Hii imekaaje wakuu?

Hii imekaaje wakuu?

Miss Kim

Senior Member
Joined
May 3, 2014
Posts
164
Reaction score
273
Kwanza nitangulize salamu wakuu. Natumai wote wazima wa afya. Ni hivi,kuna huyu kijana ambaye ni workmate na tumeshafahamiana kwa miaka 4 sasa. Kwa mda sasa kulikuwa na minong'ono ofisini kuhusu mahusiano yake ya siri na rafiki yangu wa kike ambaye kwa kipindi chote hicho alikua ametengana na mume wake. Ukweli ni kwamba hakuna mtu ambaye alikua na uhakika kuhusu mahusiano yao ila kulikuwepo na viashiria kwamba mahusiano yao yalikua zaidi ya "just casual friends".

Sasa huyu rafiki yangu mume wake amemrudia na kuomba radhi na tayari mipango ya ndoa imeshaanza. Harusi yao ni mwishoni mwa mwaka huu na vikao vimeshaanza. Sasa hapa ndo tatizo langu linapokuja. Yule kijana ambaye alikua anahisiwa kutoka na rafiki yangu alinifuata na kuniambia ukweli,kwamba ni kweli walikua na hasiano ya kimapenzi ila kwa siri kubwa sana kwasababu mume wake na rafiki yangu ni mtu mwenye hela sana na angefanikiwa kutambua chochote kuhusu mahusiano yao angeweza hata mtenda vibaya yule kijana. Ila sasa kwa kuwa rafiki yangu anaolewa anaona hana budi kutafuta mwanamke mwingine kwasababu na yeye mipango yake ni kuoa na kuanzisha familia yake by next year.

Mm nikamuuliza swali rahisi sana,kwanini mimi? Akasema kwasababu nakufahamu na ni mwanamke ambaye ningependa awe mke wangu. Nikamuuliza,je kuhusu mahusiano yako ya siri ya rafiki yangu? Akasema hiyo itabaki kuwa siri kati yetu wawili (yy na rafiki yangu). Ila kusema kweli wakuu mm binafsi nahisi hii haijakaa vizuri kwa sababu tayari nimeshafahamu kwamba jamaa alikua anatoka kimapenzi na rafiki yangu tenda kama ndugu yangu halafu leo hii mm nije kutoka naye? Yeye anasema haina shida kwa sababu hakuna aliyekua anajua kuhusu mahusiano yao,ila je rafiki yangu atanichukuliaje? Na pia najiuliza inamaana huyu kijana kaniona mm ndo "rebound love" yake?

Msaada kwenye tuta wakuu. Asanteni kwa mawazo na ushauri wenu.
 
Kidogo sijakuelwa unasema rafiki yako alitengana na mume wake, sasa mume kaomba msamaha alafu wanatarajia kufunga ndoa, sasa anakuwa mume mara ngapi? au ulimaanisha walikuwa wachumba? na kuhusu wewe hapo kwa kweli hapana loh unless u r so desperate kuolewa
 
Jibu rahisi ni hili, OLEWA tu.
Moyo wenye shabaha haupindishwi kwa tege la mkono.
 
Ww kama unataka ndoa na unampenda jamaa olewa tu
 
Kwanza nitangulize salamu wakuu. Natumai wote wazima wa afya. Ni hivi,kuna huyu kijana ambaye ni workmate na tumeshafahamiana kwa miaka 4 sasa. Kwa mda sasa kulikuwa na minong'ono ofisini kuhusu mahusiano yake ya siri na rafiki yangu wa kike ambaye kwa kipindi chote hicho alikua ametengana na mume wake. Ukweli ni kwamba hakuna mtu ambaye alikua na uhakika kuhusu mahusiano yao ila kulikuwepo na viashiria kwamba mahusiano yao yalikua zaidi ya "just casual friends".

