AmKATRINA
JF-Expert Member
- Jul 27, 2012
- 414
- 366
Mimi nakumbuka kabla dada yangu wa kwanza kuzaliwa hajaolewa, yeye ndie tulikuwa tunamuonea kwenye kupika kila siku.
Dada yangu alikuwa hana jinsi maana sisi ndio tulikuwa wadogo zake. Ila akimaliza kupika sasa, hivyo vyombo vichafu mpaka juu ya dari....ila mwisho wa siku tunaelewana na kupiga story.
Siku ya harusi yake tulilia balaa...akatutania kuwa atakuwa anakuja kutupikia siku mojamoja
Pia nakumbuka tulikuwa tunaishi na kaka etu mtoto wa baba mkubwa, yaani kipindi hajaoa, ole wako akukute umesimama na mwanaume, wote mnakula makofi anakubeba juu juu mashtaka mpaka nyumbani. Nashukuru sahv wote tumeolewa na kaka zetu wameoa..
Huwa kwenye group la wasap tunakumbushana ya nyuma tunaishia kucheka tu.
Wewe mdau unakumbuka nini kabla hujaoa au hujaolewa au kabla ndugu zako hwajaoa au kuolewa?
Maana lazima kuna wababe, watemi, vilizi, vimbelembele, wakuonewa n.k
Dada yangu alikuwa hana jinsi maana sisi ndio tulikuwa wadogo zake. Ila akimaliza kupika sasa, hivyo vyombo vichafu mpaka juu ya dari....ila mwisho wa siku tunaelewana na kupiga story.
Siku ya harusi yake tulilia balaa...akatutania kuwa atakuwa anakuja kutupikia siku mojamoja
Pia nakumbuka tulikuwa tunaishi na kaka etu mtoto wa baba mkubwa, yaani kipindi hajaoa, ole wako akukute umesimama na mwanaume, wote mnakula makofi anakubeba juu juu mashtaka mpaka nyumbani. Nashukuru sahv wote tumeolewa na kaka zetu wameoa..
Huwa kwenye group la wasap tunakumbushana ya nyuma tunaishia kucheka tu.
Wewe mdau unakumbuka nini kabla hujaoa au hujaolewa au kabla ndugu zako hwajaoa au kuolewa?
Maana lazima kuna wababe, watemi, vilizi, vimbelembele, wakuonewa n.k