Hii imekaaje kisheria wanafunzi kutozwa faini mashuleni

Kwanza naomba nikusahihishe, kwa mujibu wa maelezo yako, aliyetozwa hiyo faini ni mzazi na sio mwanafunzi . Ndio maana huyo mwanafunzi alirudishwa nyumbani ili kumwita mzazi wake.

Pili hapa JF hutapata jibu la uhakika, maana hiyo tozo inaaply kwenye hiyo kata uliyotaja, na sijaona mtu ana mwenye kuielewa vyema hapa zaidi ya wachangiaji wengi kuonyesha emotions zao binafsi kwa uzoefu wa maeneo mengine.

Mimi naungana na wanaohisi kuwa hiyo faini kwa mzazi imewekwa na baraza la maendeleo la kata hiyo (WDC) ambao kimsingi ndo wasimamizi wa shule hiyo. Na katika utungaji wa bylaw kama hizi, jamii (wananchi) ndo wahusika wakuu kwa maana wao ndio wanakubali au kukataa utaratibu huo kutumika. Kitendo cha kuambiwa kuwa kuna pesa taslim ambayo inabidi ipelekwe kwenye serikali ya mtaa kinaendelea kunipa imani kwamba hilo ni suala lililokubaliwa na jamii husika na utakuta hiyo pesa huko kwenye serikali ya mtaa ina maelekezo kabisa kuwa inaenda kufanya nini.

Na pengine kwa nini shuleni wanataka kupeleka ream ni kwa sababu ya maelekezo ya serikali ya kuzuia walim kukusanya michango (cash) kutoka kwenye jamii bila kuwa na kibali maalum.

Sent from my SM-T285 using JamiiForums mobile app
 
Una uhakika hiyo tozo inatumika kama kipato kwa wanaoikusanya? Unadhani kama hiyo tozo ipo, kwa level ya shule hiyo, hiyo tozo imewekwa na nani?
Unaita WIZI kua ni Adhabu, are you for real?
Kwani kama mtu unaona eneo lako la kazi halikupi kipato unachokihitaji kwanini usiachane napo ukaangaza mbele kuliko kuumiza wengine?

Sent from my SM-T285 using JamiiForums mobile app
 
Una uhakika hiyo tozo inatumika kama kipato kwa wanaoikusanya? Unadhani kama hiyo tozo ipo, kwa level ya shule hiyo, hiyo tozo imewekwa na nani?

Sent from my SM-T285 using JamiiForums mobile app
Unaniuliza mimi hayo maswali? Unanionea sijui chochote ila ninachojua sijawahi kusikia mzazi anatozwa faini sababu hakuripoti kutokuhudhuria kwa mtoto shule.

Sheria iwekwe na nani au nani hizo ni sheria kandamizi lakini pia ni wizi kama wizi mwingine.
 
Is this for real? Kwamba hakutoa taarifa eti kwa sababu hana namba za simu za walim, na umbali uliopo kati ya shule na makazi yake!!!! This is absurd. Ridiculous.

Kwanza kwenye taasisi yoyote taarifa ya simu sio official. Hata kama angekuwa na namba huwez kupiga simu na kurelax for all those days. Simu inatoa preliminary information ambapo inabidi u confirm in person baada ya hapo.

Halafu eti mzazi kashindwa kwenda kwa sababu kuna mbali mrefu, wakati huo huo mtoto wake anatakiwa atembee kila siku to and fro the school. Hii ni total lack of seriousness na ndo maana labda hata huo utaratibu ukawekwa kuondoa uzembe wa kipuuzi kama huu.
Kwa maelezo yake Taarifa hakutoa, hii ni kutokana na kutokua na mawasiliano na uongozi wa shule yaan nambari zao za simu, na umbali kati ya shuleni hapo na nyumbani kwa mwanafunzi huyo . Lakini kama haitoshi mtoto amekuja na vielelezo vya nyaraka mbalimbali za manunuzi ya dawa na ushahidi wa jeraha physically.. Yani jeraha bichi lipo linaonekana pasipo kuwa na shaka yoyote

Sent from my SM-T285 using JamiiForums mobile app
 
Shule ya kata ni community school, na kama community ya hilo eneo imeona moja ya njia ya kuzuia utoro ni kutoza wazi faini, hiyo ni juu yao.

Hujawahi kusikia kwa sababu hiyo sio sheria ya nchi kuwa ipo kila mahala. Kuna mambo yapo mtaani kwangu yanafanyika kisheria ambayo mtaani kwako hayapo and vice versa.

