Helikopta ya Jeshi, ZINAKODISHWA?

Halisi

JF-Expert Member
Jan 16, 2007
2,802
613
Pamoja na kukosewa kwa headline ya ajali ya helikopta, swali langu ni je, helikopta za jeshi zinakodishwa? Je, walikuwa watalii ama wageni wa jeshi/serikali? Niliwahi kumsikia KAtibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Blandina Nyoni, akisema, wageni wetu wamepata ajali ya helikopta lakini hawajafa. Je ni watalii ama wageni wa serikali? Lakini mbona kuna muongoza watalii na si ofisa wa serikali? Je, ni zile helikopta ambazo walizileta akina VITHLANI na mwenzake Tanil Somaiya wa kesi ya RADA?


Walionusurika ajali ya Helikopta ya jeshi watajwa

na David Frank, Arusha


 
Mazingaombwe na maluelue mengine haya. Nani anayeruhusu chopa za Jeshi kufanya biashara? Wanalipa kwa nani? Hizo pesa zinakuwa accounted wapi?

Jeshi lina chopa ngapi? Ziko vituo gani na kwa shughuli ipi?
 
Halisi hivyo ni vitu vya msingi sana ulivo uliza, pamoja na hayo, vipi quality ya hizi helikopta zenyewe? kwani nilisikia hazikuwa zina kidhi viwango, je huenda ni sababu za viwango duni ndo maana imeanguka??
 
Hold on a minute.. Bi. Nyoni (Katibu Mkuu Maliasili na Utalii) alipohojiwa mara baada ya ajali alisema Helikopta hiyo ilikuwa na "wageni wa serikali" those are her exact words. Sasa inawezekana walikuwa ni wageni wa Serikali ambao waliamua kufanya utaliii kidogo na wakashinda kupata usafiri mwingine wowote ambao ungempa biashara mswahili mwingine isipokuwa wa Helikopta...otherwise, kuna Prof. Ndumba Nangae mahali fulani
 
Hivi hiyo helikopta ndio hizi zinazouzwa? au ndio biashara imegomba sasa zinakodishwa?


http://www.thisday.co.tz/News/2853.html
 
Hizo Ndizo Helicopter Vithlani Alizotubambika..the Only Verdict Fitting This Husler Vithlani Is A Deathrow...]..ametuuzia Civilian Choppers Wakati Alitakiwa Atupe Millitary Brand....kapewa Oda Ya Choppers ...hajamaliza Ku Deliver....wizi Huuu...another Valambia!!!!!

Jeshi Letu Linahitaji Gunship Choppers Sio Hizi ..na Mjue Gharama Ya Kununua Vifaa Feki Vya Kijeshi....wakati Wa Amani ..ndio Huleta Gharama Kununua Vitu Genuine Wakati Wa Vita!!!! Sasa Why Not Being Honest And Nationalist..chida Yetu Mtu Anakula Rushwa Na Ananunua Vitu Mbovu...wakati Nchi Nyingine Wana Ufisadi Kwenye Millitary Procurement ..lakini Haiadhiri Ubora Wa Vifaa ...
 
Ndio hizi tiktak tumekuwa tukifichwa, sasa ajali zinafumua kila kitu. Nakumbuka mwaka juzi shangingi fulani la sirikali lilipata ajali wilayani Mkuranga mkoani Pwani likiwa limesheheni pembe za ndovu. Watu wakaanza kuulizana, meno yale yalikuwa ya nani na yanakwenda wapi? Nakumbuka viongozi fulani wa sirikali walilikana shangingi lile kuwa sio lao, ni la mradi wa UNDP, nao UNDP wakasema mradi ulikuwa umeisha na gari likarejeshwa sirikalini. Yaani ilikuwa tiktak kwenda mbele. Sijajua mpaka kesho ile kesi imeishia wapi, ila nataka kuwahakikishia wana JF kuwa haya mambo yapo kwa wingi sana sirikalini.
Kama mtakumbuka miaka michache iliyopita, Magufuli akiwa waziri wa ujenzi aliwakoromea vigogo wa sirikali waliokuwa wamesajili magari yetu walipakodi kwa namba za kiraia huku wakiwa wanachukua mafuta katika visima vya sirikali, wakati magari yakifanya kazi binafsi. Sirikalini kumeoza sana kwa dili feki kama hizi.
Kwa hiyo huenda hizi choppers zilikodishwa kwa maslahi binafsi! Sitashangaa.
 
