DullyJr
JF-Expert Member
- Apr 10, 2011
- 13,979
- 11,815
Rafu aliyocheza moroco ikasababisha goli haikuwa na sababu wakimrekebisha atakuwa mchezaji bora zaidi kwani tayari ni boraHuyu Inonga ni bonge la beki akili mingi sana. Kuna wakati unaweza sema keshapitwa na unasubiri watu warudi kati wapi bwana sekunde tu jamaa unakumta kashaingia uvunguni kwa mshambuliaji wa timu pinzani halafu anatoka na mali kama yake. Wakati mabeki wengi wanakimbilia kucheza rafu ndani ya boksi huyu mwamba yeye huwa anaenda kuuchukua mpira bila kufanya faulo yoyote.
Ila kwa zile rasta nahisi jamaa anatumia nyasi kavu kwani kuna wakati huwa anakuwa na hasira pasipo sababu za msingi anaanza kuwafokea wachezaji wenzake kati kati ya mchezo badala ya kuwaelekeza vizuri. Pia wakati mwingine anakuwa na ubabe usio na msingi na wachezaji wa timu pinzani tena mbele ya waamuzi kiasi anakaribisha kadi zisizo na msingi kabisa. Benchi la ufundi la Simba lifanyie kazi haya mapungufu yake machache.