DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Makamu Mwenyekiti wa CHADEMBA Bara, John Heche hii leo afika Mahakamani kwenye kesi iliyofunguliwa na aliyekuwa Makamu Mwenyekiti Zanzibar kwa miaka zaidi ya kumi, Said Issa Mohamed na wenzake wawili (2) dhidi ya Bodi ya wadhamini wa CHADEMA na Katibu Mkuu wa CHADEMA
"Ni wazi kwamba CCM hawawezi kushindana na sisi tena, walimkatama Mwenyekiti wetu(Tundu Lissu), wameunda vyama vibaraka vya kutumia, walitumia baadhi ya watu tuliokuwa nao kujaribu kupasua uongozi wetu, lakini bado wanataka watumie Mahakama kuzuia shughuli halali za kwetu za kisiasa, sasa hii ni hatua ya mwisho kabisa ya watu walioshindwa kufanya siasa. Ukweli ni kwamba tunaungwa mkono sana kuliko kipindi chochote na nyie mnajua”
Heche asisitiza kuwa hawana imani na Jaji anayeendesha kesi hiyo na kumtaka ajiondoe, awataka Wanachadema kuendelea na shughuli za kisiasa pasipo kuhusisha mali za chama.
"Ni wazi kwamba CCM hawawezi kushindana na sisi tena, walimkatama Mwenyekiti wetu(Tundu Lissu), wameunda vyama vibaraka vya kutumia, walitumia baadhi ya watu tuliokuwa nao kujaribu kupasua uongozi wetu, lakini bado wanataka watumie Mahakama kuzuia shughuli halali za kwetu za kisiasa, sasa hii ni hatua ya mwisho kabisa ya watu walioshindwa kufanya siasa. Ukweli ni kwamba tunaungwa mkono sana kuliko kipindi chochote na nyie mnajua”
Heche asisitiza kuwa hawana imani na Jaji anayeendesha kesi hiyo na kumtaka ajiondoe, awataka Wanachadema kuendelea na shughuli za kisiasa pasipo kuhusisha mali za chama.