Haya yataendelea mpaka lini?

Haya yataendelea mpaka lini?

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
98,087
Reaction score
143,300
Hivi sisi ni binadamu kweli? Hebu angalieni huyu "mtuhumiwa" wa wizi akiponea chupuchupu kubanikwa.....

j18.JPG


Cheki hii njemba inavyoonyesha kufurahishwa na kinachoendelea...
j16.JPG


Kwa mujibu wa Michuzi huyo bakoa ni askari kanzu...kibaka "mtuhumiwa" naona kapata second wind na kajichomoa kutoka kwenye mbaniko..
j15.JPG


Mungu mkubwa (kama unamwamini)....kibaka "mtuhumiwa" kanyanyuka..
j13.JPG


Poooow! Yuko chali....hana nguvu kabisa baada ya kisago kilichotolewa na "binadamu"...
j10.JPG


Anajaribu tena kunyanyuka....angalia hao "binadamu" wanavyomwangalia...sijui walikuwa wanamwambia nini?
j8.JPG


Anapanda kwenye gari...sijui wanampeleka wapi? Polisi?
j4.JPG


Kipigo cha "binadamu" si mchezo. Hata kukaa hawezi...yuko kifudifudi...sijui kaishiwa nguvu au nini...me I dunno...
j3.JPG


Sasa najiuliza hivi sisi tunathamini vitu au mambo gani hapa duniani? Vibaka watuhumiwa wanabanikwa. Mafisadi papa na nyangumi wanakula maisha kwenye viyoyozi...

Picha kwa hisani ya Michuzi: http://www.issamichuzi.blogspot.com/
 
....Mpaka pale adhabu kama hizo zitakapowafikia mafisadi papa na nyangumi. Na pale elimu ya form 4 ndiyo itakayokuwa elimu ya msingi!!
 
Jamii ijuayo uwiano thabiti kati ya dharau, ubinafsi, chuki na ustaarab dhidi ya jamii nyingine na baina ya watu wake ni jamii yenye maendeleo. Isiyojua ni dumazi. SDD1-09.
 
Yataendelea mpaka watu watakapojua wajibu wao... kufanya kazi halali ndio ule!!!
 
Yataendelea mpaka watu watakapojua wajibu wao... kufanya kazi halali ndio ule!!!

Sasa kwa nini yanaishia (adhabu) kwa vibaka "watuhumiwa" wenye njaa za kweli na si kwa mafisadi wasio na njaa, huruma, n.k.?
 
steveD said:
....Mpaka pale adhabu kama hizo zitakapowafikia mafisadi papa na nyangumi. Na pale elimu ya form 4 ndiyo itakayokuwa elimu ya msingi!!

steveD,

..kuna uwezekano mkubwa kabisa kwamba kiwango cha elimu ya form 4 si kama unavyoijua wewe.

..hali ya elimu ni mbaya na ya kukatisha tamaa, haswa katika hizi sekondari za kata.
 
Sasa kwa nini yanaishia (adhabu) kwa vibaka "watuhumiwa" wenye njaa za kweli na si kwa mafisadi wasio na njaa, huruma, n.k.?

Ndugu yangu msuli mdogo... ndoto ni kuandibu mwovu yeyote, lakini huyo RA tutampata wapi tumchape bakora na kumzungushia tairi wakati analindwa na umeme, computer, bunduki, watu na mbwa???

Lakini kwa trend tunayoenda... hata huko tutafika tu, we hujasikia watu na kazi zao wanauawa kimtindo bila hata kupokwa penseli??

Tanzania tumebaki na amani picha!!!
 
Nyani Ngabu,
Kweli mkuu hata mimi sizioni picha.. kiingereza chake sikijui.
 
steveD,

..kuna uwezekano mkubwa kabisa kwamba kiwango cha elimu ya form 4 si kama unavyoijua wewe.

..hali ya elimu ni mbaya na ya kukatisha tamaa, haswa katika hizi sekondari za kata.

Joka, je hiki kiwango cha elimu kimepanda au kimeshuka? Kama kimeshuka kama unavyoashiria, je ni bora form 6 ndiyo tufanye elimu ya msingi? (pamoja na kwamba nako ni kama ndoto tu vile)
 
Ndugu yangu msuli mdogo... ndoto ni kuandibu mwovu yeyote, lakini huyo RA tutampata wapi tumchape bakora na kumzungushia tairi wakati analindwa na umeme, computer, bunduki, watu na mbwa???

Lakini kwa trend tunayoenda... hata huko tutafika tu, we hujasikia watu na kazi zao wanauawa kimtindo bila hata kupokwa penseli??

Tanzania tumebaki na amani picha!!!

Statement of the Month!!

--- Mioyoni wananchi waliowengi wako kwenye vita na hali ya maisha!!
 
Nadhani hizi ni frustration za watu tu! Maisha magumu, kodi za nyumba kupanda, bili za umeme, etc. frustation zao wanamalizia kwa namna hii.
 
Sasa kwa nini yanaishia (adhabu) kwa vibaka "watuhumiwa" wenye njaa za kweli na si kwa mafisadi wasio na njaa, huruma, n.k.?

NN, mafisadi wanalindwa na vyombo vya dola. Vinginevyo wote hawa mafisadi akina Mkapa, Rostam, Chenge, Makamba, Idrissa Rashid, Jeetu, Manji, Subhash, Mkono, Mzindakaya, Yona, Mramba, Mattaka na wengi wengineo walitakiwa wawe lupango lakini bado wanapeta uraiani. Watanzania wangekuwa na uwezo wangewatendea hawa kama walivyomtenda huyo kibaka. Kumbuka wale vijana waliotiwa ndani kwa kumzomea tu fisadi Mkapa.
 
Huo ni ugumu wa maisha uliowapata Watanzania walala hoi. Huyu kijana ni njaa tuu ndiyo iliyomtuma kuiba hiyo TV na bila shaka thamani ya hiyo TV ni shs 200,000 tu.

Watanzania kama kweli tuna hasira ya kuwa na maisha magumu ambayo yamesababishwa na mafisadi kwa kiwango kikubwa kwanini tusichukue bakora, virungu, mapanga, mishale, bunduki nk tukwawavamia mafisadi na kuwapa kipondo cha kisawasawa?.
 
Back
Top Bottom