Hii mikasa inanipata mimi pekee?

Hii mikasa inanipata mimi pekee?

Saguda47

JF-Expert Member
Joined
May 1, 2016
Posts
11,757
Reaction score
21,986
Ndugu wana jamii forum Nawasalimu kwa jina la Mnyezi Mungu Muumba wetu.

Naleta maada hii kwenu ili kuwaeleza maswahibu yanayoniandama moyoni mwangu ili kama kuna yeyote aliyepitia basi tupeane faraja.

Mimi ni kijana wa kiume ambapo tarehe 30/12 mwaka huu ntatimiza umri wa miaka 26, nikiwa kidato cha sita mwaka 2012 nilipoteza baba na mama walipopata ajali na kufariki, kumbuka Mimi ndio kijana pekee wa kiume na Dada yangu mkubwa tu, nilijikaza kiume ambapo mwaka 2013 februari nlihitimu kidato cha sita, Nilijiunga na mafunzo ya JKT pale Ruvu JKT, bahati nzuri nlikuwa moja ya wanafunzi bora waliofanya vizuri kwenye shabaha na kuahidiwa kuingizwa JWTZ iwapo tungependa.

Nilishauriwa na ndugu na jamaa kuendelea na elimu ya chuo kikuu ili hata kama nataka kujiunga JW niwe na shahada tayari, nliamua kusoma degree ambapo 2016 julai nlihitimu elimu ya chuo kikuu, nlipata shule ya kufundisha ya private,

Miezi michache baadae nlikutana na kaka yangu wa ukoo ambaye ni moja ya viongozi wakubwa katika awamu hii ( sitaji jina) aliniomba niache kufundisha ili nikasimamie mradi wake huku akiahidi kunilipa mshahara kila mwezi. nilikubaliana nae....nlianza kazi vizuri katika huo mradi miezi kadhaa ikapita hata kupewa mshahara wangu kitu kilichopelekea Mimi kuanza kuuza mpunga nlionunua huko morogoro kwa mama mdogo ili nijikimu kimatunizi na mambo mengine.

Baada ya mda Mimi na Dada yangu tuliamua kugawana pesa ambayo iliachwa na wazazi wetu, nlipata kama milioni tatu hivi ( 3,000,000/=). Nlinunua kiwanja na kufungua biashara ya Grocery ambayo ilikuwa ikinilipa vizuri tu, mda huo nliendelea kufanya kazi kwenye kampuni ya huyu kaka angu japo nlizidi kuwa na malimbikizo ya mshahara wangu maana sikuwa nikilipwa kila mwezi.

Sikujali hilo na nikapata Dada mmoja ambaye baadae nikaamua kumuoa japo bado hatujafunga ndoa rasmi lakini nlishajitambulisha kwa wazazi na nduguze mambo yakawa sawa,

Zengwe limekuja hivi karibuni ambapo biashara ya hiyo grocery ilianza kudorola na kujikuta mambo yangu hayapo sawa kabisa,
Pia nimeundiwa zengwe la kuwa Nina loss kwenye biashara ya jamaa ambapo malimbikizo yangu tangu nianze kufanya kazi yanafikia milioni tatu hivi!!! niliamua kuchukua mkopo ili nifufue grocery yangu ambayo ndio inanipa ridhiki ya kila siku,

Ninaumia sana jamani hasa nikikumbuka kuwa nilipata ajira ya kufundish nikaiacha kwa kulaghaiwa na mtu mkubwa wa karibu ninayemuamini sana.

Mpaka inafika mda nawaza bora nisingeoa huyu binti wa watu ili nisimuweke kwenye hali ngumu kama hii maana naelekea kudhulumiwa haki yangu huku hali yangu mbaya kiuchumi,
imefikia hatua nataka niuze pikipiki yangu ili nijaribu bahati zingine. maana sina namna sasa.

Naombeni ushauri nifanyeje ili nipate haki yangu toka kwa huyu (kigogo) kaka yangu.
NB: naomba ushauri jamani na uzoefu wenu.
 
Kwa awamu hii undugu weka pembeni,mwambie akulipe mishahara yako anadhani utaishije?yeye ni kigogo wewe unaisoma namba!kweli?kama mbwai mbwai tu ashakulostisha kazini kwako kumbuka
 
Huyo jamaa anaroho ya kutu aseeeh.. yeye inaonekana ni wa kutumia watu tu hasa ndugu zake kwa faida yake na hili ungelielewa mapema kabla ya kurudi mara ya pili.


