Hii imekaaje kisheria wanafunzi kutozwa faini mashuleni

Mr Benja

Member
May 28, 2018
44
40
Heshima kwenu wakuu.

Ipo hivi nina jirani yangu mwanae anasoma shule fulani hapa jijini Dar es Salaam pale eneo la Temboni-Ubungo. Ni shule ya sekondari ipo chini ya umiliki wa serikali. Wiki iliyo pita tangia tarehe 3/07/2020 mwanae (wakike) alipata ajili ya kuchubuliwa(kukatwa) na kipande cha chupa kwenye mguu wake wa kushoto na kumsababishia maumivu makali na uvimbe.

Wakati huo alikua akipatiwa matibabu ya kawaida tu ya nyumbani kwa kukanda na maji ya vuguvugu na chumvi. hadi sasa jeraha limepata auheni tunamshukuru Mungu sana hadi wakaona inafaa kumruhusu mtoto aende shule wiki hii tarehe 13 mwezi huu kwa ajili ya kuendelea na masomo.

Cha ajabu walimu wakamrudisha nyumbani ili aje na mzazi wake. Mimi pamoja na mzazi wake leo tumeenda shuleni tumesangazwa na tulio ambiwa, Ni mambo ya ajabu sana..

Eti wanasema mtoto hajahudhuria shuleni takriban wiki nzima, na kila siku moja faini yake ni Rimu moja ya karatasi nyeupe (@tsh 11000). Kwa maana hiyo mtoto hakuhudhuria siku takriban 8 hivyo ni faini ya Rimu 8 kwa ujumla wake (tsh. 88000), Pamaja na pesa taslimu shilingi elfu hamsini (50,000) kwa ajili ya kupeleka serikali ya mitaa.

Msaada wangu kutoka kwenu wajuvi wa mambo ni kutaka kujua utaratibu huu wa kutoza fani umeanza lini..? Na hatakama utaratibu huo upo je kwa mazingira ya namna hii ya mwanafunzi kupata ajali na ushahidi wa jeraha upo unamhusu vipi mtu wa namna hiyo?

Sipati picha hapa mjini ipo hivi je huko vijijini itakuwaje.

P1180629.JPG
 
Je mzazi/mlezi alitoa taarifa ya ugonjwa wa mwanafunzi/mtoto wake shuleni au unauliza kiushabiki tuu?
Kwa maelezo yake Taarifa hakutoa, hii ni kutokana na kutokua na mawasiliano na uongozi wa shule yaan nambari zao za simu, na umbali kati ya shuleni hapo na nyumbani kwa mwanafunzi huyo . Lakini kama haitoshi mtoto amekuja na vielelezo vya nyaraka mbalimbali za manunuzi ya dawa na ushahidi wa jeraha physically.. Yani jeraha bichi lipo linaonekana pasipo kuwa na shaka yoyote
 
Kwa maelezo yake Taarifa hakutoa, hii ni kutokana na kutokua na mawasiliano na uongozi wa shule yaan nambari zao za simu, na umbali kati ya shuleni hapo na nyumbani kwa mwanafunzi huyo . Lakini kama haitoshi mtoto amekuja na vielelezo vya nyaraka mbalimbali za manunuzi ya dawa na ushahidi wa jeraha physically.. Yani jeraha bichi lipo linaonekana pasipo kuwa na shaka yoyote
Hiyo adhabu inatokana na kutokuwepo connection baina ya mzazi na walimu.maendeleo ya mwanafunzi kitaaluma ni lazma kuwe na ufuatiliaji wa karibu wa mzazi na mwalimu na wawe wanawasiliana.wazazi hawafuatilii maendeleo ya watoto wao wakiwa mashuleni kiasi kwamba walimu wanaamua kutengeneza sheria kali kama hizo..
 
Hiyo adhabu inatokana na kutokuwepo connection baina ya mzazi na walimu.maendeleo ya mwanafunzi kitaaluma ni lazma kuwe na ufuatiliaji wa karibu wa mzazi na mwalimu na wawe wanawasiliana.wazazi hawafuatilii maendeleo ya watoto wao wakiwa mashuleni kiasi kwamba walimu wanaamua kutengeneza sheria kali kama hizo..

Hakuna adhabu ya namna hiyo, uwe umetoa taarifa, uwe hujatoa taarifa.

Hakuna.
 
