PreGE2025 Heche John: Aliyempiga Siglada (BAWACHA) achukuliwe hatua za kisheria

PreGE2025 Heche John: Aliyempiga Siglada (BAWACHA) achukuliwe hatua za kisheria

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,499
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema, Heche John, amesema kuwa yule aliyehusika kumpiga Katibu Mwenenzi wa Baraza la Wanawake wa Chadema (BAWACHA) Taifa, Sigrada Mligo, achukuliwe hatua za kisheria.

Pia, Soma: Ghasia Ndani ya CHADEMA: Mwenezi wa BAWACHA Taifa ashambuliwa na Walinzi wa Heche

Heche John ameyasema hayo katika mahojiano na Elolama FM akieleza juu ya tukio la kupigwa kwa kiongozi huyo Machi 25, 2025, mjini Njombe.

 
Heche ameongea vizuri lakini ameharibu hapo mwishoni. Hivi haamini kuwa Sigrada alipigwa?

Amandla..
 
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema, Heche John, amesema kuwa yule aliyehusika kumpiga Katibu Mwenenzi wa Baraza la Wanawake wa Chadema (BAWACHA) Taifa, Sigrada Mligo, achukuliwe hatua za kisheria.

Pia, Soma: Ghasia Ndani ya CHADEMA: Mwenezi wa BAWACHA Taifa ashambuliwa na Walinzi wa Heche

Heche John ameyasema hayo katika mahojiano na Elolama FM akieleza juu ya tukio la kupigwa kwa kiongozi huyo Machi 25, 2025, mjini Njombe.

Pumba tupu
 
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema, Heche John, amesema kuwa yule aliyehusika kumpiga Katibu Mwenenzi wa Baraza la Wanawake wa Chadema (BAWACHA) Taifa, Sigrada Mligo, achukuliwe hatua za kisheria.

Pia, Soma: Ghasia Ndani ya CHADEMA: Mwenezi wa BAWACHA Taifa ashambuliwa na Walinzi wa Heche

Heche John ameyasema hayo katika mahojiano na Elolama FM akieleza juu ya tukio la kupigwa kwa kiongozi huyo Machi 25, 2025, mjini Njombe.

Huhitaji kulialia kiwango hicho ni kutafuta huruma??
Pole kwa hilo na punguza munkari yafanyiwe kazi.
 
Heche ameongea vizuri lakini ameharibu hapo mwishoni. Hivi haamini kuwa Sigrada alipigwa?

Amandla..
Heche alikuwepo kwenye tukio na si Heche tu hata viongozi wengine kwahiyo hao ndiyo mashuda wazuri wakumtea swala hilo likienda mahakama na siyo hao POLISI waliompeka nyumbani kwake.Hili swala ni la kisiasa na Nadhani huyu Sigranda alikuwa anajua ni nini hatima yake ndani ya Chama kwahiyo akawa anatafuta tension ili ionekane kuwa hata maamuzi yakitoka ionekane Anaonewa kwakuwa yeye ni timu Pinzani na mwenyekiti wa sasa. Kikubwa Lisu afanye kikao cha dharula ndani ya chama, cha kuhakikisha anaponya majeraha ya uchaguzi mkuu na kunapatikana muafaka kwa team zote mbili kwa sababu team mbowe wanaona kama wanabaguliwa na kuchukiwa ndani ya Chama ni wengi wao wanaonekana kama walichukua fedha kama wenje. kikubwa kikao cha upatanisho na maridhiano kinatakiwa kifanyike nchi nzima hasa Jimbo la kaskazini pamoja na wenyeviti woto wa mikoa na majembo. Ingawa kikao hicho kitakuwa siyo rasmi na hakipo kwenye katiba.Kinapaswa kiratibiwe vizuri na ili kiweze kuleta manufaa badala yakuongeza majeraha. Tundu Lisu aelewe mchuano wa uchaguzi ulikuwa mkali sana na uliacha maumivu makali sana kwa upande ulioshindwa kwa sababu haukutegemea kushindwa.
 