Ninachojua mimi msafara huu haukuwa wa watalii, kulikuwepo na watu kutoka ofisi ya raisi ambao walikuwa wameruka the day before ambao walitumwa kufuatilia utata unaoendelea sasa hivi kuhusu ujenzi wa soda ash factory ambao umeshindwa kuendelea baada ya Enviromental Impact Assesment report kuonyesha kwamba mradi is not sustainable na ungeharibu kabisa breeding site ya flamingo.

kiwanda hiki cha chumvi kinaitwa TATA kutoka India. Roumour has it that EL anataka sana hiki kiwanda kiendelee lakini watu wengi hasa conservation activist wameupiga vita kabisa na wengi bado wanaendelea kuupiga vita.

Inasemekana JK alituma vijana wake wakatafuta na wataalamu wanaolijua eneo ili kumsaidia kufanya decision kama TATA ifanye kazi au la.
 

Power to the people, hebu tueleze vizuri hao wageni waliotajwa na RPC wa Arusha wanatoka wapi kama ilikua ni safari ya maofisa wa serikali?
 

This is a problem of leaders who self-serve. Their self-interests are above everything else.
 
Wajamaa wa serikali walikuwa wafanya trip the day before, hao waliopata ajali walienda kama wataalamu, huyo muaustralia alikuwa mpiga picha na huyo jamaa wa uingereza anayeishi arusha alichukuliwa kwa sababu ni mtaalamu wa mimea na ndege na ameshafanya kazi katika maeneo hayo.

hao wengine sina uhakika walikwenda kama nani.
 

Mkuu Huoni kama maelezo yako yanapingana kabisa na maelezo ya Waziri wa Utalii hapa??

Angalieni jinsi Waziri wa Utalii anavyodanganya Watanzania waziwazi....

My Take: Hii ni biashara ya pembeni ya baadhi ya wakuu wa JWTZ; na kama ilivyo kawaida HAKUNA mwenye UJASIRI ndani na nje ya Sirikali wa kuwauliza maswali wakuu wa JWTZ.

 
JWTZ na utalii!

JUMATANO iliyopita helikopta inayomilikiwa na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) ilianguka na kushika moto Ziwa Natron mkoani Arusha.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoani Arusha, Matei Basilio, abiria waliokuwamo katika helikopta hiyo hawakuwa wanajeshi, bali watalii ambao walikwenda katika eneo hilo kwa lengo la kupiga picha maeneo ya vivutio vya utalii.

Maeneo hayo ni pamoja na Ziwa Natron na Mlima Oldonyo Lengai, ambao una sifa ya kutoa volkano hai na unaosifika kwa kulipuka mara kwa mara.

Kamanda Basilio aliwataja watalii walionusurika katika ajali hiyo kuwa ni Jeffrey Sibbery anayetoka Canada, Forest Sowyer (Marekani), Ben Herberston (Australia) na Mark Berker wa Uingereza. Pamoja nao, alikuwapo mkazi wa Kisongo wilayani Arumeru, Issaya ole Poruo, ambaye ilielezwa ya kuwa alikuwamo katika helikopta hiyo kwa ajili ya kuwaongoza watalii hao.

Kwamba helikopta ya JWTZ ilikuwa imebeba watalii pamoja na mwongozaji wao, kwa nia ya kupiga picha vivutio vya utalii mkoani Arusha, ni jambo linaloshangaza.

Linashangaza kwa sababu hakuna uhusiano wa aina yoyote kati ya JWTZ na utalii kikazi. Ilikuwaje basi, watalii wakumbwe na balaa la ajali wakiwa katika chombo kinachomilikiwa na jeshi hilo?

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Profesa Juma Athumani Kapuya na naibu wake, Omar Yussuf Mzee, hawakuwa na majibu ya kutosheleza juzi walipoulizwa baada ya kupigiwa simu.

Wakati Kapuya alisema yuko likizoni Kaliua, Tabora, na hajui chochote kuhusiana na suala hilo na kulitaka gazeti hili kumtafuta mkuu wa majeshi alielezee, naibu wake angalau alionekana kuguswa ingawa naye hakuwa na jibu la kutosheleza.

Naibu Waziri alisema tayari ameomba apatiwe taarifa za suala hilo kutoka uongozi wa JWTZ kuhusu nani walikuwamo, helikopta hiyo ilikuwa inafanya nini huko na sababu za ajali yake. Kama ilivyokuwa kwa Kapuya, naye pia alilitaka gazeti hili kupata maelezo kutoka JWTZ kwenyewe, na kumtaka mwandishi awasiliane na Mnadhimu Mkuu wa Jeshi kwa maelezo.