Kikubwa hapa ni validity ya hiyo sheria ndogo, kama kweli ipo basi watu wa hilo eneo wamekubaliana na inatumika.

Hapo ulipo na hapa nilipo haipo maana hatujakubaliana hivyo.
Unaniuliza mimi hayo maswali? Unanionea sijui chochote ila ninachojua sijawahi kusikia mzazi anatozwa faini sababu hakuripoti kutokuhudhuria kwa mtoto shule....
Sheria iwekwe na nani au nani hizo ni sheria kandamizi lakini pia ni wizi kama wizi mwingine.

Sent from my SM-T285 using JamiiForums mobile app
 
Hata mimi nahisi hivyo, shida ni kwamba wananchi wengi huwa hatuhudhurii kwenye mikutano ya mitaa au ya wazazi shuleni. Ndo hapo tunashindwa kupata taarifa rasmi.

Sasa mzazi kama huyo ambaye anashindwa kwenda shule kutoa taarifa ya ugonjwa wa mwanae kwa kigezo cha umbali, unadhani atakuwa na muda wa kwenda kwenye mikutano ya mtaa?
Inawezekana ni sheria ndogo (bylaws)zilizowekwa na serikali za mtaa(kata) ili kudhibiti utoro.Kama ni hivyo je wazazi mlishirikishwa/kufahamishwa juu ya sheria/taratibu hizo?

Sent from my SM-T285 using JamiiForums mobile app
 
Kutokuwa na hela na kutolipa hela ni vitu viwili tofauti. Anaweza asiwe nayo mda huo, akaipata bdae akalipa na mambo yakaisha.

Kwani umefuatilia ukaambiwa kama mzazi hajatoa hiyo faini mwanafunzi haruhusiwi kwenda shule?
Kwaiyo wazazi wasipo kuwa na hiyo pesa watoto wao waache shule..? hiyo bylaws ni ya kikoloni na kandamizi kabisa.. serikali za mitaa hawawezi kukaa na kutunga sheria inayo kinzana na katiba ya nchi.. Any law against national constitution is invalid.

Sent from my SM-T285 using JamiiForums mobile app
 
Nijuavyo Mimi hayo sio maamuzi ya walimu au shule husika Bali ni maamuzi ya wazazi na walimu ambayo yalifikiwa kwenye kikao halali ,wewe mtoa mada na mzazi wa mtoto yaonekana hukuhudhuria au si mhudhuriaji wa vikao vya shule,na ndio màana hata mwanao alipopata jeraha hukuweza kupeleka taarifa kwa walimu ili wapate taarifa za kuugua kwa mwanao.

Hivyo tambua kuwa hilo lililokukuta ni moja ya maamuzi yaliyofikiwa na wazazi pamoja na walimu na kuandaliwa kwa mhitasari wake ambao inaonesha uhalali wa maamuzi hayo ili kudhibiti utoro na nidhamu kwa watoto wetu.

Mwisho nenda shuleni ukaombe mwongozo na kama hakuna mhitasari wowote unaoonesha maridhiano ya adhabu kama hiyo basi ni batili na sioni uhalali wa wewe kama mzazi au mlezi kulipa adhabu hiyo.
 
Mkuu Mara nyingi mambo kama hayo huwa yameamuliwa na wazazi ktk vikao na bodi ya shule.
Ungeuliza hizo faini na adhabu zimewekwa na nani ungepata muelekeo.

Lakini nafikir ni busara na utaratibu kwa mzazi kuwasiliana na shule pale mtoto wake anapokuwa na udhuru wowote ule.Laiti Kama mngekuwa mmefanya hivyo haya yote yasingetokea
 
Mkuu Mara nyingi mambo kama hayo huwa yameamuliwa na wazazi ktk vikao na bodi ya shule.
Ungeuliza hizo faini na adhabu zimewekwa na nani ungepata muelekeo.

Lakini nafikir ni busara na utaratibu kwa mzazi kuwasiliana na shule pale mtoto wake anapokuwa na udhuru wowote ule.Laiti Kama mngekuwa mmefanya hivyo haya yote yasingetokea
Fact
 
Heshima kwenu wakuu.