Heche alikuwepo kwenye tukio na si Heche tu hata viongozi wengine kwahiyo hao ndiyo mashuda wazuri wakumtea swala hilo likienda mahakama na siyo hao POLISI waliompeka nyumbani kwake.
Hao watakuwa mashuhuda wa mlinzi na sio wa Sigrida kama polisi watamfungulia Noel mashtaka. Heche na hao viongozi wengine inaelekea hawako neutral kwenye suala maana wanaonekana tayari wana matatizo na Sigrida. Huwezi kuwaita mashuhuda wazuri kwa sababu hiyo. Polisi waliokuwa kwenye tukio la kupigwa Sigrida wataaminiwa zaidi na Mahakama maana kesi ni kupigwa kwa Sigrida sio yaliyotokea kwenye kikao.
Hili swala ni la kisiasa na Nadhani huyu Sigranda alikuwa anajua ni nini hatima yake ndani ya Chama kwahiyo akawa anatafuta tension ili ionekane kuwa hata maamuzi yakitoka ionekane Anaonewa kwakuwa yeye ni timu Pinzani na mwenyekiti wa sasa.
Kama tayari mmeisha mhukumu na mna mpango wa kumshughulikia kabla hata ya kumsikiliza kwa sababu tu ni Team Mbowe basi yuko sahihi kuona kuwa anaonewa na uongozi uliopo. Na kama unachosema ni kweli wenye tatizo ni Team Lissu kwa sababu wanaendekeza visasi badala ya kujaribu kuwavuta wale ambao walikuwa upande wa pili.
Kikubwa Lisu afanye kikao cha dharula ndani ya chama, cha kuhakikisha anaponya majeraha ya uchaguzi mkuu na kunapatikana muafaka kwa team zote mbili kwa sababu team mbowe wanaona kama wanabaguliwa na kuchukiwa ndani ya Chama ni wengi wao wanaonekana kama walichukua fedha kama wenje.
Kikao cha kuponya majeraha cha nini kama tayari mnawatuhumu kuwa walihongwa? Hilo la Wenje mpaka sasa hivi hamjatoa ushahidi wowote kuwa alihongwa ingawa mnazo taarifa zote.
kikubwa kikao cha upatanisho na maridhiano kinatakiwa kifanyike nchi nzima hasa Jimbo la kaskazini pamoja na wenyeviti woto wa mikoa na majembo. Ingawa kikao hicho kitakuwa siyo rasmi na hakipo kwenye katiba.Kinapaswa kiratibiwe vizuri na ili kiweze kuleta manufaa badala yakuongeza majeraha. Tundu Lisu aelewe mchuano wa uchaguzi ulikuwa mkali sana na uliacha maumivu makali sana kwa upande ulioshindwa kwa sababu haukutegemea kushindwa.
Unajichanganya. Hicho kikao hakitasaidia kitu kama hamtakubali ukweli kuwa waliompinga Lissu walikuwa na haki ya kufanya hivyo na hivyo wapewe heshima zao kama wanachama wengine. Kuwabagua na kuwafanyia fujo hakutatibu hayo majeraha. Wanapolalamika kuwa wanaonewa wasikilizwe na zichukuliwe hatua za dhati za kuzuia upuuzi huo. CDM bado inawahitaji sana.

Amandla...
 
Heche alikuwepo kwenye tukio na si Heche tu hata viongozi wengine kwahiyo hao ndiyo mashuda wazuri wakumtea swala hilo likienda mahakama na siyo hao POLISI waliompeka nyumbani kwake.Hili swala ni la kisiasa na Nadhani huyu Sigranda alikuwa anajua ni nini hatima yake ndani ya Chama kwahiyo akawa anatafuta tension ili ionekane kuwa hata maamuzi yakitoka ionekane Anaonewa kwakuwa yeye ni timu Pinzani na mwenyekiti wa sasa. Kikubwa Lisu afanye kikao cha dharula ndani ya chama, cha kuhakikisha anaponya majeraha ya uchaguzi mkuu na kunapatikana muafaka kwa team zote mbili kwa sababu team mbowe wanaona kama wanabaguliwa na kuchukiwa ndani ya Chama ni wengi wao wanaonekana kama walichukua fedha kama wenje. kikubwa kikao cha upatanisho na maridhiano kinatakiwa kifanyike nchi nzima hasa Jimbo la kaskazini pamoja na wenyeviti woto wa mikoa na majembo. Ingawa kikao hicho kitakuwa siyo rasmi na hakipo kwenye katiba.Kinapaswa kiratibiwe vizuri na ili kiweze kuleta manufaa badala yakuongeza majeraha. Tundu Lisu aelewe mchuano wa uchaguzi ulikuwa mkali sana na uliacha maumivu makali sana kwa upande ulioshindwa kwa sababu haukutegemea kushindwa.
Mbona unarudia yale yale?

