Hawa Ndiyo Wauza Madawa ya Kulevya Walioitikisa Dunia

emma115

Senior Member
Apr 28, 2012
135
167
Labda ulikuwa miongoni mwa watu waliosikia taarifa ya kukamatwa kwa muuza madawa ya kulevya nchini Mexico, Joaquín Guzmán Loera AKA “El Chapo Guzmán”, na ukajiuliza kuhusu wauzaji madawa ya kulevya ambao waliwahi kutokea katika dunia hii.

Wapo wengi ambao walikuwa wauzaji wa madawa ya kulevya, mabilionea ambao mwisho wao ulikuwa mbaya kama Pablo Escobar. Kama ulikuwa huwajui, hii hapa chini ni orodha ya wauzaji madawa ya kulevya hatari ambao wamewahi kuwepo katika dunia hii mpaka sasa.



1000509261001_2088156125001_Frank-Lucas-Superfly.jpg


FRANK LUCAS AKA Superfly
Unapowazungumzia wauza madawa ya kulevya ambao wamewahi kuishi katika hii dunia basi hutoweza kuliacha jina la mshikaji huyu, Mmarekani, ‘bitozi’, bilionea ambaye utajiri wake mkubwa ulitokana na uuzaji wa madawa ya kulevya.

Jamaa alivuma sana miaka ya mwishoni mwa mwaka 1960 na mwanzoni mwa mwaka 1970. Jamaa alikuwa na washikaji wengi waliokuwa wakipiga biashara hii haramu. Kila siku, alisafirisha madawa ya kulevya kupitia kwenye majeneza ya watu aliokuwa akiwaua na washikaji zake.

Mwaka 1975, jamaa alivamiwa nyumbani kwake, ndani ya nyumba tu kukakutwa kiasi cha dola laki tano (zaidi ya bilioni moja), kwa kipindi hicho, kilikuwa kiasi kikubwa sana cha fedha. Jamaa alipokamatwa, akafungwa gerezani miaka 75 kwa kesi zaidi ya 100 za madawa ya kulevya.

Dudus-Coke.jpg


CHRISTOPHER COKE AKA: “Dudus”

Jamaa alikuwa mpiga dili mkubwa tu kwenye biashara ya madawa ya kulevya. Alikuwa Mjamaika, mwenye sura ya kipole, kusaidia watu ambapo baada ya kugundulika kwamba anafanya biashara hiyo, hakutaka hata kutafutwa, mwenyewe akajipeleka polisi mwaka 2010.

Mshikaji aliingiza kiasi kikubwa cha fedha, mpaka kukamatwa kwake alikuwa ameingiza kiasi cha dola bilioni 30 (zaidi ya trilioni 60) ambapo kwa sasa tungesema kwamba yeye ni tajiri wa 18 duniani.

Japokuwa alikuwa na ubaya wake wa kufanya biashara hiyo haramu lakini mshikaji alikuwa mtu wa watu. Alikuwa akijenga hospitali, kufanya biashara nyingine na kuwaajiri watu wengi, aliwasaidia masikini na kuwafurahisha kwa kuyaboresha mazingira yao japokuwa upande wa nyuma, aliteketeza vijana kwa kuwauzia biashara hiyo.

reina400.jpg


GRISELDA BLANCO AKA: “The Cocaine Godmother”


Unaweza kumchukulia poa tu kwa sababu ni mwanamke lakini ni lazima ujue kwamba kwa watu waliokuwa wakifanya biashara ya kulevya kwa kiasi kikubwa huwezi kumuacha huyu mwanamke.

Alikuwa mtu wa dili, mbali na uuzaji wa madawa hayo, pia alikuwa muuaji mzuri tu ambaye kwa kipindi chote cha kufanya biashara yake, aliwaua watu 200 kwa risasi, tena kwa mkono wake mwenyewe.

Baada ya kufanya biashara hiyo kwa miaka kadhaa, akakamatwa na kufungwa miaka 20 gerezani, ila cha kushangaza sasa, akiwa hukohuko nyuma ya nondo, michongo yake ya biashara ilikuwa ikisonga kama kawa.

