Hawa ndiyo wabunge wa viti Maalum CHADEMA, CCM na CUF

Kinachozungumzwa hapa ni jinsi ya kujipanga kuenea kwa vuguvugu la mageuzi nchi nzima na si swal la bora mwakilishi. Kuna sehemu ambazo chama hakijaijeng saaana lakini mgombea wake labda amepata kura nying za kumfanya awe wa pili, basi jimbo au mkoa huo watafute mwanachama wa huko anyeweza kukijenga chama. Wa huko sina maana ya kabila bali ukazi.
Bahati mbaya CHADEMA hawakusikilizwa walipopinga utaratibu wa kupeleka majina tume hata kabla ya uchaguzi. hili ndilo linalotakiwa libadilishwe ili vyama viweze kuweka mikakati ya uchaguzi ujao. Ni wazo zuri ila lisitazamwe kama kwamba utaratibu huu utumike irresponsibly na wala wale ambko CHADEMA ndio stronghold wasijisikie kunyang'anywa mkate. Tuweke ujenzi wa chama nchi nzima mbele.
 

Kaka naona umesahau kuwa chadema ni chama cha kaskazini. Ukabila kwanza, vingine baadaye. Kwa hili wanadhihirisha wazi kuwa wangeshika nchi wachaga wote na wapare wangekuwa ni viongozi wa nchi hii katika kila taasisi. Lakini Mungu ameyaona haya mapema.

Hatudaganyikiiiiiii.:nono:
 
Nakuonea hruma sana kwa mtazamo wako.
Ila kama ukiamua, waweza pia kuita Mbeya kaskazini, hata Kigoma pia. Unaweza pia kuita Mramba anaekumbatiwa na CCM mkwere vilevile, au muslamu, ni hiari yako.
 
Angalieni mgawanyo usije ukaleta malalamiko ya ukabila........tunajua mikoa ambayo ina upinzani wa kweli km....mbeya,kilimanjaro,arusha,mwanza,kigoma,mara,dar,rukwa,iringa............ni vizuri pia wakachaguliwa kuzingatia nguvu hii ya umma ili kuepusha malalamiko
you are more than 100% right. Wakuu katika chadema, tekelezeni. Ni muhimu
 
Hivi Reggia mtema amechaguliwa kuwa mbunge wa kilombero? maana wengine wanasema wameshinda CCM.msaada wa data pls
 
Utaratibu ni kuwa kila mbunge wa jimbo(wa kuchaguliwa ) anaingiza wabunge wawili wa viti maalum.
kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Acha kudanyawa watu. Mwaka 2005 Chadema ilipata wabunge 4, ikapewa mmoja wa viti maalum wakawa watano, hiyo katiba yako in draft au inayotumika?
 
Acha kudanyawa watu. Mwaka 2005 Chadema ilipata wabunge 4, ikapewa mmoja wa viti maalum wakawa watano, hiyo katiba yako in draft au inayotumika?

Wewe mbona pia watudanganya? No research no right to speak!! For your information CHADEMA ilishinda majimbo matano na wakapata viti maalum sita na hivyo kuwa na wabunge 11 na moto wake kila mtu aliuona!!
 
Viti maalumu hutokana na uiano wa kura. kwa hiyo ccm mwaka huu wamelimia nyani,watavuna mabua. idadi yao itashuka sana.

Ngandema ndio maana sasa hivi wanachakachua kura za uraisi ili wapate asilimia kubwa.
 
Naona sasa tunaanza kuihalibu jamii forum, kwamba hoja inayoiponda serikali au chama tawala ndio inafaa. kama unataka kuongelea kushuka na kupanda ongelea vyama vyote ili uwe balanced.
 
wana matumaini makubwa hata wewe hujawaona leo pale JK akiapishwa walivyokuwa wanashangilia ....wanajua shavu lipo mlangoni
 
Hii ndiyo hoja ya msingi,hapa tunachotaka ni kwa CHADEMA kupingana kwa kila hali na mfumo huu mbovu na wao pia wasiingilie uhuru wa wanawake wa chama chao kuchaguwa watu wa kuwawakilisha hata kwa kisingizio gani kile.

Kama wanawake wao wamekosea kuchagua au uchaguzi wao umeingiliwa na rushwa basi chama kisahihishe makosa hayo lakini mwisho wa siku ni wanawake wenyewe wapewe nafasi ya kuchagua wawakilishi wao,
 
Na bado kuna vile walivyochukua kwa nguvu lazima tuvirudishe mujengoni kupitia The Hague
 
Jamani kila chama kina mfumo wake. Uongozi ni zaidi ya hii vita ya madaraka wanayoifanya sisi m jambo ambalo naona wengi hapa wanataka kuja nalo Chadema.

Limeshazungumzwa hapa kwamba utaratibu huo wa kuchaguana wanawake ulileta shida kiasi ambacho tungepata shida walizopata sisi m na sisi kufaidi kwa ugomvi wao. Uongozi imara na wenye busara wa Chadema ukabuni namna yao. Ukatengeneza kamati itakayoshughulikia jambo hili. Na nina hakika hata wakina mama walihusishwa katika kamati hiyo iliyokuwa chini ya Dr Kitila. Msitake kuwapotosha watu hapa na kuzalisha vita ya ki sisi m katika kura za maoni.

Waachie Chadema yao, mwenye ushauri na aweke komenti zake kwenye website yao
Tovuti ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na watayaangalia.

Hata hivyo ushauri wenu ni chachu kwa maendeleo ya Chadema ingawa chama hakilazimiki kukubaliana nao.
 
Conjesta Rwamlaza
Mwenyekiti wa Chadema kwa muda mrefu tangu kuundwa kwa Chadema mkoani Kagera na sana ni Katibu wa Chama hicho mkoani Kagera. Ni mama mpambanaji, asiyeogopa lolote, jasili wa kukabiliana na dhoruba za aina yoyote. Amekibeba chama hiki Kagera usiku na mchana.

Naomi Kaihula
Mama huyu alikuwa akigombea ubunge katika moja ya majimbo ya Dar-es-salaam ni mwalimu kitaaluma na amekuwa akifundisha katika moja ya shule za sekondari Dar.
 
Leo hinategemewa kutangaza idadi ya viti maalum kwa kila chama.By facebook mr Zitto :israel::israel::israel::israel::israel::israel::israel::israel:kwa hiyo 22+32 Jumla 54 Chadema kitakuwa chama cha upinzani bungeni kwa hiyo idadi ya viti maalum vya ccm vimepunua sana kutoa viti 80 walivyokuwa navyo Idadi hiyo hinatokana na kura za wabunge nchi nzima.sio kra za rais au viti vya wabunge
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…