Amandla...
 
Mbona
Hao watakuwa mashuhuda wa mlinzi na sio wa Sigrida kama polisi watamfungulia Noel mashtaka. Heche na hao viongozi wengine inaelekea hawako neutral kwenye suala maana wanaonekana tayari wana matatizo na Sigrida. Huwezi kuwaita mashuhuda wazuri kwa sababu hiyo. Polisi waliokuwa kwenye tukio la kupigwa Sigrida wataaminiwa zaidi na Mahakama maana kesi ni kupigwa kwa Sigrida sio yaliyotokea kwenye kikao.

Kama tayari mmeisha mhukumu na mna mpango wa kumshughulikia kabla hata ya kumsikiliza kwa sababu tu ni Team Mbowe basi yuko sahihi kuona kuwa anaonewa na uongozi uliopo. Na kama unachosema ni kweli wenye tatizo ni Team Lissu kwa sababu wanaendekeza visasi badala ya kujaribu kuwavuta wale ambao walikuwa upande wa pili.

Kikao cha kuponya majeraha cha nini kama tayari mnawatuhumu kuwa walihongwa? Hilo la Wenje mpaka sasa hivi hamjatoa ushahidi wowote kuwa alihongwa ingawa mnazo taarifa zote.

Unajichanganya. Hicho kikao hakitasaidia kitu kama hamtakubali ukweli kuwa waliompinga Lissu walikuwa na haki ya kufanya hivyo na hivyo wapewe heshima zao kama wanachama wengine. Kuwabagua na kuwafanyia fujo hakutatibu hayo majeraha. Wanapolalamika kuwa wanaonewa wasikilizwe na zichukuliwe hatua za dhati za kuzuia upuuzi huo. CDM bado inawahitaji sana.

Amandla...
Mimi nadhani kwa swala hili kwasababu lipo chini ya vyombo vya usalama kwa ajili ya uchunguzi tuliache wahusika wafanye kazi yao ila mimi kwa upande wangu sioni afya ya hicho chama mivutano ya ndani ya timu mbowe na timu Lisu. Hasa kaa upande wa bawacha hawahaminiki kabisa ktk timu ,wenyeviti wa mi,, ikoa na wa kanda karibu wote walikuwa team mbowe, ili kuweza kujinga kuaminiana lazima kufanyike kitu la sivyo kutakua na tension kubwa ya pande mbili ndani ya chama na hii itaweza kusaidia mahasimu wao wakubwa kutumia mianya hiyo kukiharibu chama hasa kipindi hiki cha uchaguzi. Mwa sababu inaonekana team mbowe tayari ilikuwa na mikakati yao waliokuwa wamekwisha panga kabla ya Mwenyekiti Lisu kuingia bila wao kutegemea na mikakati hiyo Lisu na kundi lake wanaijua kwahiyo wanacheza mchezo wa paka na panya ukiingia kwenye mtego unaliwa kichwa. Hii haitaleta maendeleo ndani ya chama. Kwa mfano swala la No reform No election pamoja ya hili swala kuanzishwa tangu kiipindi Cha mwenyekiti Mbowe lakini wao hawakuwa wamelivalia njuga kama kipindi cha Lisu na team mbowe inaonyesha walikuwa wamejipanga kugombea uhunge na udiwani hata kama hakuna reform, ila uongozi wa mwenyekiti Lisu unaweka ngumu kabisa kuhusu swala la uchaguzi bila reform hili ni tatizo ndani ya chama na ikiifika kipindi cha uchaguzi unaweza kushangaa kukawa na wagombea wengi wa CDM ambao hawakupita ktk taratibu zinazo eleweka na wengi wao wakashinda hata bila kufanya kampeni.
 
Hela za mama Abdul mlizokula ili mu hujumu chama kwa kumchagua Mbowe na mkashindwa zitawatesa sana!! Salama yenu ni kutubu na kumrudishia mama Abdul hela yake!🤪🤪
Sijawahi sikia hela ya sadakalawe ikarudishwa!
 
