vukani
JF-Expert Member
- Dec 30, 2009
- 245
- 165
Niliwahi kumtembelea rafiki yangu mmoja aliyekuwa akiishi na wazazi wake maeneo ya Tandale Uzuri,
Nakumbuka ilikuwa ni majira ya asubuhi hivi, basi nilipokaribia nyumbani kwao, nikakuta kiwingu cha watu halafu kulikuwa na wanawake wawili wadada hivi walikuwa wakizodoana na kutukanana hadharani, na mimi nikaona nisipitwe na udaku wa kitaani, nikajisogeza ili kujua kulikoni.
Walikuwa wakitukanana matusi ya mwilini yasiyofaa kuweka humu, si unajua vituko vya uswahilini?
Basi mara akaja baba mmoja ambaye nilikuja kujua baadae kuwa alikuwa ni mjumbe wa shina katika eneo lile,
Baada ya kuwatuliza ili wapunguze munkari wote walitulia ndipo, yule mama ambaye alionekana kuchonga sana alipoanza kujieleza kwa mjumbe.
Kumbe kisa cha kutukanana kiasi kile ni mavi ya mtoto, mnashangaa nini? Ndio walikuwa wakigombea mavi!
Ilikuwaje, subiri basi niwasimulie, mbona mna haraka nyie?
Haya sikiliza kwa makini.
Ilikuwa ni hivi, huyo dada wa nyumba ya jirani alikuwa akikatiza kwa huyo jirani yake, akamkuta mtoto wa jirani yake amejisaidia haja kubwa uchochoroni, basi kwa uungwana wake akazoa yale mavi na kuyatumbukiza ******, kisha akamshika yule mtoto mkono hadi kwa mama yake na kumjulisha kwamba mwanae amejisaidia haja kubwa hivyo amnawishe, hapo ndipo lilipozuka balaa, yule mama alitaka aoneshwe yalipo mavi ya mwanae, yule jirani yake akamwambia kuwa ameshayatupa ******,
He! kusikia hivyo mama wa kizaramo akaja juu anadai mavi ya mwanae na kumtuhumu jirani yake kuwa ni mchawi na amechukuwa mavi yam mwanae ili akamloge afe kama alivyo wauwa wanaae wawili.
Kumbe yule mama aliwahi kupoteza wanae wawili waliofariki kabla ya kufikisha umri wa miaka mitano, hivyo alipoenda kwa mganga akaambiwa kuwa kuna jirani yake ndiye anaemuulia watoto wake.
Bada ya kumegewa mkasa huo na wakuda nikajimuvuzisha kwa rafiki yangu nikawaacha wakiendelea kusuluhishwa na mjumbe wao.
Yaliyojiri huko nyuma yangu siyajui kwa hiyo usiniulize.
Nakumbuka ilikuwa ni majira ya asubuhi hivi, basi nilipokaribia nyumbani kwao, nikakuta kiwingu cha watu halafu kulikuwa na wanawake wawili wadada hivi walikuwa wakizodoana na kutukanana hadharani, na mimi nikaona nisipitwe na udaku wa kitaani, nikajisogeza ili kujua kulikoni.
Walikuwa wakitukanana matusi ya mwilini yasiyofaa kuweka humu, si unajua vituko vya uswahilini?
Basi mara akaja baba mmoja ambaye nilikuja kujua baadae kuwa alikuwa ni mjumbe wa shina katika eneo lile,
Baada ya kuwatuliza ili wapunguze munkari wote walitulia ndipo, yule mama ambaye alionekana kuchonga sana alipoanza kujieleza kwa mjumbe.
Kumbe kisa cha kutukanana kiasi kile ni mavi ya mtoto, mnashangaa nini? Ndio walikuwa wakigombea mavi!
Ilikuwaje, subiri basi niwasimulie, mbona mna haraka nyie?
Haya sikiliza kwa makini.
Ilikuwa ni hivi, huyo dada wa nyumba ya jirani alikuwa akikatiza kwa huyo jirani yake, akamkuta mtoto wa jirani yake amejisaidia haja kubwa uchochoroni, basi kwa uungwana wake akazoa yale mavi na kuyatumbukiza ******, kisha akamshika yule mtoto mkono hadi kwa mama yake na kumjulisha kwamba mwanae amejisaidia haja kubwa hivyo amnawishe, hapo ndipo lilipozuka balaa, yule mama alitaka aoneshwe yalipo mavi ya mwanae, yule jirani yake akamwambia kuwa ameshayatupa ******,
He! kusikia hivyo mama wa kizaramo akaja juu anadai mavi ya mwanae na kumtuhumu jirani yake kuwa ni mchawi na amechukuwa mavi yam mwanae ili akamloge afe kama alivyo wauwa wanaae wawili.
Kumbe yule mama aliwahi kupoteza wanae wawili waliofariki kabla ya kufikisha umri wa miaka mitano, hivyo alipoenda kwa mganga akaambiwa kuwa kuna jirani yake ndiye anaemuulia watoto wake.
Bada ya kumegewa mkasa huo na wakuda nikajimuvuzisha kwa rafiki yangu nikawaacha wakiendelea kusuluhishwa na mjumbe wao.
Yaliyojiri huko nyuma yangu siyajui kwa hiyo usiniulize.