Hii 'back turn' ya Butiku ni ya mashaka

Hii 'back turn' ya Butiku ni ya mashaka

Quinine

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2010
Posts
24,149
Reaction score
56,439
Mimi ni Tomaso, hiki kigeu geu cha ghafla kinanitia wasiwasi, juzi alikuwa na wauaji leo anawatetea aliowasaliti juzi, je ni dhamiri yake au kuna msukumo wa nje au kuna project ambayo watawala wanataka waifanye kwa kutumia mgongo wake baada ya kushindwa kumshawishi Warioba.

Ni juzi tu alikuwa akiwananga vijana kuwa watoe hoja kwa utaratibu si maandamano, akawaambia hoja hazitatuliwi kwa kuharibu mali, ni juzi tu alisikika akimwambia Kapteni Tesha aliyewatetea vijana kuwa sio askari hana nidhamu ni muhuni.

Leo anawaambia vijana wana haki ya kuandamana, anawaambia watawala kuwa wasiseme hawawajui wauaji, anamwambia Katibu Mwenezi CCM kuwa anafanya siasa za hovyo, anawaambia CCM kuwa wanafanya siasa huku CHADEMA na mkiti wao LISSU wamewafungia kufanya siasa.

Wasiwasi ndio akili, ngoja niendelee kuwa tomaso hadi trh 22/1 atakapokutana na wazee wa Dar kina Kikwete labda nitaelewa lengo lake hasa ni nini.
 
Kakaa kimya muda wote huu, toka mauaji ya october, toka rafiki yake Polepole atekwe. Anatokea sasa hivi miezi miwili na nusu baadaye kujikosha.
 
Haaminiki huyo,ila muda utasema mana hata saa mbovu kuna muda inasema ukweli.

Unaua raia wako wasio kuwa na silaha za moto kisa madaraka,hili halisahauriki wala halisamehekei.
 
Huenda AMEGUNDUA kuwa wananchi wamekosa imani naye na wamemweka kapu moja na akina Lukasi Mashamba. Wakati mwenzie mzee Warioba (mzee pekee anayezeeka mwili bila kuzeeka akili) akiwa amejizolea pointi zote za heshima. Sasa Butiku anajaribu kuvuta mioyo ya watu...
 
Binadamu anapokuwa mtu mzima akili yake husinyaa na kurudi kuwa kama mtoto mdogo.
Butiku ni mzee aliyefikia vigezo vyote vya akili kurudi utotoni....

Asikilizwe lakini apuuzwe tu na zaidi sana asipewe saaana audience na nyombo vya habari vinginevyo vitaishia kufokewa.
 
Mpango mzima (kwa jicho la pembeni)ni kwamba hiyo tarehe 22/01/2026, hao wazee watakaa na kutoka na kauli kwamba Lisu aachiwe, chadema ifunguliwe, Mchakato wa katiba na Tume Huru uanze na au uharakishwe ili kuondoa malalamiko ya wananchi.

Hawa wazee ni kama vile wanatuona hatujui ni mchezo gani wanataka au wapenga kuufamya.

Halafu serikali itatekeleza maazimio yao na kusema kwamba imewasikiliza wazee wenye Busara na ndicho ilicho kifanya- just to save face.

Haya mambo ya kesi ya Lissu na kufungukiwa kwa wapinzani- Lissu na Mpina, hayakutakiwa kabisa kutokea kabisa...
 
Mpango mzima (kwa jicho la pembeni)ni kwamba hiyo tarehe 22/01/2026, hao wazee watakaa na kutoka na kauli kwamba Lisu aachiwe, chadema ifunguliwe, Mchakato wa katiba na Tume Huru uanze na au uharakishwe ili kuondoa malalamiko ya wananchi.

Hawa wazee ni kama vile wanatuona hatujui ni mchezo gani wanataka au wapenga kuufamya.

Halafu serikali itatekeleza maazimio yao na kusema kwamba imewasikiliza wazee wenye Busara na ndicho ilicho kifanya- just to save face.

Haya mambo ya kesi ya Lissu na kufungukiwa kwa wapinzani- Lissu na Mpina, hayakutakiwa kabisa kutokea kabisa...
Mkuu uko mule mule, maana imekuwa ghafla mno kwa huyu mzee kubadilika ndio maana jana kagusia Chadema kufungiwa na Lissu kuendelea kushikiliwa.
 
