Hawa ndiyo wahadhiri Rais Magufuli aliowachukua pale UDSM kwa mbwembwe ambao wamefeli vibaya

G Sam

JF-Expert Member
Apr 20, 2013
11,555
35,880
Hawa ndiyo wahadhiri ambao Rais Magufuli aliwatoa pale UDSM kwa mbwembwe ili wamsaidie lakini wote pamoja na aliyewachukua wamefeli. Ajabu ni kuwa pale UDSM walikuwa walimu wazuri sana.

1. Alianza kumvuta Dr. Mussa Mgwatu kutoka Engineering. Huyu Dr. Pale UDSM alisifika sana kwa kuwa eneo la kazi muda wote na kuwajibika. Alimvuta kuwa Mkurugenzi mkuu wa TEMESA ila aliishia kumtumbua baada ya kivuko cha Ukerewe kilichozama Ukara na kuua watu wengi. Kwa sasa naamini atakuwa karudi zake UDSM na anawahi kazini kama kawaida. Aidha alimsaidia sana Magufuli kwenye masomo yake pale UDSM.

2. Dr. Titto Mwinuka: Huyu na Dr. Mgwatu ni marafiki sana na wote walikuwa wanashinda pale workshop za UDSM wakipiga ishu ndogo ndogo za "Fabrications" na walivutwa wote kipindi kimoja aidha wote walimsaidia sana Magufuli wakati anasoma. Huyu ni mkurugenzi mkuu wa Tanesco ingawa ni rafiki yangu sana ila sioni tija anayofanya pale zaidi ya Mramba. Kinachomlinda ni kuwa hajapata janga.

3. Maprofesa Ussoro na Mruma wa CoNAS. Hawa walishiriki kwenye tume za kuchunguza ubadhirifu wa madini na wakaja na ripoti zilizoandikwa na magazeti yote pamoja na kutangazwa live huku tukimshuhudia Prof. Mruma akitokwa machozi wakati akisoma ripoti yake. Ilikuwa mwaka 2016 ila hadi leo hakuna jipya lililotokea na zaidi yale makontena ya makinikia pale bandarini yamejengewe uzio yako pale tu bila kufanyiwa chochote.

4. Prof. Lorence Luoga. Huyu akiwa pale kitivo cha sheria alikuwa mwalimu mzuri sana. Magufuli akamvuta akampeleka kwenye tume alipokuja na ripoti ya kumpendeza akaamua amkabidhi majukumu pale BoT ili akaishughulikie hiyo ripoti. Ajabu hajaweza kufanya hata robo ya kazi aliyoifanya Beno Ndulu huku akiwa Gavana wa kwanza kutumia majeshi ya JWTZ katika kazi zake za kifedha.

5. Prof. Palamagamba Kabudi. Nadhani wengi wetu ni mashahidi kuwa huyu Prof. alikuwa na kiburi sana kiasi cha kuipuuza Law School of Tanzania. Pia kwenye degree yake ndiye mwanafunzi aliyegomea B+ aliyopewa na Mgongo Fimbo akidai kuwa alistahili alama A. Mgongo Fimbo akasema hajawahi kumpa mwanafunzi A maana atakuwa katunga naye mtihani. Pia huyu Prof. Baada ya kuletewa wanafunzi wa TCU kipindi hicho akiwa mkuu wa kitivo aliwatisha kuwa baada ya muda mfupi wale wa TCU wataondoka na watabaki wanafunzi wa UDSM... Alivutwa na Magufuli kuwa waziri wa sheria wakaja vijana wa CCM wakidai eti Lissu amepata mwalimu wa sheria bungeni. Badala ya kumshinda Lissu kwa hoja wakamshinda wa mtutu. Baadaye alihamishwa wizara anayoimudu na kupelekwa ugenini. Kwasasa kwenye vikao vya Baraza la mawaziri ni mwalimu mzuri wa mistari ya Biblia!

6. Prof. Kitila Mkumbo.. Huyu yupo wizara ya maji ila kwa sasa ni mtunzi mkuu wa mapambio ya kumsifu Mkubwa kwenye magazeti.

Pamoja na hayo pia Magufuli ameualia mbali vipaji vya wanasiasa wazuri kama Dr. Slaa (Ambaye kwa sasa kule Karatu akiitisha mkutano hapati hata watu 100), Kafulila, Katambi na wengine wengi.


Waliojitenga naye tunawaona...Au tuseme tena?
 
Mimi naona serikali ianze kutumia mfumo wa applications. Tumeni vigezo vyenu mnavyotaka then watu watume CV zao na nini wanachopanga kufanya ili kuleta mabadiliko katika sekta husika. Yaani mfumo uwe huru na competitive ili kupata best Thinkers and doers.

Kuna sekta na wizara ambazo zinahitaji watu walio business minded mfano maliasili na utalii. Sasa mwisho wa siku tunachukua wabunge randomly au kuwateua academicians ambao maisha yao yote yapo vitabuni tu halafu tunategemea maajabu !!!!...
 
