Mie sijui ndo ukoloni unaniathiri? Hivi mtu mzima kufikia kwa watu inakuwaje? Manake kuna wengine usiku wanapandisha maruhani utafanyaje kama haumjui? Unless ni ndugu ama rafiki wa karibu sana nadhani hata akija unapaswa umuweke hoteli.
Nijibu kiuwazi. Kuna siku rafiki yangu wa karibu sana alikuja kikazi mji nnaoishi. Akakaa hoteli akamaliza shughuli zake. Kwa sababu alikuwa anaondoka alfajiri na alifanya shopping sana kama kawaida yetu wadada nikamuambia nitamchukua aje alale kwangu ili alfajiri nimpeleke na mizigo yake stendi (taxi isingemtosha). Kabla sijamfuata akanipigia kuniambia yuko na dada mwingine ambae walizoeana hapo mkutanoni na anaona vibaya kumuacha. Nilimuambia mtu nisiemjua uzuri hawezi lala kwangu. Nilikosea?