Naamini hakuna njia moja ya kutatua tatizo moja. Ingekuwa mimi ningemfanyia haya.

1. Kulipeleka kwa wazee wa ukoo wanaoheshimiwa na ndugu zenu mlizungumze kwa undani. Ikishindikana...

2. Kwenda kwenye vyombo vya sheria hasa kwa kuanzia kwa serikali za mitaa ikiwezekana ni kiongozi basi ataona aibu yakishindikana fungua kesi.

3. Kama nipo position ambayo nashika pesa za kampuni ningejilipa tena zaidi ya ninachomdai ili aonje niliyoonja.

Mimi kwenye ishu za kumdai mtu natumia ubabe..kama nakudai nakuja kwako nakujabmisha nakupa siku 2 kwa hili nimefanikiwa kwa aslimia nyingi.
 
kwanini usitafute kazi nyingine ?
Una mkataba wa kufanya kazi hapo miaka yote ?
Umejaribu kutafuta nafasi jeshini ukakosa ?
 
Kwa awamu hii undugu weka pembeni,mwambie akulipe mishahara yako anadhani utaishije?yeye ni kigogo wewe unaisoma namba!kweli?kama mbwai mbwai tu ashakulostisha kazini kwako kumbuka
Broo kuna watu wenye roho mbaya sana Ila ukimuona akijinasibu ITV you can't believe if he would be a such devil!!
 
Makubaliano yenu toka mwanzo yalikuwaje? na kwa nini muda wote ulikuwa hudai mshahara? nataka nisikie na upande wa pili.
 
Huyo jamaa anaroho ya kutu aseeeh.. yeye inaonekana ni wa kutumia watu tu hasa ndugu zake kwa faida yake na hili ungelielewa mapema kabla ya kurudi mara ya pili.


Naamini hakuna njia moja ya kutatua tatizo moja. Ingekuwa mimi ningemfanyia haya.

1. Kulipeleka kwa wazee wa ukoo wanaoheshimiwa na ndugu zenu mlizungumze kwa undani. Ikishindikana...

2. Kwenda kwenye vyombo vya sheria hasa kwa kuanzia kwa serikali za mitaa ikiwezekana ni kiongozi basi ataona aibu yakishindikana fungua kesi.

3. Kama nipo position ambayo nashika pesa za kampuni ningejilipa tena zaidi ya ninachomdai ili aonje niliyoonja.

Mimi kwenye ishu za kumdai mtu natumia ubabe..kama nakudai nakuja kwako nakujabmisha nakupa siku 2 kwa hili nimefanikiwa kwa aslimia nyingi.
yaani mkuu nikikumbuka nlivojitesa kusimamia, inafika kipindi nalala na ghetoni kwangu na kama milioni 40,000,000/= ikiwa siku siyo ya kuweka hela benki mfano jpli
 
yaani mkuu nikikumbuka nlivojitesa kusimamia, inafika kipindi nalala na ghetoni kwangu na kama milioni 40,000,000/= ikiwa siku siyo ya kuweka hela benki mfano jpli
Kama kuna uwezekano wa kushika pesa yake tena... unachukua hata hiyo 40m unakaa nazo.

Kama hamna basi njia zingine zinakuhusu.
 
Dah kaka una washaur wabaya ever... katika historia yako pale tu ulipopata nafasi ya kubaki na kupata nafas ya kuingia jw a watu wakakwambia uendelee na uchuo ni uchawi tosha... by the way.. pole bro.. matatizo ni ya kwetu.. hapo amna namna ni kumfungulia Madai tu na ikiwezekana na tort juu
 
Makubaliano yenu toka mwanzo yalikuwaje? na kwa nini muda wote ulikuwa hudai mshahara? nataka nisikie na upande wa pili.
makubaliano ni mimi kufanya kazi na yeye kunilipa mshahara, lakini nlipoona analimbikiza miezi nilimuuliza akasema hamna shida atanilipa hela yote bila shida, nlimuamini kwa kuwa ni mtu na heshima zake za juu tu, lakini saivi kanichenjia
 
Kama kuna uwezekano wa kushika pesa yake tena... unachukua hata hiyo 40m unakaa nazo.

Kama hamna basi njia zingine zinakuhusu.
Nikikumbuka naumia sana!! but one day yes ntatoboa tu.
 
Back
Top Bottom