Mkuu hao anaowafelisha ni magufuli mwenyewe.Magufuli haruhusu wataalam kufanya maamuzi yao.Anataka wafanye yale anayoona ni mema machoni pake.Ndio maana utaona mtu kama kabudi wa 2014,si wa 2019.Na unafiki uliojadi ya watanzania ndio unaowatafuta wakina Mtatiro,Katambi,slaa,Kafulila n.k.saizi kafulila uwezo aa kuchambua mambo anazidiwa hata na mkewe mama Jesca kishoa
 
Prof Luoga naona kama unamuonea, bila crackdown kwenye yale maduka ya kubadilishia fedha basi shilingi ingeendelea kuchezewa na wahujumu uchumi wachache huku nchi nzima tukiumia. Kwasasa shilingi iko 'stable', ukipanga bajeti leo unauhakika miezi mitatu ijayo hela yako itatosha kutekeleza bajeti yako.
 
Ukipata kitabu kinaitwa "Peter's Princople" utapata majibu ya kwa nini iko hivyo
Summary
tumblr_mz04vmp5p01su40qeo1_500.jpeg
Figure%201%20-%20Peter%20Principle.jpeg
 
Hawa ndiyo wahadhiri ambao Rais Magufuli aliwatoa pale UDSM kwa mbwembwe ili wamsaidie lakini wote pamoja na aliyewachukua wamefeli. Ajabu ni kuwa pale UDSM walikuwa walimu wazuri sana.

1. Alianza kumvuta Dr. Mussa Mgwatu kutoka Engineering. Huyu Dr. Pale UDSM alisifika sana kwa kuwa eneo la kazi muda wote na kuwajibika. Alimvuta kuwa Mkurugenzi mkuu wa TEMESA ila aliishia kumtumbua baada ya kivuko cha Ukerewe kilichozama Ukara na kuua watu wengi. Kwa sasa naamini atakuwa karudi zake UDSM na anawahi kazini kama kawaida. Aidha alimsaidia sana Magufuli kwenye masomo yake pale UDSM.

2. Dr. Titto Mwinuka: Huyu na Dr. Mgwatu ni marafiki sana na wote walikuwa wanashinda pale workshop za UDSM wakipiga ishu ndogo ndogo za "Fabrications" na walivutwa wote kipindi kimoja aidha wote walimsaidia sana Magufuli wakati anasoma. Huyu ni mkurugenzi mkuu wa Tanesco ingawa ni rafiki yangu sana ila sioni tija anayofanya pale zaidi ya Mramba. Kinachomlinda ni kuwa hajapata janga.

3. Maprofesa Ussoro na Mruma wa CoNAS. Hawa walishiriki kwenye tume za kuchunguza ubadhirifu wa madini na wakaja na ripoti zilizoandikwa na magazeti yote pamoja na kutangazwa live huku tukimshuhudia Prof. Mruma akitokwa machozi wakati akisoma ripoti yake. Ilikuwa mwaka 2016 ila hadi leo hakuna jipya lililotokea na zaidi yale makontena ya makinikia pale bandarini yamejengewe uzio yako pale tu bila kufanyiwa chochote.

4. Prof. Lorence Luoga. Huyu akiwa pale kitivo cha sheria alikuwa mwalimu mzuri sana. Magufuli akamvuta akampeleka kwenye tume alipokuja na ripoti ya kumpendeza akaamua amkabidhi majukumu pale BoT ili akaishughulikie hiyo ripoti. Ajabu hajaweza kufanya hata robo ya kazi aliyoifanya Beno Ndulu huku akiwa Gavana wa kwanza kutumia majeshi ya JWTZ katika kazi zake za kifedha.

5. Prof. Palamagamba Kabudi. Nadhani wengi wetu ni mashahidi kuwa huyu Prof. alikuwa na kiburi sana kiasi cha kuipuuza Law School of Tanzania. Pia kwenye degree yake ndiye mwanafunzi aliyegomea B+ aliyopewa na Mgongo Fimbo akidai kuwa alistahili alama A. Mgongo Fimbo akasema hajawahi kumpa mwanafunzi A maana atakuwa katunga naye mtihani. Pia huyu Prof. Baada ya kuletewa wanafunzi wa TCU kipindi hicho akiwa mkuu wa kitivo aliwatisha kuwa baada ya muda mfupi wale wa TCU wataondoka na watabaki wanafunzi wa UDSM... Alivutwa na Magufuli kuwa waziri wa sheria wakaja vijana wa CCM wakidai eti Lissu amepata mwalimu wa sheria bungeni. Badala ya kumshinda Lissu kwa hoja wakamshinda wa mtutu. Baadaye alihamishwa wizara anayoimudu na kupelekwa ugenini. Kwasasa kwenye vikao vya Baraza la mawaziri ni mwalimu mzuri wa mistari ya Biblia!

6. Prof. Kitila Mkumbo.. Huyu yupo wizara ya maji ila kwa sasa ni mtunzi mkuu wa mapambio ya kumsifu Mkubwa kwenye magazeti.

Pamoja na hayo pia Magufuli ameualia mbali vipaji vya wanasiasa wazuri kama Dr. Slaa (Ambaye kwa sasa kule Karatu akiitisha mkutano hapati hata watu 100), Kafulila, Katambi na wengine wengi.


Waliojitenga naye tunawaona...Au tuseme tena?
Mh!!!
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Back
Top Bottom