Mwaka 2004 akatolewa gerezani lakini ilipofika mwaka 2012, akauawa kwa kupigwa risasi na mshikaji aliyekuwa akiendesha pikipiki. Huo ukawa mwisho wake, akazikwa ingawa bado anajulikana kama mfanyabiashara mkubwa wa biashara hiyo haramu.

MellyLee-Freeway-RickRoss-4.jpg


Rick Ross AKA: “Freeway”

Siyo huyu unayemjua wewe! Siyo yule jamaa mwenye mwili mkubwa, mwanamuziki wa Kimarekani, achana na huyo, mshikaji mwenyewe alilichukua jina la Rick Ross kutoka kwa huyu jamaa.

Mwili mdogo, mtanashati, alipenda kutabasamu lakini nyuma ya tabasamu lake, jamaa alikuwa ‘mbaya’ kwenye biashara ya madawa ya kulevya.

Jamaa alianza kufanya biashara hiyo miaka ya 1980. Alianza kama ‘punda’ yaani mbebaji lakini baadaye akajizatiti na kuwa na biashara yake mwenyewe. Jamaa alikuwa akiuza mzigo wa dola milioni 3 (zaidi ya bilioni 6) kila siku iendayo kwa Mungu. Mshikaji alikuwa akiuza kilo 400 kila wiki.

arturo-beltran-leyva-muerto-narco-cuernavaca.jpg



Arturo Beltrán Leyva AKA: “Boss of Bosses”

Kama washikaji wa hapo juu, hata huyu mwana alikuwa nuksi kwenye uuzaji wa madawa ya kulevya. Mshikaji alikuwa na kundi lake liitwalo Beltran Leyva Cartel, kundi lililosumbua sana nchini Mexico.

Kulikuwa na kesi nyingi dhidi ya kundi hilo, watu walikuwa wakiuawa, wanawake walibakwa, walisafirisha sana silaha kwenda sehemu mbalimbali, wengine waliteswa na kutekwa. Kwa kifupi, kundi hili lilikuwa hatari zaidi kuliko makundi mengine yaliyowahi kutokea huko.

Jamaa aliuawa na wanajeshi wa majini mwaka 2009 katika majibizano ya kurushiana risasi na wanajeshi hao.

776e756c0a1c6c3c9e6ed7eea93ab0b7.jpg


Felix Mitchell AKA: “The Cat”

Jamaa alikuwa si kitoto, huyu ni miongoni mwa wauza madawa ya kulevya wakubwa waliowahi kutokea duniani. Alikuwa na kundi lake liitwalo 69 Mob. Jamaa alikuwa akipiga dili za chinichini, ilikuwa vigumu kukamatwa kwani alikuwa mjanja kupindukia.

Alipokamatwa, alifungwa jela miaka mingi tu ila wakati akiwa ametumikia kifungo kwa miaka miwili, kuna jamaa hukohuko jela akamuua kwa kumchoma kisu, hiyo ilikuwa mwaka 1986 na mazishi yake yalihudhuriwa na watu wengi, sawa na mazishi ya aliyekuwa mwanaharakati, Martin Luther King Jr.

bcc6bda7cbceb497c66dfeb6dca608f6.jpg



Amado Carrillo Fuentes AKA: “Lord of the Skies”

Alikuwa Mmexico aliyekuwa akifanya biashara ya madawa ya kulevya kwa kiasi kikubwa. Hakuwa mkuu wa kitengo, aliajiriwa na bosi wake aliyeitwa Rafael Aguilar Guajardo ila akaamua kumuua na kushikilia yeye hicho kitengo.

Ndiye muuzaji pekee wa madawa ya kulevya aliyekuwa akiingiza kiasi kikubwa nchini Marekani kuliko mtu yeyote.

Alikuwa bilionea, mwenye kupenda watu na kusaidia masikini. Hakuwa na utani katika biashara hiyo, aliua wote aliohisi kwamba walikuwa watu wabaya katika biashara yake.

Alitumia ndege zake kusafirisha madawa ya kulevya kwenda nchini Marekani mara nne kwa siku. Kumkamata haikuwa kazi nyepesi kwa sababu alikuwa akibadilisha sura yake kwa kuvaa sura ya bandia.

