Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
John Heche, Makamu Mwenyekiti wa Chadema Bara akizungumza kwenye mkutano wa hadhara wilayani Kyerwa Mkoani Kagera leo Mei 07, 2025.
"Leo mnaishi kwenye nchi ya asali na maziwa, watu wetu ni maskini, matibabu ni ya shida hata barabara ya kuunganisha wilaya na wilaya ndio hiyo tunatembea - kwa nchi ya tatu kwa dhahabu duniani.
Sasa tumekataa hayo mambo halafu kuna watu waliokuwa miongoni mwetu ambao tulikuwa tunazungumza nao lugha moja, leo wanasema eti kusema hivyo ni kosa. Wanataka twende kwenye uchaguzi ambao tumeenda 2019 tumenyang'anywa, tukaenda 2020 tukanyang'anywa, tukaenda 2024 tumenyang'anywa mwaka jana.
Hao watu wameenda kwenye hicho Chama na walikuwa viongozi wa Chama hiki wana miujiza gani tofauti na kutumiwa? Mimi na Lissu tumekataa kutumiwa na CCM. Mnasemaje hapo?
Sasa ipo hivi na hili niwaambie, baada ya Bunge la Ulaya jana kuwakalia kooni kwamba lazima mfanye mabadiliko, Viongozi wa dini mmewasikia wamesema lazima mabadiliko yafanyike, kila sehemu nchi hii Viongozi wa kiislamu, Kikristo na masharika wanasema lazima mabadiliko yafanyike. Mzee Warioba aliyekuwa Waziri Mkuu na Makamu wa Rais, Mzee Butiku wanasema lazima mabadiliko yafanyike. Wanataka kutumia watu waliokuwa miongoni mwetu wawasanitize serikali kwamba sasa wawaambie wanahamia chama fulani ndani ya siku mbili hizi na walikuwa viongozi humu tukashindwa uchaguzi tukiwa nao, leo wanaambiwa mkija huku mtapata viti, huo muujiza wanaupata wapi?"
Pia, Soma: Baadhi ya G-55 wakiwemo Benson Kigaila, John Mrema, Catherine Ruge na Salum Mwalimu wajiondoa CHADEMA
"Leo mnaishi kwenye nchi ya asali na maziwa, watu wetu ni maskini, matibabu ni ya shida hata barabara ya kuunganisha wilaya na wilaya ndio hiyo tunatembea - kwa nchi ya tatu kwa dhahabu duniani.
Sasa tumekataa hayo mambo halafu kuna watu waliokuwa miongoni mwetu ambao tulikuwa tunazungumza nao lugha moja, leo wanasema eti kusema hivyo ni kosa. Wanataka twende kwenye uchaguzi ambao tumeenda 2019 tumenyang'anywa, tukaenda 2020 tukanyang'anywa, tukaenda 2024 tumenyang'anywa mwaka jana.
Hao watu wameenda kwenye hicho Chama na walikuwa viongozi wa Chama hiki wana miujiza gani tofauti na kutumiwa? Mimi na Lissu tumekataa kutumiwa na CCM. Mnasemaje hapo?
Sasa ipo hivi na hili niwaambie, baada ya Bunge la Ulaya jana kuwakalia kooni kwamba lazima mfanye mabadiliko, Viongozi wa dini mmewasikia wamesema lazima mabadiliko yafanyike, kila sehemu nchi hii Viongozi wa kiislamu, Kikristo na masharika wanasema lazima mabadiliko yafanyike. Mzee Warioba aliyekuwa Waziri Mkuu na Makamu wa Rais, Mzee Butiku wanasema lazima mabadiliko yafanyike. Wanataka kutumia watu waliokuwa miongoni mwetu wawasanitize serikali kwamba sasa wawaambie wanahamia chama fulani ndani ya siku mbili hizi na walikuwa viongozi humu tukashindwa uchaguzi tukiwa nao, leo wanaambiwa mkija huku mtapata viti, huo muujiza wanaupata wapi?"
Pia, Soma: Baadhi ya G-55 wakiwemo Benson Kigaila, John Mrema, Catherine Ruge na Salum Mwalimu wajiondoa CHADEMA