Mbona

Mimi nadhani kwa swala hili kwasababu lipo chini ya vyombo vya usalama kwa ajili ya uchunguzi tuliache wahusika wafanye kazi yao
Hili suala linakiathiri kuliko unavyofikiria. CDM ilipaswa kulizima mapema ili kuzuia CCM kulitumia kisiasa. Na tayari wanalitumia kupakazia chama kizima wakati nyie mnajifanya hamuoni.
ila mimi kwa upande wangu sioni afya ya hicho chama mivutano ya ndani ya timu mbowe na timu Lisu.
Hamna mvutano maana kila mtu anajua Team Lissu ilishinda uchaguzi. Hao unaowaita Team Mbowe hawana mamlaka yeyote ndani ya Chadema. Ni wajibu wa Team Lissu kuwaonyesha kuwa pamoja na wao kushinda uchaguzi, wale walioshindwa bado wana nafasi na heshima katika chama. Kuwananga ni siasa mbovu.
Hasa kaa upande wa bawacha hawahaminiki kabisa ktk timu ,wenyeviti wa mi,, ikoa na wa kanda karibu wote walikuwa team mbowe, ili kuweza kujinga kuaminiana lazima kufanyike kitu la sivyo kutakua na tension kubwa ya pande mbili ndani ya chama na hii itaweza kusaidia mahasimu wao wakubwa kutumia mianya hiyo kukiharibu chama hasa kipindi hiki cha uchaguzi.
Tangu lini kuwa Team Mbowe imekuwa dhambi? Mlitaka wote wawe Team Lissu? Kama kigezo cha kumuamini mtu ni kumkubali Lissu basi tatizo ni kubwa. Wanaokiharibu chama chenu sio CCM bali ni wale wanaotaka kutumia nafasi zao au ukaribu wao na viongozi kulipa visasi. Sagrida sio mnafik. Anachotaka ni heshima wanayostahili kama viongozi. Aidha, anakataa kubagaza mchango mkubwa wa Mbowe kwa chama chake. Kufanya hivyo sio kukataa kuutambua uongozi wa sasa.
Mwa sababu inaonekana team mbowe tayari ilikuwa na mikakati yao waliokuwa wamekwisha panga kabla ya Mwenyekiti Lisu kuingia bila wao kutegemea na mikakati hiyo Lisu na kundi lake wanaijua kwahiyo wanacheza mchezo wa paka na panya ukiingia kwenye mtego unaliwa kichwa.
Kama mna imani hiyo hapatakuwa na kuponya vidonda. Hivi unadhani Mbowe angetaka kuendelea kama Mwenyekiti angeshindwa? Amesaidia kufanikisha uchaguzi uliokuwa huru na haki na amempisha Mwenyekiti mpya aongoze chama. Tofauti na unavyosema, ni Team Lissu ndio inaelekea haikutegemea kushinda maana wanajua ni vigumu wa viongozi wa vyama vya siasa nyumbani kukubali kushindwa. Walijua Mbowe atatumia hata mbinu chafu kubaki madarakani. Alipoendesha uchaguzi ambao kila mtu ameusifia na kukubali kushindwa iliwastua. Kinachosikitisha ni kuwa badala ya kuhakikisha chama kinabakia kimoja, baadhi yao wanaendekeza siasa za visasi na kuchafuana.
Hii haitaleta maendeleo ndani ya chama. Kwa mfano swala la No reform No election pamoja ya hili swala kuanzishwa tangu kiipindi Cha mwenyekiti Mbowe lakini wao hawakuwa wamelivalia njuga kama kipindi cha Lisu
Approach ya Mbowe na Lissu ni tofauti. Hata hivyo hamna kampeni ya chama ambayo Mbowe hakujihusisha kikamilifu.
na team mbowe inaonyesha walikuwa wamejipanga kugombea uhunge na udiwani hata kama hakuna reform, ila uongozi wa mwenyekiti Lisu unaweka ngumu kabisa kuhusu swala la uchaguzi bila reform hili ni tatizo ndani ya chama na ikiifika kipindi cha uchaguzi unaweza kushangaa kukawa na wagombea wengi wa CDM ambao hawakupita ktk taratibu zinazo eleweka na wengi wao wakashinda hata bila kufanya kampeni.
Sio dhambi kujitayarisha kugombea ili kama uongozi ukibadili mawazo au mabadiliko ya maana yakifanyika wawe katika nafasi nzuri ya kushinda nafasi za kutosha. Ni kuwaonea kuwashutumu kuwa watakuwa tayari kutumika ili mradi tu wapate ushindi. Mtazamo huo ndio unaharibia chama chenu. CCM haishindwi kuweka mtu ambae hata sio mwanachama wa CDM kugombea. Aidha, wanaweza kuhakikisha wagombea kutoka vyama vingine vitakavyoshiriki kwenye uchaguzi vinashinda. Kama ilivyofanywa kwa Chaumma. Vyama kama CUF, NCCR Mageuzi hata ACT-WAZALENDO havitajivunga nafasi hiyo ikitokea.