Hiyo adhabu inatokana na kutokuwepo connection baina ya mzazi na walimu.maendeleo ya mwanafunzi kitaaluma ni lazma kuwe na ufuatiliaji wa karibu wa mzazi na mwalimu na wawe wanawasiliana.wazazi hawafuatilii maendeleo ya watoto wao wakiwa mashuleni kiasi kwamba walimu wanaamua kutengeneza sheria kali kama hizo..
Unaita WIZI kua ni Adhabu, are you for real?
Kwani kama mtu unaona eneo lako la kazi halikupi kipato unachokihitaji kwanini usiachane napo ukaangaza mbele kuliko kuumiza wengine?
 
Hiyo adhabu inatokana na kutokuwepo connection baina ya mzazi na walimu.maendeleo ya mwanafunzi kitaaluma ni lazma kuwe na ufuatiliaji wa karibu wa mzazi na mwalimu na wawe wanawasiliana.wazazi hawafuatilii maendeleo ya watoto wao wakiwa mashuleni kiasi kwamba walimu wanaamua kutengeneza sheria kali kama hizo..
Ground ya tukio hili ni shiria ya tozo la faini ya fedha au mali kwa wazazi, kukinzana na sheria zetu za nchi. Kimsingi haikua busara kwa walimu kutoza faini za fedha taslimu au mali mbadala wake wangeli toa angalau adhabu kwa wanafunzi wakosefu
 
Ground ya tukio hili ni shiria ya tozo la faini ya fedha au mali kwa wazazi, kukinzana na sheria zetu za nchi. Kimsingi haikua busara kwa walimu kutoza faini za fedha taslimu au mali mbadala wake wangeli toa angalau adhabu kwa wanafunzi wakosefu
Mi nafikiri ingekuwa busara zaidi mkarudi na kuliweka sawa hili kwan haikuwa na haja kutoza fine kwa mwanafunzi aliye na sababu kama hyo.

Kama itashindikana ni bora ukaenda kwa Afisa elimu kulalamika kwan naamini ukilileta huku bado hutoweza kupata suluhu kamili na hata ikitokea walimu wametumbuliwa huko shuleni ataye athirika ni mwanafunzi na wanafunzi wenzie.
 
Inawezekana ni sheria ndogo (bylaws)zilizowekwa na serikali za mtaa(kata) ili kudhibiti utoro.Kama ni hivyo je wazazi mlishirikishwa/kufahamishwa juu ya sheria/taratibu hizo?
Umewaza kama mimi maana hakuna namna walimu wanaweza kujitungia tu taratibu hizo. Maana hata hiyo pesa wamesema inakwenda serikali ya kijiji.
 
Kwa maelezo yake Taarifa hakutoa, hii ni kutokana na kutokua na mawasiliano na uongozi wa shule yaan nambari zao za simu, na umbali kati ya shuleni hapo na nyumbani kwa mwanafunzi huyo . Lakini kama haitoshi mtoto amekuja na vielelezo vya nyaraka mbalimbali za manunuzi ya dawa na ushahidi wa jeraha physically.. Yani jeraha bichi lipo linaonekana pasipo kuwa na shaka yoyote
Mkuu, kiuhalisia hapo ni kwamba mzazi/mlezi wa mtoto/mwanafunzi anakomolewa somehow kwa maana ya kushindwa kuonyesha ushirikiano kwa walimu wa mtoto wake kwa sababu aliyekuwa anaumwa ni mtoto na mzazi angefanya hima kutoa taarifa shuleni kwakuwa serikalini kinachoaminika ni sick sheet na si vinginevyo na siku hizi miongozo ni mingi mno kwenye kazi za serikali hadi sio poa
 
Umewaza kama mimi maana hakuna namna walimu wanaweza kujitungia tu taratibu hizo. Maana hata hiyo pesa wamesema inakwenda serikali ya kijiji.
Kwaiyo wazazi wasipo kuwa na hiyo pesa watoto wao waache shule..? hiyo bylaws ni ya kikoloni na kandamizi kabisa.. serikali za mitaa hawawezi kukaa na kutunga sheria inayo kinzana na katiba ya nchi.. Any law against national constitution is invalid.
 
Kwaiyo wazazi wasipo kuwa na hiyo pesa watoto wao waache shule..? hiyo bylaws ni ya kikoloni na kandamizi kabisa.. serikali za mitaa hawawezi kukaa na kutunga sheria inayo kinzana na katiba ya nchi.. Any law against national constitution is invalid.
Mkuu unajua kwamba kuna sheria ndogo ndogo ambazo zaweza kutumika kama reference hata kwenye hyo katiba ya nchi?

90 days mwanafunzi asipohudhuria shule huyo ni mtoro na sheria ndogo-ndogo za wizara zinaeleza kuwa mwanafunzi huyo kufutwa ni 90-100% lakini katiba inasema kila mtu ni sawa na haki vile vile ni sawa
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom