Katika kile kinachoonekana kama kelele za mpita njia hazimzuii mwenye nyumba kulala Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Hifadhi ya Jamii-SSRA imesema haishtushwi na kelele zinazopigwa na wafanyakazi kote nchini kuhusu sheria mpya inayopiga marufuku wafanyakazi kuchukua stahiki zao wanapostaafu hadi wafikishe miaka 55 na badala ya ke imesema tayari sheria hiyo mpya imeanza kutumika tangu Julai 20.
Taarifa iliyotolewa jana jijini Dar es Salaam na kitengo cha Mawasiliano na Uhamasishaji cha SSRA, imefafanua kuwa sheria hiyo imeshaanza kutumika na maombi mapya ya kujitoa yamesitishwa kwa kipindi cha miezi sita hadi muongozo mwingine utakapotolewa.
Ilibainisha kuwa lengo la kusitisha maombi ya kujitoa uanachama ni mamlaka na mifuko ya hifadhi ya jamii kutoa elimu kwa wadau ambao ndio wanachama wa sekta hiyo.
Taarifa hiyo ilisema wamesitisha fao la kujitoa si kwa sababu ya serikali au mifuko ya hifadhi kufilisika kama baadhi ya watu wanavyodai bali inalenga kuboresha maslahi ya wanachama.
Tunapenda kuwahakikishia wanachama kuwa mifuko ya hifadhi ya jamii ni thabiti na michango yote ya wanachama iko salama.
Tunawaomba wanachama na wadau wote wa sekta ya Hifadhi ya Jamii kuwa na utulivu mchakato huu ukiwa unaendelea kwa lengo la kulinda na kutetea maslahi ya wanachama, ilisema.
Source:Tanzania Daima
Mkuu mimi naona tunawaonea SSRA, Kwani wao wanatakeleza sheria iliyotungwa na wawakilishi wetu! Tuwe makini kuachagua wabunge, Tukiendelea kuchagua watu wanapitisha na kuunga mkono 100/100 matokeo yake ndiyo haya Mkuu!