Hawa tembo maliasili mnawaona Mvomero?

Hawa tembo maliasili mnawaona Mvomero?

Dumishamila

Member
Joined
Nov 5, 2018
Posts
40
Reaction score
30
Nianze kwa kuwasalimu.
Kuna tembo ambao wanaozunguka katika kijiji vya Wami Luhindo kitongoji Majichumvi na vingine wilaya ya Mvomero. Wanaharibu mazao ya watu na wanaweza kuumiza wananchi. Afisa maliasili mpo tu mnaridhika watu wafe au namna gani?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkisema hao tembo wametumwa na chadema mpaka ikulu itaingilia
 
Wanaharibu mazao sana. Maafisa wa maliasili walikuja eti wanajifanya kutoa elimu na wakisema eti hairuhusiwi kuua tembo na wanadai familia itakayopoteza mtu kwa kudhuriwa na tembo basi itafidiwa Tsh 1millioni. Hivi badala ya kutafuta njia ya kuwarudisha mbugani mnakuja na maneno ya kitoto hivyo. Tembo ni mali sawa lakini wanakaa mbugani. Warudisheni.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom