Hii imekaaje wakuu?

Hii imekaaje wakuu?

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
38,072
Reaction score
57,726
Kuna hii hali ya ndugu na marafiki wanakuja kwako kukuomba hela, ila kwa kuona ili asiendelee kuwa ombaomba pamoja na kuwa na maisha magumu, unaamua kumpa kazi kwenye biashara zako au kampuni.

Matokeo yake anakataa kazi na kulalamika ya kuwa, umeshindwa kumsaidia.

Hii imekaaje wakuu?, Na wahenga wanasema, ‘Mtu akikuomba samaki usimpe samaki bali mfundishe namna ya kuvua samaki.”​
 
Tajiri hiyi ya kuwaingiza ndugu kazini, inapaswa uifanye kwa umakini sana.
Mimi nimelizwa na kufanyia "sabotage" sana kwenye biashara zangu na ndugu, niliowaaminii. Unamuweka ndugu kumsaidia yeye anawaza kukupiga.
 
Hawa wenzetu asili ya Asia, wanafanikiwaje?

Wale wana "succession plan" na "wealth lineage" nzuri. Mtu anazaliwa anafundisha na kuiishi biashara. Sisi hapa ndugu ukitoboa ndio wanakuja, kwa kaka, kwa mjomba, kwa shemeji n.k.
Wenzetu biashara kwao ni tabia, wamezijenga, zimewajenga. Fikiria mtu anakuja kwako kwa wazo la kujiegesha wakati anasubiria kazi za serikali ambazo waga hapati! 😊
Mindset mtu wangu!
 
Wale wana "succession plan" na "wealth lineage" nzuri. Mtu anazaliwa anafundisha na kuiishi biashara. Sisi hapa ndugu ukitoboa ndio wanakuja, kwa kaka, kwa mjomba, kwa shemeji n.k.
Wenzetu biashara kwao ni tabia, wamezijenga, zimewajenga. Fikiria mtu anakuja kwako kwa wazo la kujiegesha wakati anasubiria kazi za serikali ambazo waga hapati! 😊
Mindset mtu wangu!
Uko sahihi, kwa mazigira ya sasa, una pambana nao vipi?
 
Uko sahihi, kwa mazigira ya sasa, una pambana nao vipi?

Toka mwaka juzi mimi, niliweka nadhiri ya kutomhusisha ndugu kwenye biashara zangu! Kama ikitokea basi sio kwenye nafasi za maamuzi "decision making".... fedha na mipango. Kuna ndugu mmoja wa kuja, juzi kati tuu hapa akauza mpango kwa mshindani "competitor" ... iliniathiri sio kidogo.
Emagine! Mtu ni in charge wa biashara, anafanya partnership/sidelining ya siri na competitor. Manipulation was well orchestrated, nilipochukua hatua ya kumpiga chini, akaenda upande wa adui... disrespect was unbelievable....!!
Usiniulize nilifanikiwa vipi kurudi njiani tena na biashara ile,,, itakusisimua....
 
Kuna siri moja nimejifunza USA .Matajiri wanaishi porini sio changa nyikeni.Na uwezi kuwapata kirahisi wala kuwaona
 
Back
Top Bottom