Ipo hivi nina jirani yangu mwanae anasoma shule fulani hapa jijini Dar es Salaam pale eneo la Temboni-Ubungo. Ni shule ya sekondari ipo chini ya umiliki wa serikali. Wiki iliyo pita tangia tarehe 3/07/2020 mwanae (wakike) alipata ajili ya kuchubuliwa(kukatwa) na kipande cha chupa kwenye mguu wake wa kushoto na kumsababishia maumivu makali na uvimbe...
Taja jina la shule, huo ni wizi wa mchana kweupee.
 
Inawezekana ni sheria ndogo (bylaws) zilizowekwa na serikali za mtaa(kata) ili kudhibiti utoro.Kama ni hivyo je wazazi mlishirikishwa/kufahamishwa juu ya sheria/taratibu hizo?
By-laws nyingi ni magumashi, kila siku tunafanya kazi ya kuzihakiki na KUZIFUTA.

Nyingi zimetungwa kienyeji enyeji tu bila kufuata sheria kuu.

Kamtu kakiamka tu kanajitungia sheria zake uchwara.

Fuatilia hilo. Hakuna adhabu ya aina hiyo!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nina uhakika mleta mada kwa namna yoyote hao wazazi watajikuta ndo wenye makosa wala usihangaike sana huku JF, hakuna mwalimu yeyote Tanzania anaweza kujiwekea sheria za namna hiyo haswa enzi za sasa hivi, sheria hizo zitakuwa na baraka za wananchi wenyeji wa shule hiyo ikiwemo ngazi ya serikali za mitaa hiyo.

Pia hizo sheria unakuta wazazi/walezi na wadau wa elimu waliziweka wao ili pengine kudhibiti utoro uliokuwa umekithiri katika shule hiyo. Yawezekana pia mzazi/mlezi wa huyo mtoto hana ushirikiano wowote na shule kwani hajui kinachoendelea.

Kwa mfano kwenye shule nyingi kudhibiti mienendo kama hiyo huwa zinawekwa adhabu ambazo hutengenezwa jamii husika kama mtoto kuleta tofali mbili au idadi kadhaa, kuleta mawe, kuleta miti ya kupanda nk.

Haya si mageni katika uga wa elimu zetu labda kama hujui. Aidha nahisi nyie walez na wazazi wa mwanafunzi huyo mmekosea, mnakaa na mwanafunzi siku8 bila kutoa taarifa shuleni alafu unalalamika kupewa adhabu.
 
Walimu wanakuwaga na mambo ya ajabu sana wakati mwingine, nakumbuka mwaka 2017 kijana wangu alikuwa anasoma shule moja ya serikali boarding ( Shule kongwe maarufu kama shule za vipaji) Akiwa shule mtoto aliugua akiwa analalamika maumivu ya kichwa ambayo yalichukuwa takribani wiki nzima, baada ya wiki moja mtoto hali ilikuwa mbaya sana akiwa zahanati ya shule ambayo inatumia pia na chuo kikuu chenye jina sawa na hiyo shule aliomba simu kwa msamaria mwema na akampigia mamake. Akimweleza anaumwa na hali yake ni mbaya, nilivorudi toka kwenye mihangaiko yangu wife akanieleza mkasa mzima.

Asubuhi na mapema nikawahi stendi kutafuta usafiri bahati nzuri nikapata gari moja ya binafsi nikaondoka kuelekea shule. Nilivofika shule kabla ya kuonana na kijana nilitafuta walimu kama watatu ambao nilikuwa na namba zao za simu.

Hakuna hata mmoja aliyepokea simu, nikauliza wanafunzi wachache ambao walikuwepo shule ambao walijitambulisha kuwa jumuiya ya kikristo na walikuwa wakijiandaa kufanya mahafari yao, ili wanieleze ni namna gani naweza kupata mwalimu wa zamu nikaambiwa walimu wote wamenda trip kwa vile siku hiyo ilikuwa ni sikukuu.

Hivo nilimomba kijana mmoja anitafutie mwanangu alipokuja uso wote ulikuwa umevimba na sura imeanza kupotea. Nikamshika kichwa kama nanyanyua kidevu juu kwa kuwa niliona kuna dalili za pua kuvimba, ghafla mtoto akaanza kutokwa na usaha mwingi sana puani.
Kwa vile hakukuwa na mwalimu nilichukuwa jukumu la kumwahisha mtoto hospitali, hospitali ya kwanza ilikuwa ni Aga Khan iliyoko mkoa huo, ambao walijaribu kunyonya usaha kwa kutumia sindano lakini bado usaha haukukoma, siku ya tatu nikamuhamishia Aga Khan DAR ambako ilionekana ana jipu kubwa puani kuelekea kichwani na anatakiwa upasuaji wa haraka.

