Mna akili za kikatili sana. Halafu mnadhubutu kwenda makanisani na misikitini kusali na kuswali.
Tanzania imesaini mikataba ya haki za binadamu. Kila binadamu hata aliyevunja sheria, ana haki ya kusikilizwa na kuadhibiwa kwa namna sheria zinavyosema.
Tukitaka kutenda matendo ya kinyama kama hayo, tuwaite al-shabaab waje watutawale. Au sisi wenyewe tujitangaze kuwa tumeweka sheria pembeni kwa muda ili tuuvae unyama na kutenda hayo mambo ya kinyama.
Ushauri wangu ni serikali kuongeza nguvu, ubunifu na weledi wa jeshi la polisi. Kama ikiwezekana hili jeshi la nchi nzima lipunguzwe ukubwa ili yaundwe majeshi madogo madogo ya majiji, miji nk. yanayoendana na mahitaji ya mahali husika.
Tusikubali jeshi la polisi lijifiche na kukimbia jukumu la ulinzi na usalama wa raia na mali zao. Tusikubali kujiingiza kwenye umwagaji damu usiofuata misingi ya sheria.