Mwaka 1997 alipokuwa akifanyiwa upasuaji wa kuwekewa sura ya bandia katika Hospitali ya Santa Monica nchini Mexico, dawa zilizidi hivyo kufariki dunia na baada ya siku mbili, wale madaktari waliofanya upasuaji huo wa kumuwekea sura ya bandia wakakutwa wameuawa kinyama na miili yao kutupwa.

legendary-drug-lord-pablo-escobar-lost-21-billion-in-cash-each-year--and-it-didnt-matter.jpg


Pablo Escobar AKA: “The World’s Greatest Outlaw”
Huyu jamaa alikuwa kiboko, ni Mcolombia aliyekuwa akiuza madawa ya kulevya kwa kiasi kikubwa. Alikuwa katili, kuua watu waliokuwa kinyume naye ilikuwa ishu ndogo sana kwake.

Hakutaka mchezo, hakuwahi kuweka fedha benki, alikuwa akizihifadhi ndani na wakati mwingine zilikuwa zikiliwa na panya. Kuna kipindi mtoto wake alikuwa akiumwa, alizitumia dola za Kimarekani kumuwashia moto, eti kupoza baridi lililokuwa likimpiga, kitu kilichowakasirisha sana Wamarekani, waliona wamedharauliwa sana mpaka noti yao kuchomwa moto.

Alikuwa na utajiri mkubwa na mwaka 1989 alitangazwa kama tajiri wa saba duniani akiwa na utajiri wa dola bilioni 25 (zaidi ya shilingi trilioni 50). Jamaa alikuwa akimiliki 4/5 ya soko kubwa la madawa ya kulevya duniani.

Jamaa alikuwa akisafirisha tani 15 za madawa ya kulevya kila siku barani America. Jamaa aliua majaji 30 waliokuwa wakisimamia kesi zake na polisi 400 ambao walionekana kimbelembele kumfuatilia kwenye mishe zake na pia aliilipua ndege aina ya Avianca Flight 203 ambayo ilikuwa ikimbeba waziri mkuu wa kipindi hicho nchini Colombia.

Kwa kifupi, jamaa alikuwa na pesa ndefu kiasi cha kuiambia serikali yake kwamba imuache afanye mishe zake kwani angelipia deni la dola bilioni 20 (zaidi trilioni 40) lililokuwa ikidaiwa, ila serikali ikakaata na kumuua.

183386-004-BBC389E6.jpg


Joaquín Guzmán Loera AKA “El Chapo Guzmán”


Hapa ndipo kwenye kazi sasa. Huyu anaonekana kama mwamba wa biashara hii ya madawa ya kulevya. Ni Mmexico mwenye mkwanja mrefu ambapo amekuwa akiupata kupitia biashara yake haramu.

Alikuwa mtu anayetafutwa kwa nguvu zote kabla ya kukamatwa. Aliwekeza nguvu kubwa katika biashara hii, Wamarekani na Wamexico walimtafuta lakini hawakumpata.

Wakati wakiwa na uchungu naye, wakafanikiwa kumpata na hivyo kufungwa nchini Mexico. Kutokana na fedha alizokuwa nazo, inasemekana kwamba aliwahonga askari magereza na kutoroka kwa kupitia katika bomba la choo, unaamini hilo?

Wamarekani walikasirika sana, wakaahidi kumtafuta, kweli wakaingia mzigoni. Hawakuchukua muda sana, wakamnasa na hivyo kuiambia Serikali ya Mexico kwamba watamfunga wao wenyewe ili wamuonyeshee kwamba wao si watu wa mchezo, kweli wakamfunga na mpaka leo hii yupo gerezani akiendelea kutumikia kifungo chake ambacho hakikuwekwa wazi ni cha muda gani.
 
Beka renja anashika nafasi ya ngapi hapo.

Ila Pablo Escobar Bavilio anaongoza.
 
Colombia na mexico ndiyo top iliyotoa sana top ya wauza unga.unga unaoingia marekani asilimia kubwa unatoka mexico na kama ukija kucheki list marekani ipo top 3
 
Back
Top Bottom