Sasa huyu rafiki yangu mume wake amemrudia na kuomba radhi na tayari mipango ya ndoa imeshaanza. Harusi yao ni mwishoni mwa mwaka huu na vikao vimeshaanza. Sasa hapa ndo tatizo langu linapokuja. Yule kijana ambaye alikua anahisiwa kutoka na rafiki yangu alinifuata na kuniambia ukweli,kwamba ni kweli walikua na hasiano ya kimapenzi ila kwa siri kubwa sana kwasababu mume wake na rafiki yangu ni mtu mwenye hela sana na angefanikiwa kutambua chochote kuhusu mahusiano yao angeweza hata mtenda vibaya yule kijana. Ila sasa kwa kuwa rafiki yangu anaolewa anaona hana budi kutafuta mwanamke mwingine kwasababu na yeye mipango yake ni kuoa na kuanzisha familia yake by next year.

Mm nikamuuliza swali rahisi sana,kwanini mimi? Akasema kwasababu nakufahamu na ni mwanamke ambaye ningependa awe mke wangu. Nikamuuliza,je kuhusu mahusiano yako ya siri ya rafiki yangu? Akasema hiyo itabaki kuwa siri kati yetu wawili (yy na rafiki yangu). Ila kusema kweli wakuu mm binafsi nahisi hii haijakaa vizuri kwa sababu tayari nimeshafahamu kwamba jamaa alikua anatoka kimapenzi na rafiki yangu tenda kama ndugu yangu halafu leo hii mm nije kutoka naye? Yeye anasema haina shida kwa sababu hakuna aliyekua anajua kuhusu mahusiano yao,ila je rafiki yangu atanichukuliaje? Na pia najiuliza inamaana huyu kijana kaniona mm ndo "rebound love" yake?

Msaada kwenye tuta wakuu. Asanteni kwa mawazo na ushauri wenu.

Rafiki yako alikuwa na mume halafu wakaachana. Wanarudiana tena halafu hapo hapo wanafunga ndoa tena. Je, ndoa inafungwa mara mbili na watu walewale?

Any way turudi kwenye mada. Suala la kuoa au kuolewa ni suala nyeti ambalo baadhi ya watu kwa kulichukulia kirahisi rahisi wamejikuta wakiingia katika majuto baadaye baada ya kuwa tayari wameshafunga ndoa. Huyo kijana wewe ndiye unamfahamu vizuri. Mnafanya kazi ofisi moja. Achana na mambo ya historia kuhusu uhusiano wake na huyo rafiki yako kwa sasababu hata wewe si ajabu ulikuwa au una mpenzi mpaka sasa. Huyo rafiki yako tayari kapatana na mume wake na wewe angalia maisha yako. La msingi ni kuanagalia dhamira ya huyo kijana ya kuomba kuanzisha uhusiano na wewe kama ni ya ndoa kweli au ni zinaa tu. Na wewe je, una malengo gani kuhusu maisha yako ya mahusiano ya kimapenzi; kuolewa au vinginevyo? Je, unampenda huyo kijana? Ukipata majibu ya maswali hayo nafikiri itakuwa rahisi kwako kuchukua uamuzi sahihi kuhusu suala hilo.


 
Kabla hujafuata moyo wako (maana it seems unampenda ingekua otherwise ungeshamalizana naye huko huko kwa kumkatalia) kumbuka tu kuna ule msemo 'uhawara haufi', hii inaweza kukusumbua mbeleni maana ukimuona tu rafiki yako ananong'ona na husbie wako unaweza dhani wanataka kupasha kiporo kama waliweza fanya sirini then why not now?
All in all, mshirikishe sana Mungu, wish you luck.
 
Majibu yote unayo ajabu Unataka tukushauri....au tukushauri ukubali?
 

Rafiki yako alikuwa na mume halafu wakaachana. Wanarudiana tena halafu hapo hapo wanafunga ndoa tena. Je, ndoa inafungwa mara mbili na watu walewale?