Amandla...
 
Hili suala linakiathiri kuliko unavyofikiria. CDM ilipaswa kulizima mapema ili kuzuia CCM kulitumia kisiasa. Na tayari wanalitumia kupakazia chama kizima wakati nyie mnajifanya hamuoni.

Hamna mvutano maana kila mtu anajua Team Lissu ilishinda uchaguzi. Hao unaowaita Team Mbowe hawana mamlaka yeyote ndani ya Chadema. Ni wajibu wa Team Lissu kuwaonyesha kuwa pamoja na wao kushinda uchaguzi, wale walioshindwa bado wana nafasi na heshima katika chama. Kuwananga ni siasa mbovu.

Tangu lini kuwa Team Mbowe imekuwa dhambi? Mlitaka wote wawe Team Lissu? Kama kigezo cha kumuamini mtu ni kumkubali Lissu basi tatizo ni kubwa. Wanaokiharibu chama chenu sio CCM bali ni wale wanaotaka kutumia nafasi zao au ukaribu wao na viongozi kulipa visasi. Sagrida sio mnafik. Anachotaka ni heshima wanayostahili kama viongozi. Aidha, anakataa kubagaza mchango mkubwa wa Mbowe kwa chama chake. Kufanya hivyo sio kukataa kuutambua uongozi wa sasa.

Kama mna imani hiyo hapatakuwa na kuponya vidonda. Hivi unadhani Mbowe angetaka kuendelea kama Mwenyekiti angeshindwa? Amesaidia kufanikisha uchaguzi uliokuwa huru na haki na amempisha Mwenyekiti mpya aongoze chama. Tofauti na unavyosema, ni Team Lissu ndio inaelekea haikutegemea kushinda maana wanajua ni vigumu wa viongozi wa vyama vya siasa nyumbani kukubali kushindwa. Walijua Mbowe atatumia hata mbinu chafu kubaki madarakani. Alipoendesha uchaguzi ambao kila mtu ameusifia na kukubali kushindwa iliwastua. Kinachosikitisha ni kuwa badala ya kuhakikisha chama kinabakia kimoja, baadhi yao wanaendekeza siasa za visasi na kuchafuana.

Approach ya Mbowe na Lissu ni tofauti. Hata hivyo hamna kampeni ya chama ambayo Mbowe hakujihusisha kikamilifu.

Sio dhambi kujitayarisha kugombea ili kama uongozi ukibadili mawazo au mabadiliko ya maana yakifanyika wawe katika nafasi nzuri ya kushinda nafasi za kutosha. Ni kuwaonea kuwashutumu kuwa watakuwa tayari kutumika ili mradi tu wapate ushindi. Mtazamo huo ndio unaharibia chama chenu. CCM haishindwi kuweka mtu ambae hata sio mwanachama wa CDM kugombea. Aidha, wanaweza kuhakikisha wagombea kutoka vyama vingine vitakavyoshiriki kwenye uchaguzi vinashinda. Kama ilivyofanywa kwa Chaumma. Vyama kama CUF, NCCR Mageuzi hata ACT-WAZALENDO havitajivunga nafasi hiyo ikitokea.

Amandla...
Ok nikushukuru kwa mda wako na uchambuzi wako umenisaidia kwa namna fulani ubarikiwe sana
 
Ok nikushukuru kwa mda wako na uchambuzi wako umenisaidia kwa namna fulani ubarikiwe sana
Usisahau kuwa Lissu alimpigia debe sana na kwa wazi mshindani wake Sharifa? Alipaswa kuhakikisha kuwa anapewa heshima anayostahili na hahujumiwi kama ambavyo yeye anavyotaka wale ambao walikuwa upande wa pili wamheshimu. Bawacha ni nguzo muhimu ya CDM na wakiisononesha itakula kwao. Kuna hasara gani kwa Makamu Mwenyekiti kwenda hospitali kumjulia hali Katibu Mwenezi wa Bawacha? Jambo hilo lingepunguza sana tension unayoisema kuliko watu kushinda mtandaoni kumchafua Sigrada.

Amandla...
 
Back
Top Bottom