GhostRyder1
JF-Expert Member
- Aug 16, 2016
- 286
- 212
Mjomba Misifa..Kuweka kwenye mitandao ni sehemu tu ya usambazaji wa report na matamko. Report zote zinasambazwa kwa wadau wote kwa njia nyingine mbalimbali. Zinatolewa bure jwa yeyote anayehitaji. Matamko yote, ambayo ni kwa vyombo vya habari yanatolewa mbele ya vyombo vya habari. Kama umeangalia na kusikiliza taarifa za habari leo naamini utakuwa umeona kuwa Kituo kimetoa tamko kukemea mauaji yaliyofanywa dhidi ya polisi. Kituo kina vipindi vya TV na Radio. ITV Kipimajoto kila mwisho wa mwezi, na Channel 10 Kipindi cha Pambanu kila Alhamisi. Vyote hivi vina lengo la kuelimisha umma kwa ujumla, Serikali na wananchi juu ya kuzingatia misingi ya haki za binadamu. Hii ni mbali na vipindi vingine vingi vya redio ambapo Kituo kinaalikwa kuelezea kuhusu masuala ya haki za binadamu, bila kubagua ni binadamu gani haswa anayetajwa. Kama una nafasi fika ofisi zao Makao Makuu Kijitonyama, Kituo cha Msaada wa Sheria Kinondoni na Ofisi Ndogo Arusha kujua hasa kazi za Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu. Inachekesha kudhihaki umuhimu wa mtandao wakati na anayedhihaki anafanya hivyo akiwa mtandaoni.
Hii kitu ungeweza kuifupisha na ikaleta maana zaidi. Ila kwa kuwa umeamua kuifanya blogu nimeshindwa kusoma.