mizambwa
JF-Expert Member
- Oct 8, 2008
- 4,422
- 1,790
Ndugu wadau:
Tukiwa tunatimiza miaka 13 toka kuondokewa na Baba wa Taifa letu Tanzania, ambaye alikuwa Rais wa kwanza wa JMT.
Kifo chake si kwamba kilituhudhunisha Watanzania tu bali Afrika na Dunia ilihudhunishwa.
Kama ilivyo kawaida Binadamu siyo Malaika, katika maisha yetu tunatenda mazuri na pia mabaya tunayatenda. Hivyo zote ni sifa za Binadamu katika maisha hapa Duniani
Je, ni mambo gani ambayo tunamkumbuka, mazuri na mabaya????????
Mfano mimi binafsi namkumbuka "kama mwanamichezo namba moja na mpenda utamaduni" Enzi za utawala wake kulikuwa na mwamko katika timu za mpira mbalimbali, mashirika ya umma yalikuwa na timu.
Timu zetu ziliweza kuingia fainali ya Afrika.
Hivyo ni jitihada za uongozi wake zilisababisha haya mafanikio.
Natoa hoja.
MIZAMBWA
NABII MTARAJIWA!!!