Kama ilikuwa inafanya kazi huko kwa maslahi ya watu binafsi, watu hao ni nani na kwa nini wasichukuliwe hatua?

Tunasema hivi kwa sababu tayari kuna hisia kwamba huenda helikopta hiyo ilikodiwa na kama ilikuwa hivyo, huo ndio utaratibu wa kawaida na unafahamika?

Upo wasiwasi miongoni mwa jamii kwamba vyombo vya asasi ambavyo vinanunuliwa kwa bei kubwa kutokana na kodi za wananchi, vinatumika vibaya na wanasiasa na watu waliokabidhiwa kwa ajili ya asasi hizo.

Kwa kweli kuna haja kwa serikali kuanza kulitolea maelezo suala hilo. Na bila shaka watu wengi watakuwa na shauku ya kusikia maelezo kuhusiana na ajali hiyo ya helikopta ya JWTZ mkoani Arusha ikiwa na kundi la watalii.

Haiyumkiniki kwamba waziri mwenye dhamana ya Ulinzi anajivua wajibu kwa maelezo kwamba yuko likizo na kwa sababu hiyo hana taarifa kuhusu tukio muhimu kama hilo.Waziri ni waziri wakati wote, hata anapokuwa likizo na ni wajibu wake kushughulikia mambo yanayojitokeza katika himaya yake, hususan pale mambo hayo yanapoelekea kuzua maswali mengi zaidi kuliko majibu.

Bado tutakuwa na shauku ya kujua ni nini hasa kilitokea katika ukodishaji wa helikopta hiyo na ajali iliyotokea. Baadhi ya wananchi wameanza kujiuliza iwapo helikopta hiyo ina uhusiano wo wote na taarifa za hivi karibuni kuhusu utoaji wa zabuni za vifaa vya jeshi hilo kwa wafanyabiashara waliohusishwa na utaratibu usioridhisha wa utoaji tenda kwa ajili ya ununuzi wa vifaa hivyo. Wananchi wanayo haki ya kupata maelezo kamili.
 
Pamoja na utata wote huo bado sioni kama mtu ndani serikali ya JK anaweza kusimama na kutoa tamko kuhusu hiyo kadhia ya Chopper za JWTZ. Kweli Bongo watu wanafanya kufuru tena kwa kiburi kabisa na kwa uwazi mkubwa na wanajua hata bomu likilipuka hakuna madhara maana awamu ya nne mambo ni tambarare, kila mtu anawahi chake mapema kabla mtandao haujasambaratika kabisa.

Mungu endelea kuwaumbua kwa kuwaweka nuruni ili hayo madudu wanayoyafanya yajulikane, maana hiyo shughuli kama ingeisha salama ndiyo watu wangekuwa wameishalamba BINGO ya nguvu na watu tusingejua lolote. Lakini ajali hiyo imetufumbua macho na wao wanazidi kushituka na kuona kwamba dili za gizani zinaendelea kuonekana na hivyo kuwaumbua. Kaazi kweli kweli, lakini tutafika tu hata kama ni mbali sana!!
 

Usishangae EL anahisa kubwa katika kiwanda hicho TATA. Hayo ndiyo maandalizi ya ufisadi LIVE
 
Air of mystery engulfs TPDF helicopter crash

-All passengers and crew members survived, but the questions still linger

THISDAY REPORTER
Dar es Salaam

WHY was a Tanzanian military helicopter used to fly a group of foreigners on an assignment to shoot a wildlife documentary film in Arusha Region?

This is the big question now emerging following last week’s near-fatal crash involving a Tanzania People’s Defence Forces (TPDF) chopper in the Lake Natron area.

The 12bn/- aircraft, now believed to have been one of the four Agusta Bell model 412 EP helicopters owned by the military, was apparently on a civilian mission when it went down and exploded on Wednesday morning, with eight people on board.

Although all civilian passengers and military crew members survived, questions now linger on how a TPDF chopper came to be used for an obviously non-military mission.

When contacted for comment by THISDAY, the Deputy Minister for Defence and National Service, Omar Yusuf Mzee, said he was also in the dark over the whole incident.

Mzee said he had instructed the TPDF top brass to send him a report on the accident and circumstances leading up to it.

’’I am still waiting for the report�you can contact the military for additional information on the matter,’’ he said.

The Chief of Defence Forces (CDF), General Davis Mwamunyange, was yesterday not immediately available for comment.