Any way turudi kwenye mada. Suala la kuoa au kuolewa ni suala nyeti ambalo baadhi ya watu kwa kulichukulia kirahisi rahisi wamejikuta wakiingia katika majuto baadaye baada ya kuwa tayari wameshafunga ndoa. Huyo kijana wewe ndiye unamfahamu vizuri. Mnafanya kazi ofisi moja. Achana na mambo ya historia kuhusu uhusiano wake na huyo rafiki yako kwa sasababu hata wewe si ajabu ulikuwa au una mpenzi mpaka sasa. Huyo rafiki yako tayari kapatana na mume wake na wewe angalia maisha yako. La msingi ni kuanagalia dhamira ya huyo kijana ya kuomba kuanzisha uhusiano na wewe kama ni ya ndoa kweli au ni zinaa tu. Na wewe je, una malengo gani kuhusu maisha yako ya mahusiano ya kimapenzi; kuolewa au vinginevyo? Je, unampenda huyo kijana? Ukipata majibu ya maswali hayo nafikiri itakuwa rahisi kwako kuchukua uamuzi sahihi kuhusu suala hilo.



Nashukuru sana Q Man kwa majibu yako yenye mantiki, thank you. Kwanza ni fafanue kwann nilisema "mume wake". Walikua wameshafunga ndoa ya kimila na alikua keshapeleka "kishika uchumba" kabla hawajatengana, so huyo alikua bado ni mume wake. Sasa wanataka kufunga ndoa ya kanisani na kuweka mambo sawa.

Ushauri wako nitaufanyia kazi. Umeniuliza maswali ya msingi sana,asante kaka.
 
Wewe unampenda huyo kijana?Na vipi hauna mpenzi?Hebu tuanzie hapo kwanza

Nashukuru Honey Faith. I am currently single ila nikisema nampenda huyo kijana nitakua nadanganya. Ila naamini kwamba it's a matter of time before i let my heart fall for him but i wouldn't wish to let myself fall for the wrong person. Ndo maana nikaja omba ushauri kabla ya kufanya maamuzi yeyote.
 
Kidogo sijakuelwa unasema rafiki yako alitengana na mume wake, sasa mume kaomba msamaha alafu wanatarajia kufunga ndoa, sasa anakuwa mume mara ngapi? au ulimaanisha walikuwa wachumba? na kuhusu wewe hapo kwa kweli hapana loh unless u r so desperate kuolewa

Asante Mrs.Leo. Hilo jibu kuhusu mume nilishajibu kwenye post ya Q Man,kindly refer. Hapana,i am not desperate to get married, i have never been. Ila nimeomba tu ushauri nisije jiingiza kwenye jambo ambalo nitakuja jutia.
 
unampenda huyu kijana

Hapana,bado ni mapema sana kusema kwamba nampenda. I like him just as a friend ila in a different situation i wouldn't mind dating him,tatizo langu alishatoka na rafiki yangu kipenzi tena kwa siri kubwa and he confessed this to me. That's where the dilemma comes in.
 
Wewe kakuambia siri itabaki kuwa ya wao wawili halafu wewe umekuja kuutangazia ulimwengu!!? Hakuna tena siri hapo kila mtu atajua unakula kiporo......
 
Majibu yote unayo ajabu Unataka tukushauri....au tukushauri ukubali?

Asante,you don't have to be so negative man. Ningekua na majibu yote nisingeomba ushauri,ila asante kwa kutia mkono humu.
 
Wewe kakuambia siri itabaki kuwa ya wao wawili halafu wewe umekuja kuutangazia ulimwengu!!? Hakuna tena siri hapo kila mtu atajua unakula kiporo......

Wrong perception. Hunifahamu mm wala wahusika niliowazungumzia humu. So bado ni siri na itabaki kuwa siri.
 
Ni hivi unampenda huyo kaka?
Napia sikiliza moyo wako,kumbuka yaliyo kwisha fanyika yashafanyika cha msingi shukuru mungu pia amekuambia ukweli so fata moyo wako kuwa watakaje.
 
Back
Top Bottom