Bosi Michembe
JF-Expert Member
- Jun 24, 2011
- 271
- 87
Wewe huamini vitu visivyoonekana? Kwa Mfano Upepo unaweza kuona? mbona unamini kama upepo upo?
Usichanganye upepo ambayo ni force iko wazi na habari za mungu au malaika hapa hoja haipo
kuna viumbe mungu ameviweka humu humu duniani tunaishi navyo hatuviwezi kuviona lakini hivyo viumbe vinatuona
Nionyeshe mungu yuko wapi from there ntamuuliza kwanini anafichaficha vitu na haelewekieleweki na sio muwazi.
wewe kwani huna Dini?Mkristo au ni muislam? unaamini kuwa iko siku utakufa? Je Umesha wahi kuona kifo kwa macho yako?kama una amini iko siku utakufa basi amini kuna Mwenyeezi Mungu ,Majini na malaika na amini ipo siku ya mwisho siku ya hukumu amini kuna moto wajahanamu na kuna pepo acha usingizi wako huo.
Mi ni Muafrika nikuulize wewe na hilo liko wazi msamiati wa dini hauko kichwani mwangu. Kila kitu kinachoishi hufikia mwisho wa maisha yake kama ilivyo kwako kwa kuku, mbuzi, sungura vyote vifo na hakuna baada ya hapo. Hizo stori za jehanamu na majini watishe wengine mkuu wenye uelewa kama wako. Nipe ramani ya huko jehanmu kama kupo kama sio stori mlizokaririshwa na viongozi wenu wa dini.. Hukumu ya nini tena? kwa kosa gani?? Huyo mungu kama yupo atakuwa na matatizo makubwa sana ya kisaikolojia aisee why create something you cannot control afu mwisho wa siku you know it's end.. JIPANGE..
.