Mimi ni Tomaso, hiki kigeu geu cha ghafla kinanitia wasiwasi, juzi alikuwa na wauaji leo anawatetea aliowasaliti juzi, je ni dhamiri yake au kuna msukumo wa nje au kuna project ambayo watawala wanataka waifanye kwa kutumia mgongo wake baada ya kushindwa kumshawishi Warioba.

Ni juzi tu alikuwa akiwananga vijana kuwa watoe hoja kwa utaratibu si maandamano, akawaambia hoja hazitatuliwi kwa kuharibu mali, ni juzi tu alisikika akimwambia Kapteni Tesha aliyewatetea vijana kuwa sio askari hana nidhamu ni muhuni.

Leo anawaambia vijana wana haki ya kuandamana, anawaambia watawala kuwa wasiseme hawawajui wauaji, anamwambia Katibu Mwenezi CCM kuwa anafanya siasa za hovyo, anawaambia CCM kuwa wanafanya siasa huku CHADEMA na mkiti wao LISSU wamewafungia kufanya siasa.

Wasiwasi ndio akili, ngoja niendelee kuwa tomaso hadi trh 22/1 atakapokutana na wazee wa Dar kina Kikwete labda nitaelewa lengo lake hasa ni nini.
Nakubaliana na wewe kuwa Huyu Butiku sio mtu wa kumuamini kwani anatumia taasisi na jina la Nyerere kama kitega uchumi chake , na hana credibility tena kwa wa Tanganyika! Sio Siri kuwa kumsaliti Kwake Humphrey Polepole ni pigo kubwa sana kwa wazalendo wa nchi hii. Hata akatae vipi ukweli utabakia pale pale kuwa alimuuza kwa vipande vya fedha toka kwa Samia na hii ndio sababu ya kuweweseka kwake!
Kuhusu ccm kumshambulia Warioba kuwa asizungumze hadharani kutoa maoni yake juu ya serikali, Hawa vijana wa ccm hawajui historia ya chama na serikali yao ndio maana wanalopoka hovyo. Kukosolewa kwa viongozi wa serikali na chama hakujaanza leo ! Nyerere alimkosoa Rais Mwinyi hadharani kuhusu udhaifu wa uongozi wake na kuifanya Ikulu pango la walanguzi . Nakutokana na ukosoaji huo nchi hii ikanusulika!!
Sasa huo ulikuwa wakati wa mtu msikivu kama marehemu mzee Mwinyi sembuse leo enzi za “Chura kiziwi “ : Huyu kiziwi bila kumkosowa hadharani anaipeleka nchi hii Kizimu! Hivi sasa tu ametumia u.s$ million moja Kukodisha kampuni iwabembeleze wafadhiri (aliowaita WHO ARE YOU ?)wampe mikopo : bila kumthibiti binti Kiziwi atauza nchi.
Hawa wazee anaowajua Butiku wasipoteze muda ,kama wana hoja wazipeke kwa jaji Chande wasipoteze wakati na huyu mamluki Butiku.
 
Nchi hii inatakiwa kuanza upya. Historia mbovu ya uasisi wa taifa hili iliyohusisha chama kilichoko madarakani, muungano unaofanana na ndoa za utotoni na taasisi zote za ulinzi wa raia na mipaka ya nchi vinatakiwa kuwekwa kwenye makumbusho ya taifa.

Tuweke misingi mipya ya utawala unaotii matakwa ya raia kama mwajiri wa watawala na vyombo vyake.
 
Nchi hii inatakiwa kuanza upya. Historia mbovu ya uasisi wa taifa hili iliyohusisha chama kilichoko madarakani, muungano unaofanana na ndoa za utotoni na taasisi zote za ulinzi wa raia na mipaka ya nchi vinatakiwa kuwekwa kwenye makumbusho ya taifa.
Tuweke misingi mipya ya utawala unaotii matakwa ya raia kama mwajiri wa watawala na vyombo vyake.
Tunatakiwa kubonyeza button ya RESET TANZANIA ili tuanze upya.
 
Back
Top Bottom