It has been established that the military helicopter was being deployed by a crew of four television documentary makers from assorted Western countries - Australia, Canada, the United States and Britain � on a mission to film flamingos over Lake Natron.

The Arusha Regional Police Commander, Matei Basilio, identified the crash survivors as Jeffrey Sibbery (Canada), Forest Sowyer (US), Ben Herberston (Australia) and Mark Berker (UK).

Tanzanians who survived the crash were named as Lt. Col. Mayenga, the TPDF pilot; Lt. Edward (his co-pilot), helicopter technician Gabriel Majala, and the crew�s tour guide Issaya ole Poruo.

Interviewed by one Australian newspaper, two of the crash survivors - Sydney cameraman Ben Herbertson and producer Jeff Sibbery - narrated how they had been in the air for little more than five minutes and were flying at a very low altitude over the lake, when the pilot dipped too low - catching the water with the helicopter’s landing skis.

In an instant, they said, the aircraft plunged nose-first into the shallow lake, breaking apart and tossing those on board into the hot, caustic water.

’’The skids hit the water and we just crashed and smashed into pieces,’’ Herbertson said.
’’The next thing I knew, I was in the lake and the water was burning my eyes.’’

He added: ’’The reason the flamingos breed there is because the conditions are so harsh there are no predators. The water is physically hot.’’

Sibbery broke his hip on impact, while the pilot, Lt. Col. Mayenga, ended up with a badly broken leg and deep bleeding cuts on his face.

’’We managed to get all the injured people out of the helicopter, but then we had to figure out how to get out of there because it really looked like it was going to explode,’’ Herbertson said.

According to the survivors, it was the women and children from nearby Maasai tribal homesteads who came to their rescue. And as they were being assisted onto the salt plateau, the wreck of the helicopter did explode, sending an empty fuel tank flying and a plume of thick black smoke into the air.

Reports say the group was planning an extended flight so the chopper was heavy with fuel, but luckily nobody was injured in the blast.

The injured Sibbery and pilot Mayenga were airlifted out of the area, the former to a hospital in Nairobi in neighbouring Kenya where he underwent an operation that same night.

News of the crash and the type of aircraft involved come in the wake of reports that the government, through the Ministry of Defence and National Service, recently bought four Agusta Bell model 412 EP helicopters for the TPDF in somewhat controversial circumstances.

Investigations by THISDAY have established that the choppers bought are of soft-skin, civilian mode, and not suitable for specialised military operations.

A private local company, Khaisa Enterprises Limited, has since filed a 17bn/- suit against the defence ministry for breach of contract in connection with the supply of helicopters to the TPDF.

According to details of the plaint obtained by THISDAY, Khaisa Enterprises claims that the defence ministry went against a valid contract in which the company was to supply six units of COUGAR AS 532 helicopters manufactured by France’s Eurocopters company at a total cost of 125 million euros (approx. 210bn/-).

It is alleged that the Augusta Bell choppers eventually purchased for the TPDF ’’had already been rejected by the defendants (defence ministry), on the basis that the same were of inferior quality and were civilian helicopters, while the defendants required helicopters for military use.’’

It is further alleged that the defence ministry ’’purchased the helicopters at a higher cost of $9.263m each, contrary to the ones proposed by the plaintiff (Khaisa Enterprises Ltd) which were relatively cheaper at $4.7m each, thus making the nation suffer a loss of $4.563m for each helicopter purchased.’’

Our sources say the controversial military radar agent Shailesh Vithlani and his business partner were the agents used to supply the Agusta Bell helicopters to the government at vastly inflated prices.

Vithlani is currently wanted by Tanzanian authorities over perjury charges before the Kisutu Resident Magistrate’s Court in Dar es Salaam.

Meanwhile, the actual cause of the military helicopter crash in Arusha has yet to be established.

 
Tume nyingine mbili hizo zaja

Moja kuchunguza chanzo cha ajali na kuchunguza kwa nini military copter itumiwe civilian tena foreigners

Pili kuchunguza manunuzi ya ndege hizo ambazo zimekuwa inflated, na sio zilizokuwa zinahitajika na mengine
 
Hivi huyu rais Mjeshi kashaanza military spending? Mi nilifikiri ile mikogo yake iliyo U-Tube (rampant blubbering on the verge of undiplomatic warmongering about Uganda) were just one of his gazillion gaffes.

It is a good thing to see these previously "sacred military" matters being discussed in the press, watu wanamtafuta mpaka mkuu wa majeshi wamuhoji, tumetoka mbali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…