Upasuaji ulifanywa chini ya ETN Physician Pro Massawe. Baada ya siku saba mtoto aliruhusiwa kutoka hosp na hatimaye kurudi shule. Kipindi chote mtoto akiwa shule nilikuwa nawasiliana na mwalimu wa malezi, ajabu siku mtoto anarudi shule wakamkataa kuwa aende na mzazi, ikabidi mke wangu aende wakakataa wakadai wananitaka mimi niliyeiba mtoto shule, sikufanya ajizi nikaenda tukaparulana sana kwenye kikao. Nikaambiwa kwangu mimi uhai wa mtoto ilikuwa ni mhimu kuliko kuhudhuria masomo kwa wakati huo, pamoja na ushahidi wa picha mtoto akiwa theatre na akiwa wodini na risti zote za gharama za matibabu takriban milion 7 hivi, lkn walimu wa hiyo shule walijifanya hawaelewi.

Mpka kikao kinaisha wakadai watampa mtoto adhabu nikawaambiwa siko tayari, kwa shingo upande wakampokea mtoto. Lakini mwaka ulifuata wakafukuza mtoto shule wakidai wamekuta na simu chini ya godoro simu ambayo yeye alidai siyo ya kwake. Na akaenda mbali akidai hiyo simu iletwe siku ya kikao cha maamuzi lakini hawakufanya hivo. Mtoto akasimamishwa masomo na kuruhusiwa kurudi kufanya mtihani wa mwisho.

Nikamchukuwa mtoto nikampeleka shule ya binafsi nikalipa ada akasoma ilipokaribia mtihani akaenda wakamkataa na kusema alishafukuzwa kwa hiyo afanye mtihani akitokea nyumbani. Changamoto mimi niko Dar mtoto atoke Dar kwenda Morogoro kufanya mtihani. Nikatafuta suluhisho bahati nzuri chuoni wanachuo walikuwa wamemaliza ama wako likizo nikapanga hostel ambayo nayo niliambiwa nilazima nilipe miezi mitatu. Nikalipa mtoto akafanya mtihani matokeo kuja ana one na maisha yanaendelea.

Ningekuwa sina uwezo huo mtoto asingefanya mtihani kwa sababu ya uzembe wa shule ambao uligeuzwa kuwa chuki kwa mwanangu. Walimu wanatabia ya kujaribu sana mara nyingi kukomoa wazazi.
 
Nina uhakika mleta mada kwa namna yoyote hao wazazi watajikuta ndo wenye makosa wala usihangaike sana huku JF, hakuna mwalimu yeyote Tanzania anaweza kujiwekea sheria za namna hiyo haswa enzi za sasa hivi, sheria hizo zitakuwa na baraka za wananchi wenyeji wa shule hiyo ikiwemo ngazi ya serikali za mitaa hiyo...
Si watetei walimu kabisa, lkn hata ukiangalia hawa ambao wengi hujiita kamati ya shule ni mnyororo wa kuwakamua wazazi kwa sababu unakuta wamekaa labda watu kumi wanapitisha maazimio ambayo, hayahusishi majority. Hizo rim 8 kwa siku nane zinafidia nini ktka masomo aliyokosa huyo mtoto? kama ana jeraha ambalo linaonekana kwa nini utu ustumike?

Maisha yalivo huyo mzazi unakuta anaangaika kutafuta riziki kwa ajili ya huyo mtoto, pengine ameajiriwa hizi kazi za wahidi utamwambia unaomba ruhusa ili uwende shuleni kwa mtoto anaweza toa au asitoe, soma post yangu hapo chini ili ujue yanayofanyika kipindi hiki hiki unachodai hayawezi kufanyika
 
Hizo ni sheria za ndani(by laws)ambazo hukubaliana baina ya wazazi na walimu katika vikao vya wazazi.Afisa mtendaji na MEK pia wanakuwepo au wawakilishi wao pamoja na wenyekiti was vijiji na madiwani.mkishakubalian suala linabaki ,gumu kwa wazazi .mtoto akipata tatizo na hajatoa lipoti kimsingi anakuw kinyume na utaratibu huo.
 
Hakuna sheria hiyo nenda kwa afisa elimu ukishindwa nenda kwa mkurugenzi ukishindwa lirudishe hapa tujue namna ya kukushauri
 
Back
Top Bottom