazwa. Na utafiti mpya utaanzia kwako.
PS, mimi sio scientists, naweza nikawa nimetumia terms ambazo siyo za kitaalamu ila cha msingi ni ujumbe.